Natasha Lisimo - Umwema Lyrics

Umwema Lyrics

Hey yeah yeah .... Wewe ni mwema

Niliyovuka ni mengi
Siwezi tazama nyuma
Kwa visa vingi vitimbwi
Aaai, asante Baba

Si kwa akili zangu
Wala nguvu zangu mwenyewe
Wewe ni mwema
Umenuivusha na mengi magumu
Yanayoelezeka na yasiyoelezeka
Umenifuta maumivu
Ukanipa amani

Wa ajabu, fahari yangu
Mtetezi wangu, wewe ni mwema
Mwalimu wangu, shujaa wangu
Kiongozi wangu wewe ni Baba

Oooh oooh ...umenikunguta mavumbi wewe ni mwema
Oooh oooh ...umenipandisha pandisha wewe ni Baba
Oooh oooh ...umenifanya chombo cha sifa kwa walimwengu
Oooh oooh ...umenipandisha pandisha wewe ni mwema

Ungetazama vyeo
Uzuri na mali mimi ningekuwa wapi?
Kiukweli upendo wako hauna kipimo
Umenipenda bure
Kwa kupigwa kwako mimi nimepona
Neema yako ya kweli ya ajabu

Umenifanya mwanao
Ukanipa uzima na afya
Umenifuta maumivu (eh)
ukanipa amani
Wa ajabu, fahari yangu
Mtetezi wangu, wewe ni mwema
Mwalimu wangu, shujaa wangu
Kiongozi wangu wewe ni baba

Oooh oooh ...umenikunguta mavumbi wewe ni mwema
Oooh oooh ...umenipandisha pandisha wewe ni Baba
Oooh oooh ...umenifanya chombo cha sifa kwa walimwengu
Oooh oooh ...umenikunguta mavumbi wewe ni mwema

Wewe ulikuwa mwanzo
Na bado utabaki kuwa mwisho
Kwenye utata na vikwazo
Bado utabaki sukuhisho

Wewe ni taa na mwanga
Humulika popote palipo na giza
Maana hakuna jambo gumu ambalo wewe bwana unashindwa

Umenipa amani (aaah hey)
Umenipa furaha(aah hey)
Jemedari (aah hey)
Yesu nakupenda

Umenipa uzima (aaah hey)
Umenipa heshima(aah hey)
Yesu weeeh (aah hey)
Bwana nakusifu

Oooh oooh ...umenikunguta mavumbi wewe ni mwema
Oooh oooh ...umenipandisha pandisha wewe ni Baba
Oooh oooh ...umenifanya chombo cha sifa kwa walimwengu
Oooh oooh ...umenipandisha pandisha wewe ni mwema

 


Umwema Video

Natasha Lisimo Songs

Related Songs