Goodluck Gozbert - Kampeni Lyrics
Lyrics
Waliponikaribia na kuniaibisha eeh Haukunyamaza ukanipigania eeh Waliponivua utu na kulichana vazi langu Na heshima ulinikumbatia nisiaibike
Waliposema mi mjinga, ujinga ninao Sababu hekima haiezi bila upendo Nilipoyafunika madhaifu yao Na kumbe tafsiri ni mjinga kwao
Hata nilipokaa kimya wewe uliona yote Uliponyamaza hukuacha nife Ninakushukuru ooh, ooh Jire Dumo Asante, ooh, oooh Igwe
Nitafanya kampeni za wema wako Wajue Mungu ni mwema Nitafanya kampeni za wema wako Wajue Yesu ni mwema
Unaponibariki bariki adui zangu Ili wasinisonge kutaka uhai wangu Unapopiga mapigo samehe rafiki zangu Wanaoning'ata alafu wanapuliza puu
Hata nilipokaa kimya wewe uliona yote Uliponyamaza hukuacha nife Ninakushukuru ooh, ooh Jire Dumo Asante, ooh, oooh Igwe
Nitafanya kampeni za wema wako Wajue Mungu ni mwema Nitafanya kampeni za wema wako Wajue Yesu ni mwema
Fadhili zako zadumu kila asubuhi Wewe ni Mungu unayesimamisha mianga angani Pendo lako lanitosha daima Huruma yako imepita fahamu zangu Ninakupenda Yesu, ninakupenda mwamba wangu
Video
GOODLUCK GOZBERT - KAMPENI (Official Video)