Natasha Lisimo - Umwema Lyrics

Lyrics

Hey yeah yeah .... Wewe ni mwema

Niliyovuka ni mengi Siwezi tazama nyuma Kwa visa vingi vitimbwi Aaai, asante Baba

Si kwa akili zangu Wala nguvu zangu mwenyewe Wewe ni mwema Umenuivusha na mengi magumu Yanayoelezeka na yasiyoelezeka Umenifuta maumivu Ukanipa amani

Wa ajabu, fahari yangu Mtetezi wangu, wewe ni mwema Mwalimu wangu, shujaa wangu Kiongozi wangu wewe ni Baba

Oooh oooh ...umenikunguta mavumbi wewe ni mwema Oooh oooh ...umenipandisha pandisha wewe ni Baba Oooh oooh ...umenifanya chombo cha sifa kwa walimwengu Oooh oooh ...umenipandisha pandisha wewe ni mwema

Ungetazama vyeo Uzuri na mali mimi ningekuwa wapi? Kiukweli upendo wako hauna kipimo Umenipenda bure Kwa kupigwa kwako mimi nimepona Neema yako ya kweli ya ajabu

Umenifanya mwanao Ukanipa uzima na afya Umenifuta maumivu (eh) ukanipa amani Wa ajabu, fahari yangu Mtetezi wangu, wewe ni mwema Mwalimu wangu, shujaa wangu Kiongozi wangu wewe ni baba

Oooh oooh ...umenikunguta mavumbi wewe ni mwema Oooh oooh ...umenipandisha pandisha wewe ni Baba Oooh oooh ...umenifanya chombo cha sifa kwa walimwengu Oooh oooh ...umenikunguta mavumbi wewe ni mwema

Wewe ulikuwa mwanzo Na bado utabaki kuwa mwisho Kwenye utata na vikwazo Bado utabaki sukuhisho

Wewe ni taa na mwanga Humulika popote palipo na giza Maana hakuna jambo gumu ambalo wewe bwana unashindwa

Umenipa amani (aaah hey) Umenipa furaha(aah hey) Jemedari (aah hey) Yesu nakupenda

Umenipa uzima (aaah hey) Umenipa heshima(aah hey) Yesu weeeh (aah hey) Bwana nakusifu

Oooh oooh ...umenikunguta mavumbi wewe ni mwema Oooh oooh ...umenipandisha pandisha wewe ni Baba Oooh oooh ...umenifanya chombo cha sifa kwa walimwengu Oooh oooh ...umenipandisha pandisha wewe ni mwema

 

Video

Natasha Lisimo UMwema

Thumbnail for Umwema video
Loading...
In Queue
View Lyrics