Yohana 7 Swahili & English
Listen/Download AudioYohana 7 (Swahili) | John 7 (English) |
---|---|
Na baada ya hayo Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya; maana hakutaka kutembea katika Uyahudi, kwa sababu Wayahudi walikuwa wakitafuta kumwua. Yohana 7:1 |
After these things, Jesus was walking in Galilee, for he wouldn't walk in Judea, because the Jews sought to kill him. |
Na sikukuu ya Wayahudi, Sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu. Yohana 7:2 |
Now the feast of the Jews, the Feast of Booths, was at hand. |
Basi ndugu zake wakamwambia, Ondoka hapa, uende Uyahudi, wanafunzi wako nao wapate kuzitazama kazi zako unazozifanya. Yohana 7:3 |
His brothers therefore said to him, "Depart from here, and go into Judea, that your disciples also may see your works which you do. |
Kwa maana hakuna mtu afanyaye neno kwa siri, naye mwenyewe ataka kujulikana. Ukifanya mambo haya, basi jidhihirishe kwa ulimwengu. Yohana 7:4 |
For no one does anything in secret, and himself seeks to be known openly. If you do these things, reveal yourself to the world." |
Maana hata nduguze hawakumwamini. Yohana 7:5 |
For even his brothers didn't believe in him. |
Basi Yesu akawaambia, Haujafika bado wakati wangu; ila wakati wenu sikuzote upo. Yohana 7:6 |
Jesus therefore said to them, "My time has not yet come, but your time is always ready. |
Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi; bali hunichukia mimi, kwa sababu mimi naushuhudia ya kuwa kazi zake ni mbovu. Yohana 7:7 |
The world can't hate you, but it hates me, because I testify about it, that its works are evil. |
Kweeni ninyi kwenda kula sikukuu; mimi sikwei bado kwenda kula sikukuu hii, kwa kuwa haujatimia wakati wangu. Yohana 7:8 |
You go up to the feast. I am not yet going up to this feast, because my time is not yet fulfilled." |
Naye alipokwisha kuwaambia hayo, alikaa vivi hivi huko Galilaya. Yohana 7:9 |
Having said these things to them, he stayed in Galilee. |
Hata ndugu zake walipokwisha kukwea kuiendea sikukuu, ndipo yeye naye alipokwea, si kwa wazi bali kana kwamba kwa siri. Yohana 7:10 |
But when his brothers had gone up to the feast, then he also went up, not publicly, but as it were in secret. |
Basi Wayahudi wakamtafuta kwenye sikukuu, wakasema, Yuko wapi yule? Yohana 7:11 |
The Jews therefore sought him at the feast, and said, "Where is he?" |
Kukawa na manung'uniko mengi katika makutano juu yake. Wengine wakasema, Ni mtu mwema. Na wengine wakasema, Sivyo; bali anawadanganya makutano. Yohana 7:12 |
There was much murmuring among the multitudes concerning him. Some said, "He is a good man." Others said, "Not so, but he leads the multitude astray." |
Walakini hakuna mtu aliyemtaja waziwazi, kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi. Yohana 7:13 |
Yet no one spoke openly of him for fear of the Jews. |
Hata ikawa katikati ya sikukuu Yesu alikwea kuingia hekaluni, akafundisha. Yohana 7:14 |
But when it was now the midst of the feast, Jesus went up into the temple and taught. |
Wayahudi wakastaajabu wakisema, Amepataje huyu kujua elimu, ambaye hakusoma? Yohana 7:15 |
The Jews therefore marveled, saying, "How does this man know letters, having never been educated?" |
Basi Yesu akawajibu, akasema, Mafunzo yangu si yangu mimi, ila ni yake yeye aliyenipeleka. Yohana 7:16 |
Jesus therefore answered them, "My teaching is not mine, but his who sent me. |
Mtu akipenda kuyatenda mapenzi yake, atajua habari ya yale mafunzo, kwamba yatoka kwa Mungu, au kwamba mimi nanena kwa nafsi yangu tu. Yohana 7:17 |
If anyone desires to do his will, he will know about the teaching, whether it is from God, or if I am speaking from myself. |
