1
Wakasimama mkutano wote, wakampeleka kwa Pilato.
Then the whole council rose and led Jesus away to Pilate.
2
Wakaanza kumshitaki, wakisema, Tumemwona huyu akipotosha taifa letu, na kuwazuia watu wasimpe Kaisari kodi, akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo, mfalme.
And they began to accuse Him, saying, “We found this man subverting our nation, forbidding payment of taxes to Caesar, and proclaiming Himself to be Christ, a King.”
3
Pilato akamwuliza, akisema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Akajibu akamwambia, Wewe wasema.
So Pilate asked Him, “Are You the King of the Jews?” “You have said so,” Jesus replied.
4
Pilato akawaambia wakuu wa makuhani na makutano, Sioni neno lililo ovu katika mtu huyu.
Then Pilate said to the chief priests and the crowds, “I find no basis for a charge against this man.”
5
Nao walikaza sana, wakisema, Huwataharakisha watu, akifundisha katika Uyahudi yote, tokea Galilaya mpaka huku.
But they kept insisting, “He stirs up the people all over Judea with His teaching. He began in Galilee and has come all the way here.”
6
Pilato aliposikia hayo aliuliza kama huyu ni mtu wa Galilaya.
When Pilate heard this, he asked if the man was a Galilean.
7
Na alipopata habari ya kuwa yu chini ya mamlaka ya Herode, alimpeleka kwa Herode, kwa kuwa yeye naye alikuwapo Yerusalemu siku zile.
And learning that Jesus was under Herod’s jurisdiction, he sent Him to Herod, who himself was in Jerusalem at that time.
8
Na Herode alipomwona Yesu alifurahi sana, kwa sababu alikuwa akitaka sana kumwona tangu siku nyingi, maana amesikia habari zake, akataraji kuona ishara iliyofanywa na yeye.
When Herod saw Jesus, he was greatly pleased. He had wanted to see Him for a long time, because he had heard about Him and was hoping to see Him perform a miracle.
9
Akamwuliza maneno mengi, yeye asimjibu lo lote.
Herod questioned Jesus at great length, but He gave no answer.
10
Wakuu wa makuhani na waandishi wakasimama wakamshitaki kwa nguvu sana.
Meanwhile, the chief priests and scribes stood there, vehemently accusing Him.
11
Basi Herode akamfanya duni, pamoja na askari zake, akamdhihaki, na kumvika mavazi mazuri; kisha akamrudisha kwa Pilato.
And even Herod and his soldiers ridiculed and mocked Him. Dressing Him in a fine robe, they sent Him back to Pilate.
12
Basi siku ile ile Herode na Pilato walipatana kwa urafiki kwa maana hapo kwanza walikuwa na uadui wao kwa wao.
That day Herod and Pilate became friends; before this time they had been enemies.
13
Na Pilato akawakutanisha wakuu wa makuhani, na wakubwa, na watu,
Then Pilate called together the chief priests, the rulers, and the people,
14
akawaambia, Mtu huyu mmemleta kwangu kana kwamba anapotosha watu; nami, tazama, nimeamua mambo yake mbele yenu, ila sikuona kwake kosa lo lote katika mambo hayo mliyomshitaki;
and said to them, “You brought me this man as one who was inciting the people to rebellion. I have examined Him here in your presence and found Him not guilty of your charges against Him.
15
wala hata Herode, kwa maana amemrudisha kwetu; basi tazama, hakuna neno lo lote alilolitenda lipasalo kufa.
Neither has Herod, for he sent Him back to us. As you can see, He has done nothing deserving of death.
16
Kwa hiyo nitamrudi, kisha nitamfungua. [
Therefore I will punish Him and release Him.”
17
Maana ilimlazimu kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa sikukuu.]
18
Wakapiga kelele wote pamoja, wakisema, Mwondoe huyu, utufungulie Baraba.
But they all cried out in unison: “Away with this man! Release Barabbas to us!”
19
Naye ni mtu aliyetupwa gerezani kwa ajili ya fitina iliyotokea mjini, na kwa uuaji
(Barabbas had been imprisoned for an insurrection in the city, and for murder.)
20
Basi Pilato alisema nao mara ya pili, kwa vile alivyotaka kumfungua Yesu.
Wanting to release Jesus, Pilate addressed them again,
21
Lakini wakapiga kelele, wakisema, Msulibishe. Msulibishe.
but they kept shouting, “Crucify Him! Crucify Him!”
22
Akawaambia mara ya tatu, Kwa sababu gani? Huyu ametenda uovu gani? Sikuona kwake hata neno lipasalo kufa. Basi nikiisha kumrudi nitamfungua.
A third time he said to them, “What evil has this man done? I have found in Him no offense worthy of death. So after I punish Him, I will release Him.”
23
Lakini wakatoa sauti zao kwa nguvu sana, wakitaka asulibiwe. Sauti zao zikashinda.
But they were insistent, demanding with loud voices for Jesus to be crucified. And their clamor prevailed.
24
Pilato akahukumu kwamba haja yao ifanyike.
So Pilate sentenced that their demand be met.
25
Akamfungua yule aliyetupwa gerezani kwa ajili ya fitina na uuaji, yule waliyemtaka, akamtoa Yesu wamfanyie watakavyo.
As they had requested, he released the one imprisoned for insurrection and murder, and he handed Jesus over to their will.
26
Na walipokuwa wakimwondoa walimkamata mtu mmoja, Simoni Mkirene, aliyekuwa ametoka shamba, wakamtwika msalaba, auchukue nyuma yake Yesu.
