Lyrics
Verse 1
Kama machozi yangeweza kusimulia
namna gani moyo unatunza mengi
Kama machozi yangeweza kusimulia
namna gani moyo unavumilia
Verse 2
Moyo umebeba jeraha zangu
Eeh Moyo umebeba huzuni zangu
Moyo umebeba furaha yangu
Eeh Moyo umebeba ushindi wangu
Pre-Chorus
Kuna muda kinywa kinatabasamu lakini Moyo unalia
Kuna muda macho yanafurahi lakini Moyo unalia
Chorus
Nitaulinda moyo wangu kuliko yote niyalindayo , niyalindayo,
Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima , Za uzima, za uzima
Nitaulinda moyo wangu kuliko yote niyalindayo niyalindayo,
Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima , Za uzima, za uzima
Verse 1 (Reprise)
Kama machozi yangeweza kusimulia
namna gani Moyo unatunza mengi
Kama machozi yangeweza kusimulia
namna gani Moyo unavumilia
Chorus
Linda Moyo wako kuliko yote uyalindayo
Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima
Bridge
MUNGU BABA nifute machozi yangu mimi
Waujua Moyo wangu nigange jeraha zangu nibaki
MUNGU BABA nifute machozi yangu mimi
Waujua moyo wangu nigange jeraha zangu nibaki
Credits & Song Information
Video
Meaning & Inspiration
In this live recording, AIC Chang’ombe Choir reflects on the heart as the place where grief, joy, wounds, and victory are held. The central refrain turns that reflection into a call to guard the heart and a prayer for God’s comfort and healing.