Waebrania 5 Swahili & English

Listen/Download Audio
Waebrania 5 (Swahili) Hebrews 5 (English)

Maana kila kuhani mkuu aliyetwaliwa katika wanadamu amewekwa kwa ajili ya wanadamu katika mambo yamhusuyo Mungu, ili atoe matoleo na dhabihu kwa ajili ya dhambi; Waebrania 5:1

For every high priest, being taken from among men, is appointed for men in things pertaining to God, that he may offer both gifts and sacrifices for sins.

awezaye kuwachukulia kwa upole wao wasiojua na wenye kupotea, kwa kuwa yeye mwenyewe yu katika hali ya udhaifu; Waebrania 5:2

The high priest can deal gently with those who are ignorant and going astray, because he himself is also surrounded with weakness.

na kwa sababu hiyo imempasa, kama kwa ajili ya watu, vivyo hivyo kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi. Waebrania 5:3

Because of this, he must offer sacrifices for sins for the people, as well as for himself.

Na hapana mtu ajitwaliaye mwenyewe heshima hii, ila yeye aitwaye na Mungu, kama vile Haruni. Waebrania 5:4

Nobody takes this honor on himself, but he is called by God, just like Aaron was.

Vivyo hivyo Kristo naye hakujitukuza nafsi yake kufanywa kuhani mkuu, lakini yeye aliyemwambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa. Waebrania 5:5

So also Christ didn't glorify himself to be made a high priest, but it was he who said to him, "You are my Son. Today I have become your father."

kama asemavyo mahali pengine, Ndiwe kuhani wa milele Kwa mfano wa Melkizedeki. Waebrania 5:6

As he says also in another place, "You are a priest forever, After the order of Melchizedek."

Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu; Waebrania 5:7

He, in the days of his flesh, having offered up prayers and petitions with strong crying and tears to him who was able to save him from death, and having been heard for his godly fear,

na, ingawa ni Mwana, alijifunza kutii kwa mateso hayo yaliyompata; Waebrania 5:8

though he was a Son, yet learned obedience by the things which he suffered.

naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii; Waebrania 5:9

Having been made perfect, he became to all of those who obey him the author of eternal salvation,

kisha ametajwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki. Waebrania 5:10

named by God a high priest after the order of Melchizedek.

Ambaye tuna maneno mengi ya kunena katika habari zake; na ni shida kuyaeleza kwa kuwa mmekuwa wavivu wa kusikia. Waebrania 5:11

About him we have many words to say, and hard to interpret, seeing you have become dull of hearing.

Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu. Waebrania 5:12

For when by reason of the time you ought to be teachers, you again need to have someone teach you the rudiments of the first principles of the oracles of God. You have come to need milk, and not solid food.

Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga. Waebrania 5:13

For everyone who lives on milk is not experienced in the word of righteousness, for he is a baby.

Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya. Waebrania 5:14

But solid food is for those who are full grown, who by reason of use have their senses exercised to discern good and evil.