1
Naye alipoingia Yeriko alipita katikati yake.
Then Jesus entered Jericho and was passing through.
2
Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri.
And there was a man named Zacchaeus, a chief tax collector, who was very wealthy.
3
Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo.
He was trying to see who Jesus was, but could not see over the crowd because he was small in stature.
4
Akatangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu apate kumwona, kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile.
So he ran on ahead and climbed a sycamore tree to see Him, since Jesus was about to pass that way.
5
Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, shuka upesi, kwa kuwa leo imenipasa kushinda nyumbani mwako.
When Jesus came to that place, He looked up and said, “Zacchaeus, hurry down, for I must stay at your house today.”
6
Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha.
So Zacchaeus hurried down and welcomed Him joyfully.
7
Hata watu walipoona, walinung'unika wote, wakisema, Ameingia kukaa kwa mtu mwenye dhambi.
And all who saw this began to grumble, saying, “He has gone to be the guest of a sinful man!”
8
Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang'anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.
But Zacchaeus stood up and said to the Lord, “Look, Lord, half of my possessions I give to the poor, and if I have cheated anyone, I will repay it fourfold.”
9
Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu.
Jesus said to him, “Today salvation has come to this house, because this man too is a son of Abraham.
10
Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.
For the Son of Man came to seek and to save the lost.”
11
Waliposikia hayo, aliongeza kusema mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu utaonekana mara.
While the people were listening to this, Jesus proceeded to tell them a parable, because He was near Jerusalem and they thought the kingdom of God would appear imminently.
12
Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi.
So He said, “A man of noble birth went to a distant country to lay claim to his kingship and then return.
13
Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, Fanyeni biashara hata nitakapokuja.
Beforehand, he called ten of his servants and gave them ten minas. ‘Conduct business with this until I return,’ he said.
14
Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale.
But his subjects hated him and sent a delegation after him to say, ‘We do not want this man to rule over us.’
15
Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake.
When he returned from procuring his kingship, he summoned the servants to whom he had given the money, to find out what each one had earned.
16
Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.
The first servant came forward and said, ‘Master, your mina has produced ten more minas.’
17
Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.
His master replied, ‘Well done, good servant! Because you have been faithful in a very small matter, you shall have authority over ten cities.’
18
Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida.
The second servant came and said, ‘Master, your mina has made five minas.’
19
Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano.
And to this one he said, ‘You shall have authority over five cities.’
20
Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso.
Then another servant came and said, ‘Master, here is your mina, which I have laid away in a piece of cloth.
21
Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda.
For I was afraid of you, because you are a harsh man. You withdraw what you did not deposit and reap what you did not sow.’
22
Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda;
His master replied, ‘You wicked servant, I will judge you by your own words. So you knew that I am a harsh man, withdrawing what I did not deposit and reaping what I did not sow?
23
basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake?
Why then did you not deposit my money in the bank, and upon my return I could have collected it with interest?’
24
Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang'anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi.
Then he told those standing by, ‘Take the mina from him and give it to the one who has ten minas.’
25
Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi.
‘Master,’ they said, ‘he already has ten!’
26
Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang'anywa hata alicho nacho.
He replied, ‘I tell you that everyone who has will be given more; but the one who does not have, even what he has will be taken away from him.
27
Tena, wale adui zangu, wasiotaka niwatawale, waleteni hapa mwachinje mbele yangu.
And these enemies of mine who were unwilling for me to rule over them, bring them here and slay them in front of me.’”
28
Na alipokwisha kusema hayo, alitangulia mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
After Jesus had said this, He went on ahead, going up to Jerusalem.
29
Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, kwenye mlima uitwao wa Mizeituni, alituma wawili katika wale wanafunzi,
As He approached Bethphage and Bethany at the Mount of Olives, He sent out two of His disciples,
30
akisema, Nendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mtakapoingia ndani mtaona mwana-punda, amefungwa, ambaye hajapandwa na mtu ye yote bado, mfungueni mkamlete hapa.
saying, “Go into the village ahead of you, and as you enter it, you will find a colt tied there, on which no one has ever sat. Untie it and bring it here.
31
Na kama mtu akiwauliza, Mbona mnamfungua? Semeni hivi, Bwana anamhitaji.
If anyone asks, ‘Why are you untying it?’ tell him, ‘The Lord needs it.’”
32
Na wale waliotumwa wakaenda wakaona kama alivyowaambia.
So those who were sent went out and found it just as Jesus had told them.
33
Na walipokuwa wakimfungua mwana-punda, wenyewe waliwaambia, Mbona mnamfungua mwana-punda?
As they were untying the colt, its owners asked, “Why are you untying the colt?”
34
Wakasema, Bwana ana haja naye.
“The Lord needs it,” they answered.
35
Wakampeleka kwa Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana-punda, wakampandisha Yesu.
Then they led the colt to Jesus, threw their cloaks over it, and put Jesus on it.
36
Na alipokuwa akienda walitandaza nguo zao njiani.
As He rode along, the people spread their cloaks on the road.
37
Hata alipokuwa amekaribia matelemko ya mlima wa Mizeituni, kundi zima la wanafunzi wake walianza kufurahi na kumsifu Mungu kwa sauti kuu, kwa ajili ya matendo yote ya uwezo waliyoyaona,
And as He approached the descent from the Mount of Olives, the whole multitude of disciples began to praise God joyfully in a loud voice for all the miracles they had seen:
38
wakasema, Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana; amani mbinguni, na utukufu huko juu.
“Blessed is the King who comes in the name of the Lord!” “Peace in heaven and glory in the highest!”
39
Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, uwakanye wanafunzi wako.
But some of the Pharisees in the crowd said to Him, “Teacher, rebuke Your disciples!”
40
Akajibu, akasema, Nawaambia ninyi, wakinyamaza hawa, mawe yatapiga kelele.
“I tell you,” He answered, “if they remain silent, the very stones will cry out.”
41
Alipofika karibu aliuona mji, akaulilia,
As Jesus approached Jerusalem and saw the city, He wept over it
42
akisema, Laiti ungalijua, hata wewe katika siku hii, yapasayo amani! Lakini sasa yamefichwa machoni pako.
and said, “If only you had known on this day what would bring you peace! But now it is hidden from your eyes.
43
Kwa kuwa siku zitakuja, adui zako watakapokujengea boma, likuzunguke; watakuzingira na kukuhusuru pande zote;
For the days will come upon you when your enemies will barricade you and surround you and hem you in on every side.
44
watakuangusha chini wewe na watoto wako ndani yako, wasikuachie jiwe juu ya jiwe, kwa sababu hukutambua majira ya kujiliwa kwako.
They will level you to the ground—you and the children within your walls. They will not leave one stone on another, because you did not recognize the time of your visitation from God.”
45
Akaingia hekaluni, akaanza kuwatoa wale waliokuwa wakifanya biashara,
Then Jesus entered the temple courts and began to drive out those who were selling there.
46
akiwaambia, Imeandikwa, Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.
He declared to them, “It is written: ‘My house will be a house of prayer.’ But you have made it ‘a den of robbers.’”
47
Naye akawa akifundisha kila siku hekaluni. Lakini wakuu wa makuhani, na waandishi, na wakuu wa watu walikuwa wakitafuta njia ya kumwangamiza;
Jesus was teaching at the temple every day, but the chief priests, scribes, and leaders of the people were intent on killing Him.
48
wasione la kutenda, kwa kuwa watu wote walikuwa wakiandamana naye, wakimsikiliza.
Yet they could not find a way to do so, because all the people hung on His words.