Emma Omonge - Mungu wa Ishara - Uinuliwe Lyrics

Lyrics

Baada ya kilio furaha sasa aah Mafuta ya shangwe ondoa kuomboleza aah Pahala pa dhihaka leta heshima Majira na nyakati zote unabaki mwaminifu Juu ya neema yako nashangaa ntakulipa nini Uu mwaminifu ee Bwana, eeh Bwana, U mwaminifu, ee Bwana.

Usiyepuuza kilio cha yeyote, wakubwa kwa wadogo Maskini hata tajiri, sikio lako halibagui Ukifuta makosa wala hukumbuki tena Juu ya neema yako nashangaa ntakulipa nini Uu mwaminifu ee Bwana, eeh Bwana, U mwaminifu, ee Bwana.

Uinuliwe Mungu wa Ishara Uinuliwe Mungu wa ajabu Uinuliwe Mungu wa uweza Uinuliwe Mungu wa ushindi

Uinuliwe Mungu wa Ishara Uinuliwe Mungu wa ajabu Uinuliwe Mungu wa uweza Uinuliwe Mungu wa ushindi Uinuliwe,Uinuliwe

Video

Emma Omonge -| Mungu Wa ishara | Official video| [sms]Skiza 5356199 to 811

Thumbnail for Mungu wa Ishara - Uinuliwe video
Loading...
In Queue
View Lyrics