Joel Lwaga - Muda Lyrics
Lyrics
Here are the lyrics for "Muda" by Joel Lwaga:
[Verse 1] Jitu Ni kweli naonekana niko Nyuma Kila kukicha watu washamiri, kwa magari majumba Juzi juzi wengine tulikuwa nao sawa tu Ila kwa sasa si wenzangu tena, siwagusi hata nukta Ni kama niko duniani kuwasindikiza wao Usipotulia unaweza sema Mungu ni wa peke yao Ila maisha ni kama foleni inajongea Mdogo Mdogo Mungu wao ndio Mungu wangu, ndio wa Isaka na Yakobo
[Pre-Chorus] Wakati na Bahati huwapata wote Zamu yangu itafika, Wacha niingojee La maana ni uhai, Mungu ni wote Ndio anapanga aanze nani, nani afuate
[Chorus] Yani ni suala la Muda MUDA, nipeni tu MUDA Mungu ni wa wote jamani MUDA, nipeni tu MUDA Yani ni suala la Muda MUDA, nipeni tu MUDA Kikubwa niko kwa foleni MUDA, nipeni tu MUDA
[Verse 2] Najua wengi husema kila asiyenacho hunyenyekea Ila nimemwomba Mungu nisibadilike Akinipea Vile nawaona Watu na kuwachukulia nikiwa Sina Nisije jiona Mungu mtu pindi mambo yakininyookea Najitahidi kugawana hichi kidogo Nilichonacho na wenzangu Nimejifunza kwamba kutoa ni Moyo siyo mpaka kiwe kingi changu Kwenye sadaka sinaga visingizio hio ni kama Pai kwangu Hata nikiwa sina kabisa siku hyo, Mungu anaujua Moyo wangu
[Pre-Chorus] Wakati na Bahati huwapata wote Zamu yangu itafika, Wacha niingojee La maana ni uhai, Mungu ni wote Ndio anapanga aanze nani, nani afuate
[Chorus] Yani ni suala la Muda MUDA, nipeni tu MUDA Mungu ni wa wote jamani MUDA, nipeni tu MUDA Yani ni suala la Muda MUDA, nipeni tu MUDA Kikubwa niko kwa foleni MUDA, nipeni tu MUDA Yani ni suala la Muda MUDA, nipeni tu MUDA Mungu ni mwaminifu MUDA, nipeni tu MUDA
[Bridge] Maana maisha ni foleni Kila siku inatembea pole pole Namwamini Mungu ipo siku nitafanikiwa Maana maisha ni foleni Kila siku inatembea pole pole Namwamini Mungu ipo siku nitafanikiwa
[Outro] Kweli ni suala la Muda MUDA, nipeni tu MUDA Mungu ni mwaminifu jamani! MUDA, nipeni tu MUDA
Video
Joel Lwaga - Muda (Lyric Video)