Sifa Lyrics

Asante by Natasha Lisimo cover art

Natasha Lisimo - Asante Lyrics

Artist:
Natasha Lisimo

Lyrics

Ni rahisi moyo lawama linapotokea mbaya 


Ninasahau hayo yote ni mpango wako 


Ninapata shida kichwani ninachanganyikiwa 


Nikumbushe wema wako, wakati wote nikuabudu 


Nikusifu kwa hali zote nisiende mbali nawe 


Wakati wote niwe nawe (Baba) 


Machozi yangu yafute (Mungu)


Wakati wote niwe nawe (Bwana) 


Machozi yangu yafute (Mungu)


Ni wewe ndiwe mfariji wapekee 


Baba wa yatima, mume wa wajane 


Niwezeshe kustahimili kiangazi na masika 


Pepo mbaya na mzuri pale unaponipitia 


Nisimame mbele zako milele milele 


Nishike na mkono wako daima daima 


Maana kila litokalo wewe umepanga litokee 


Sio kwamba nia yako tupotee ila tuzidishe imani 


Wakati wote niwe nawe (Baba) 


Machozi yangu yafute (Mungu)


Wakati wote niwe nawe (Bwana) 


Machozi yangu yafute (Baba) 


Asante kwa yote (Baba) 


Nimekuwa jasiri (Asante) 


Asante kwa yote mema 


(asante kwa yote) 


Kwa utukufu wako (asante) 


Asante Baba (asante) 


Pokea moyo shukurani (asante kwa yote) 


Oh Baba (asante ) 


Nakushukuru kwa njia zako (asante) 


Nakushukuru kwa matendo yako (asante)


Video