Waebrania 10 Swahili & English

Listen/Download Audio
Waebrania 10 (Swahili) Hebrews 10 (English)

Basi torati, kwa kuwa ni kivuli cha mema yatakayokuwa, wala si sura yenyewe ya mambo hayo, kwa dhabihu zile zile wanazozitoa kila mwaka daima, haiwezi wakati wo wote kuwakamilisha wakaribiao. Waebrania 10:1

For the law, having a shadow of the good to come, not the very image of the things, can never with the same sacrifices year by year, which they offer continually, make perfect those who draw near.

Kama ndivyo, je! Dhabihu hazingekoma kutolewa; kwa maana waabuduo, wakiisha kusafishwa mara moja, wasingejiona tena kuwa na dhambi? Waebrania 10:2

Or else wouldn't they have ceased to be offered, because the worshippers, having been once cleansed, would have had no more consciousness of sins?

Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka. Waebrania 10:3

But in those sacrifices there is yearly reminder of sins.

Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi. Waebrania 10:4

For it is impossible that the blood of bulls and goats should take away sins.

Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema, Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari; Waebrania 10:5

Therefore when he comes into the world, he says, "Sacrifice and offering you didn't desire, But a body did you prepare for me;

Sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi hukupendezwa nazo; Waebrania 10:6

In whole burnt offerings and sacrifices for sin you had no pleasure.

Ndipo niliposema, Tazama, nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa) Niyafanye mapenzi yako, Mungu. Waebrania 10:7

Then I said, 'Behold, I have come (In the scroll of the book it is written of me) To do your will, God.'"

Hapo juu asemapo, Dhabihu na matoleo na sadaka za kuteketezwa na hizo za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo (zitolewazo kama ilivyoamuru torati), Waebrania 10:8

Previously saying, "Sacrifices and offerings and whole burnt offerings and sacrifices for sin you didn't desire, neither had pleasure in them" (those which are offered according to the law),

ndipo aliposema, Tazama, nimekuja niyafanye mapenzi yako. Aondoa la kwanza, ili kusudi alisimamishe la pili. Waebrania 10:9

then he has said, "Behold, I have come to do your will." He takes away the first, that he may establish the second,

Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu. Waebrania 10:10

by which will we have been sanctified through the offering of the body of Jesus Christ once for all.

Na kila kuhani husimama kila siku akifanya ibada, na kutoa dhabihu zile zile mara nyingi; ambazo haziwezi kabisa kuondoa dhambi. Waebrania 10:11

Every priest indeed stands day by day ministering and often offering the same sacrifices, which can never take away sins,

Lakini huyu, alipokwisha kutoa kwa ajili ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu; Waebrania 10:12

but he, when he had offered one sacrifice for sins for ever, sat down on the right hand of God;

tangu hapo akingojea hata adui zake wawekwe kuwa chini ya miguu yake. Waebrania 10:13

from that time waiting until his enemies are made the footstool of his feet.

Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa. Waebrania 10:14

For by one offering he has perfected forever those who are being sanctified.

Na Roho Mtakatifu naye amshuhudia; kwa maana, baada ya kusema, Waebrania 10:15

The Holy Spirit also testifies to us, for after saying,

Hili ni agano nitakaloagana nao baada ya siku zile, anena Bwana, Nitatia sheria zangu mioyoni mwao, Na katika nia zao nitaziandika; ndipo anenapo, Waebrania 10:16

"This is the covenant that I will make with them: 'After those days,' says the Lord, 'I will put my laws on their heart, I will also write them on their mind;'" then he says,

Dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kabisa. Waebrania 10:17

"I will remember their sins and their iniquities no more."

Basi, ondoleo la hayo likiwapo, hapana toleo tena kwa ajili ya dhambi. Waebrania 10:18

Now where remission of these is, there is no more offering for sin.