Yeye anenaye kwa nafsi yake tu hutafuta utukufu wake mwenyewe; bali yeye anayetafuta utukufu wake aliyempeleka, huyo ni wa kweli, wala ndani yake hamna udhalimu. Yohana 7:18 |
He who speaks from himself seeks his own glory, but he who seeks the glory of him who sent him, the same is true, and no unrighteousness is in him. |
Je! Musa hakuwapa torati? Wala hakuna mmoja wenu aitendaye torati. Mbona mnatafuta kuniua? Yohana 7:19 |
Didn't Moses give you the law, and yet none of you keeps the law? Why do you seek to kill me?" |
Mkutano wakajibu, Ama! Una pepo! Ni nani anayetafuta kukuua? Yohana 7:20 |
The multitude answered, "You have a demon! Who seeks to kill you?" |
Yesu akajibu, akawaambia, Mimi nalitenda kazi moja, nanyi nyote mnaistaajabia. Yohana 7:21 |
Jesus answered them, "I did one work, and you all marvel because of it. |
Musa aliwapa tohara; lakini si kwamba yatoka kwa Musa, bali kwa mababa; nanyi siku ya sabato humtahiri mtu. Yohana 7:22 |
Moses has given you circumcision (not that it is of Moses, but of the fathers), and on the Sabbath you circumcise a boy. |
Basi ikiwa mtu hupashwa tohara siku ya sabato, ili torati ya Musa isije ikavunjika, mbona mnanikasirikia mimi kwa sababu nalimfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya sabato? Yohana 7:23 |
If a boy receives circumcision on the Sabbath, that the law of Moses may not be broken, are you angry with me, because I made a man every bit whole on the Sabbath? |
Basi msihukumu hukumu ya macho tu, bali ifanyeni hukumu iliyo ya haki. Yohana 7:24 |
Don't judge according to appearance, but judge righteous judgment." |
Basi baadhi ya watu wa Yerusalemu wakasema, Je! Huyu siye wanayemtafuta ili wamwue? Yohana 7:25 |
Therefore some of them of Jerusalem said, "Isn't this he whom they seek to kill? |
Na kumbe! Anena waziwazi, wala hawamwambii neno! Yamkini hao wakuu wanajua hakika ya kuwa huyu ndiye Kristo? Yohana 7:26 |
Behold, he speaks openly, and they say nothing to him. Can it be that the rulers indeed know that this is truly the Christ? |
Lakini huyu twamjua atokako; bali Kristo atakapokuja hakuna ajuaye atokako. Yohana 7:27 |
However we know where this man comes from, but when the Christ comes, no one will know where he comes from." |
Basi Yesu akapaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, Mimi mnanijua, na huko nitokako mnakujua; wala sikuja kwa nafsi yangu; ila yeye aliyenipeleka ni wa kweli, msiyemjua ninyi. Yohana 7:28 |
Jesus therefore cried out in the temple, teaching and saying, "You both know me, and know where I am from. I have not come of myself, but he who sent me is true, whom you don't know. |
Mimi namjua, kwa kuwa nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma. Yohana 7:29 |
I know him, because I am from him, and he sent me." |
Basi wakatafuta kumkamata; lakini hakuna mtu aliyeunyosha mkono wake ili kumshika, kwa sababu saa yake ilikuwa haijaja bado. Yohana 7:30 |
They sought therefore to take him; but no one laid a hand on him, because his hour had not yet come. |
Na watu wengi katika mkutano wakamwamini; wakasema, Atakapokuja Kristo, je! Atafanya ishara nyingi zaidi kuliko hizi alizozifanya huyu? Yohana 7:31 |
But of the multitude, many believed in him. They said, "When the Christ comes, he won't do more signs than those which this man has done, will he?" |
Mafarisayo wakawasikia mkutano wakinung'unika hivi juu yake; basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakatuma watumishi ili wamkamate. Yohana 7:32 |
The Pharisees heard the multitude murmuring these things concerning him, and the chief priests and the Pharisees sent officers to arrest him. |
Basi Yesu akasema, Bado kitambo kidogo nipo pamoja nanyi; kisha naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka. Yohana 7:33 |
