Goodluck Gozbert - Kampeni Lyrics

Lyrics

Waliponikaribia na kuniaibisha eeh Haukunyamaza ukanipigania eeh Waliponivua utu na kulichana vazi langu Na heshima ulinikumbatia nisiaibike

Waliposema mi mjinga, ujinga ninao Sababu hekima haiezi bila upendo Nilipoyafunika madhaifu yao Na kumbe tafsiri ni mjinga kwao

Hata nilipokaa kimya wewe uliona yote Uliponyamaza hukuacha nife Ninakushukuru ooh, ooh Jire Dumo Asante, ooh, oooh Igwe

Nitafanya kampeni za wema wako Wajue Mungu ni mwema Nitafanya kampeni za wema wako Wajue Yesu ni mwema

Unaponibariki bariki adui zangu Ili wasinisonge kutaka uhai wangu Unapopiga mapigo samehe rafiki zangu Wanaoning'ata alafu wanapuliza puu

Hata nilipokaa kimya wewe uliona yote Uliponyamaza hukuacha nife Ninakushukuru ooh, ooh Jire Dumo Asante, ooh, oooh Igwe

Nitafanya kampeni za wema wako Wajue Mungu ni mwema Nitafanya kampeni za wema wako Wajue Yesu ni mwema

Fadhili zako zadumu kila asubuhi Wewe ni Mungu unayesimamisha mianga angani Pendo lako lanitosha daima Huruma yako imepita fahamu zangu Ninakupenda Yesu, ninakupenda mwamba wangu

Video

GOODLUCK GOZBERT - KAMPENI (Official Video)

Thumbnail for Kampeni video
Loading...
In Queue
View Lyrics