Basi, ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia patakatifu kwa damu ya Yesu, Waebrania 10:19

Having therefore, brothers, boldness to enter into the holy place by the blood of Jesus,

njia ile aliyotuanzia iliyo mpya, iliyo hai, ipitayo katika pazia, yaani, mwili wake; Waebrania 10:20

by the way which he dedicated for us, a new and living way, through the veil, that is to say, his flesh;

na kuwa na kuhani mkuu juu ya nyumba ya Mungu; Waebrania 10:21

and having a great priest over the house of God,

na tukaribie wenye moyo wa kweli, kwa utimilifu wa imani, hali tumenyunyiziwa mioyo tuache dhamiri mbaya, tumeoshwa miili kwa maji safi. Waebrania 10:22

let's draw near with a true heart in fullness of faith, having our hearts sprinkled from an evil conscience, and having our body washed with pure water,

Na mlishike sana ungamo la tumaini letu, lisigeuke; maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu; Waebrania 10:23

let us hold fast the confession of our hope unyieldingly. For he who promised is faithful.

tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri; Waebrania 10:24

Let us consider how to provoke one another to love and good works,

wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia. Waebrania 10:25

not forsaking our own assembling together, as the custom of some is, but exhorting one another; and so much the more, as you see the Day approaching.

Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi; Waebrania 10:26

For if we sin willfully after we have received the knowledge of the truth, there remains no more a sacrifice for sins,

bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao. Waebrania 10:27

but a certain fearful expectation of judgment, and a fierceness of fire which will devour the adversaries.

Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu. Waebrania 10:28

A man who disregards Moses' law dies without compassion on the word of two or three witnesses.

Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema? Waebrania 10:29

How much worse punishment, do you think, will he be judged worthy of, who has trodden under foot the Son of God, and has counted the blood of the covenant with which he was sanctified an unholy thing, and has insulted the Spirit of grace?

Maana twamjua yeye aliyesema, Kupatiliza kisasi ni juu yangu, mimi nitalipa. Na tena, Bwana atawahukumu watu wake. Waebrania 10:30

For we know him who said, "Vengeance belongs to me," says the Lord, "I will repay." Again, "The Lord will judge his people."

Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai. Waebrania 10:31

It is a fearful thing to fall into the hands of the living God.

Lakini zikumbukeni siku za kwanza, ambazo, mlipokwisha kutiwa nuru, mlistahimili mashindano makubwa ya maumivu; Waebrania 10:32

But remember the former days, in which, after you were enlightened, you endured a great struggle with sufferings;

pindi mlipotwezwa kwa mashutumu na dhiki, na pindi mliposhirikiana na wale waliotendewa hayo. Waebrania 10:33

partly, being exposed to both reproaches and oppressions; and partly, becoming partakers with those who were treated so.

Maana mliwaonea huruma wale waliokuwa katika vifungo, tena mkakubali kwa furaha kunyang'anywa mali zenu, mkijua kwamba nafsini mwenu mna mali iliyo njema zaidi, idumuyo. Waebrania 10:34

For you both had compassion on me in my chains, and joyfully accepted the plundering of your possessions, knowing that you have for yourselves a better possession and an enduring one in the heavens.

Basi msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kuu. Waebrania 10:35

Therefore don't throw away your boldness, which has a great reward.

Maana mnahitaji saburi, ili kwamba mkiisha kuyafanya mapenzi ya Mungu mpate ile ahadi. Waebrania 10:36

For you need endurance so that, having done the will of God, you may receive the promise.

Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia. Waebrania 10:37

"In a very little while, He who comes will come, and will not wait.

Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye. Waebrania 10:38

But the righteous will live by faith. If he shrinks back, my soul has no pleasure in him."

Lakini sisi hatumo miongoni mwao wasitao na kupotea, bali tumo miongoni mwa hao walio na imani ya kutuokoa roho zetu. Waebrania 10:39

But we are not of those who shrink back to destruction, but of those who have faith to the saving of the soul.