Waebrania BSB

Waebrania 3

Hebrews Chapter 3

1
Kwa hiyo, ndugu watakatifu, wenye kuushiriki mwito wa mbinguni, mtafakarini sana Mtume na Kuhani Mkuu wa maungamo yetu, Yesu,
Therefore, holy brothers, who share in the heavenly calling, set your focus on Jesus, the apostle and high priest whom we confess.
2
aliyekuwa mwaminifu kwake yeye aliyemweka, kama Musa naye alivyokuwa, katika nyumba yote ya Mungu.
He was faithful to the One who appointed Him, just as Moses was faithful in all God’s house.
3
Kwa maana huyo amehesabiwa kuwa amestahili utukufu zaidi kuliko Musa, kama vile yeye aitengenezaye nyumba alivyo na heshima zaidi ya hiyo nyumba.
For Jesus has been counted worthy of greater glory than Moses, just as the builder of a house has greater honor than the house itself.
4
Maana kila nyumba imetengenezwa na mtu; ila yeye aliyevitengeneza vitu vyote ni Mungu.
And every house is built by someone, but God is the builder of everything.
5
Na Musa kweli alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu kama mtumishi, awe ushuhuda wa mambo yatakayonenwa baadaye;
Now Moses was faithful as a servant in all God’s house, testifying to what would be spoken later.
6
bali Kristo, kama mwana, juu ya nyumba ya Mungu; ambaye nyumba yake ni sisi, kama tukishikamana sana na ujasiri wetu na fahari ya taraja letu mpaka mwisho.
But Christ is faithful as the Son over God’s house. And we are His house, if we hold firmly to our confidence and the hope of which we boast.
7
Kwa hiyo, kama anenavyo Roho Mtakatifu, Leo, kama mtaisikia sauti yake,
Therefore, as the Holy Spirit says: “Today, if you hear His voice,
8
Msifanye migumu mioyo yenu, Kama wakati wa kukasirisha, Siku ya kujaribiwa katika jangwa,
do not harden your hearts, as you did in the rebellion, in the day of testing in the wilderness,
9
Hapo baba zenu waliponijaribu, wakanipima, Wakaona matendo yangu miaka arobaini.
where your fathers tested and tried Me, and for forty years saw My works.
10
Kwa hiyo nalichukizwa na kizazi hiki, Nikasema, Sikuzote ni watu waliopotoka mioyo hawa; Hawakuzijua njia zangu;
Therefore I was angry with that generation, and I said, ‘Their hearts are always going astray, and they have not known My ways.’
11
Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu.
So I swore on oath in My anger, ‘They shall never enter My rest.’”
12
Angalieni, ndugu zangu, usiwe katika mmoja wenu moyo mbovu wa kutokuamini, kwa kujitenga na Mungu aliye hai.
See to it, brothers, that none of you has a wicked heart of unbelief that turns away from the living God.
13
Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.
But exhort one another daily, as long as it is called today, so that none of you may be hardened by sin’s deceitfulness.
14
Kwa maana tumekuwa washirika wa Kristo, kama tukishikamana na mwanzo wa uthabiti wetu kwa nguvu mpaka mwisho;
We have come to share in Christ if we hold firmly to the end the assurance we had at first.
15
hapo inenwapo, Leo, kama mtaisikia sauti yake, Msifanye migumu mioyo yenu, Kama wakati wa kukasirisha.
As it has been said: “Today, if you hear His voice, do not harden your hearts, as you did in the rebellion.”
16
Maana ni akina nani waliokasirisha, waliposikia? Si wale wote waliotoka Misri wakiongozwa na Musa?
For who were the ones who heard and rebelled? Were they not all those Moses led out of Egypt?
17
Tena ni akina nani aliochukizwa nao miaka arobaini? Si wale waliokosa, ambao mizoga yao ilianguka katika jangwa?
And with whom was God angry for forty years? Was it not with those who sinned, whose bodies fell in the wilderness?
18
Tena ni akina nani aliowaapia ya kwamba hawataingia katika raha yake, ila wale walioasi?
And to whom did He swear that they would never enter His rest? Was it not to those who disobeyed?
19
Basi twaona ya kuwa hawakuweza kuingia kwa sababu ya kutokuamini kwao.
So we see that it was because of their unbelief that they were unable to enter.

Chagua Sura

1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13