Baba yetu aliye mbinguni, amenifurahisha yakini,
kuniambia mwake chuoni, ya kuwa nami Yesu pendoni.
Anipenda Mwokozi Yesu, anipenda, anipenda;
Anipenda Mwokozi Yesu, anipenda mimi.
Nimuachapo kutanga mbali, yeye yu vivyo, hupenda kweli,
hunirejeza kwake moyoni; kweli yu nami Yesu pendoni.
Anipenda! Nami nampenda; kwa wokovu alionitenda;
akanifia Msalabani, kwa kuwa nami Yesu pendoni.
Haya kujua yanipa raha; kumuamini kuna furaha;
Humfukuza mara shetani, kwona yu nami Yesu Pendoni.
Sifa ni nyingi asifiwazo, moja ni sana katika hizo,
wala siachi, hata Mbinguni, kwimba, "Yu nami Yesu pendoni".