As the soldiers led Him away, they seized Simon of Cyrene on his way in from the country, and they put the cross on him to carry behind Jesus.
27
Mkutano mkubwa wa watu wakamfuata, na wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea.
A great number of people followed Him, including women who kept mourning and wailing for Him.
28
Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu.
But Jesus turned to them and said, “Daughters of Jerusalem, do not weep for Me, but weep for yourselves and for your children.
29
Kwa maana tazama, siku zitakuja watakaposema, Heri walio tasa, na matumbo yasiyozaa, na maziwa yasiyonyonyesha.
Look, the days are coming when people will say, ‘Blessed are the barren women, the wombs that never bore, and breasts that never nursed!’
30
Ndipo watakapoanza kuiambia milima, Tuangukieni, na vilima, Tufunikeni.
At that time ‘they will say to the mountains, “Fall on us!” and to the hills, “Cover us!”’
31
Kwa kuwa kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
For if men do these things while the tree is green, what will happen when it is dry?”
32
Wakapelekwa na wawili wengine, wahalifu, wauawe pamoja naye.
Two others, who were criminals, were also led away to be executed with Jesus.
33
Na walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, ndipo walipomsulibisha yeye, na wale wahalifu, mmoja upande wa kuume, na mmoja upande wa kushoto.
When they came to the place called The Skull, they crucified Him there, along with the criminals, one on His right and the other on His left.
34
Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura.
Then Jesus said, “Father, forgive them, for they do not know what they are doing.” And they divided up His garments by casting lots.
35
Watu wakasimama wakitazama. Wale wakuu nao walikuwa wakimfanyia mzaha, wakisema, Aliokoa wengine; na ajiokoe mwenyewe, kama ndiye Kristo wa Mungu, mteule wake.
The people stood watching, and the rulers sneered at Him, saying, “He saved others; let Him save Himself if He is the Christ of God, the Chosen One.”
36
Wale askari nao wakamfanyia dhihaka, wakimwendea na kumletea siki,
The soldiers also mocked Him and came up to offer Him sour wine.
37
huku wakisema, Kama wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi, ujiokoe mwenyewe.
“If You are the King of the Jews,” they said, “save Yourself!”
38
Na juu yake palikuwa na anwani; HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.
Above Him was posted an inscription: THIS IS THE KING OF THE JEWS.
39
Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi.
One of the criminals who hung there heaped abuse on Him. “Are You not the Christ?” he said. “Save Yourself and us!”
40
Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?
But the other one rebuked him, saying, “Do you not even fear God, since you are under the same judgment?
41
Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.
We are punished justly, for we are receiving what our actions deserve. But this man has done nothing wrong.”
42
Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.
Then he said, “Jesus, remember me when You come into Your kingdom!”
43
Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.
And Jesus said to him, “Truly I tell you, today you will be with Me in Paradise.”
44
Hapo ilikuwa yapata saa sita, kukawa giza juu ya nchi yote hata saa kenda,
It was now about the sixth hour, and darkness came over all the land until the ninth hour.
45
jua limepungua nuru yake; pazia la hekalu likapasuka katikati.
The sun was darkened, and the veil of the temple was torn down the middle.
46
Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu.
Then Jesus called out in a loud voice, “Father, into Your hands I commit My Spirit.” And when He had said this, He breathed His last.
47
Alipokwisha kusema hayo alikata roho. Yule akida alipoona yaliyotukia, alimtukuza Mungu, akisema, Hakika yake, mtu huyu alikuwa mwenye haki.
When the centurion saw what had happened, he gave glory to God, saying, “Surely this was a righteous man.”
48
Na makutano yote ya watu waliokuwa wamekutanika kutazama mambo hayo, walipoona yaliyotendeka, wakaenda zao kwao, wakijipiga-piga vifua.
And when all the people who had gathered for this spectacle saw what had happened, they returned home beating their breasts.
49
Na wote waliojuana naye, na wale wanawake walioandamana naye toka Galilaya, wakasimama kwa mbali, wakitazama mambo hayo.
But all those who knew Jesus, including the women who had followed Him from Galilee, stood at a distance watching these things.
50
Na tazama, akatoka mtu mmoja, jina lake Yusufu, ambaye ni mtu wa baraza, mtu mwema, mwenye haki;
Now there was a Council member named Joseph, a good and righteous man,
51
(wala hakulikubali shauri na tendo lao), naye ni mtu wa Arimathaya, mji mmoja wa Wayahudi, tena anautazamia ufalme wa Mungu;
who had not consented to their decision or action. He was from the Judean town of Arimathea and was waiting for the kingdom of God.
52
mtu huyo alikwenda kwa Pilato, akataka kupewa mwili wa Yesu.
He went to Pilate to ask for the body of Jesus.
53
Akaushusha, akauzinga sanda ya kitani, akauweka katika kaburi lililochongwa mwambani, ambalo hajalazwa mtu bado ndani yake.
Then he took it down, wrapped it in a linen cloth, and placed it in a tomb cut into the rock, where no one had yet been laid.
54
Na siku ile ilikuwa siku ya Maandalio, na sabato ikaanza kuingia.
It was Preparation Day, and the Sabbath was beginning.
55
Na wale wanawake waliokuja naye toka Galilaya walifuata, wakaliona kaburi, na jinsi mwili wake ulivyowekwa.
The women who had come with Jesus from Galilee followed, and they saw the tomb and how His body was placed.
56
Wakarudi, wakafanya tayari manukato na marhamu. Na siku ya sabato walistarehe kama ilivyoamriwa.
Then they returned to prepare spices and perfumes. And they rested on the Sabbath, according to the commandment.