Bahati - Magufuli (Safiri Salama) Lyrics
Lyrics
Nina imani tutaonana tena Tena mmmh
Ila yangu swali? Mbona umeondoka mapema na haukusema Jua linatua kila pande ni manjozi Mwongoza njia umetuacha Magufuli Nani ataitwa mlezi wa wasanii Na simba amsifie? Nani ataleta ndege Tanzania uchumi auinue
Aah mbona umetuacha Aah bado mapema Aah..Magufuli safiri salama Aah mbona umetuacha Aah bado mapema Aah..Magufuli we safiri salama
Bado siamini hatutakuona tena Kwanini baba yo umeondoka mapema Msalimie baba Mzee Jomo Kenyatta Mwambie Kenya imara mwanae anatawala Aah na mzee Odinga naye mpe salamu Mwanaye ni gwiji sasa mwambie atabasamu Umtafute Mzee Moi, umkumbatie Natamani maziwa ya Nyayo iturudie
Aah mbona umetuacha Aah bado mapema Aah..Magufuli safiri salama Aah mbona umetuacha Aah bado mapema Aah..Magufuli we safiri salama
I wish ungejua siku barua ungetuandikia Ila Mungu ndo anapanga pole kwa mama Samia Rafiki yangu babu Tale chawa wako wanaumia Swali mbona ni mapema Afrika inakulilia
Magu aah mbona umetuacha? Aah bado mapema Aah..Magufuli we safiri salama Aah mbona umetuacha? Aah bado mapema Aah..Magufuli we safiri salama
Video
BAHATI - MAGUFULI (SAFIRI SALAMA) OFFICIAL VIDEO