Then Jesus said, "I will be with you a little while longer, then I go to him who sent me. |
Mtanitafuta wala hamtaniona; nami nilipo ninyi hamwezi kuja. Yohana 7:34 |
You will seek me, and won't find me; and where I am, you can't come." |
Basi Wayahudi wakasemezana, Huyu atakwenda wapi hata sisi tusimwone? Ati! Atakwenda kwa Utawanyiko wa Wayunani, na kuwafundisha Wayunani? Yohana 7:35 |
The Jews therefore said among themselves, "Where will this man go that we won't find him? Will he go to the Dispersion among the Greeks, and teach the Greeks? |
Ni neno gani hilo alilolisema, Mtanitafuta wala hamtaniona; nami nilipo ninyi hamwezi kuja? Yohana 7:36 |
What is this word that he said, 'You will seek me, and won't find me; and where I am, you can't come?'" |
Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe. Yohana 7:37 |
Now on the last and greatest day of the feast, Jesus stood and cried out, "If anyone is thirsty, let him come to me and drink! |
Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake. Yohana 7:38 |
He who believes in me, as the Scripture has said, from within him will flow rivers of living water." |
Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa. Yohana 7:39 |
But he said this about the Spirit, which those believing in him were to receive. For the Holy Spirit was not yet given, because Jesus wasn't yet glorified. |
Basi wengine katika mkutano walipoyasikia maneno hayo, walisema, Hakika huyu ndiye nabii yule. Yohana 7:40 |
Many of the multitude therefore, when they heard these words, said, "This is truly the prophet." |
Wengine walisema, Huyu ndiye Kristo. Wengine wakasema, Je! Kristo atoka Galilaya? Yohana 7:41 |
Others said, "This is the Christ." But some said, "What, does the Christ come out of Galilee? |
Andiko halikusema ya kwamba Kristo atoka katika uzao wa Daudi, na kutoka Bethlehemu, mji ule alioukaa Daudi? Yohana 7:42 |
Hasn't the Scripture said that the Christ comes of the seed of David, and from Bethlehem, the village where David was?" |
Basi kukaingia matengano katika mkutano kwa ajili yake. Yohana 7:43 |
So there arose a division in the multitude because of him. |
Baadhi yao wakataka kumkamata, lakini hakuna mtu aliyenyosha mikono yake ili kumshika. Yohana 7:44 |
Some of them would have arrested him, but no one laid hands on him. |
Basi wale watumishi wakawaendea wakuu wa makuhani na Mafarisayo. Nao wakawaambia, Mbona hamkumleta? Yohana 7:45 |
The officers therefore came to the chief priests and Pharisees, and they said to them, "Why didn't you bring him?" |
Wale watumishi wakajibu. Hajanena kamwe mtu ye yote kama huyu anavyonena. Yohana 7:46 |
The officers answered, "No man ever spoke like this man!" |
Basi Mafarisayo wakawajibu, Je! Ninyi nanyi mmedanganyika? Yohana 7:47 |
The Pharisees therefore answered them, "You aren't also led astray, are you? |
Ni nani katika wakuu amwaminiye, au katika Mafarisayo? Yohana 7:48 |
Have any of the rulers believed in him, or of the Pharisees? |
Lakini makutano hawa wasioifahamu torati wamelaaniwa. Yohana 7:49 |
But this multitude that doesn't know the law is accursed." |
Akawaambia Nikodemo, (naye ni yule aliyemwendea zamani, maana ni mmoja wao), Yohana 7:50 |
Nicodemus (he who came to him by night, being one of them) said to them, |
Je! Torati yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza, na kujua atendavyo? Yohana 7:51 |
"Does our law judge a man, unless it first hears from him personally and knows what he does?" |
Wakajibu, wakamwambia, Je! Wewe nawe umetoka Galilaya! Yohana 7:52 |
They answered him, "Are you also from Galilee? Search, and see that no prophet has arisen out of Galilee." |
Tafuta, ukaone ya kuwa kutoka Galilaya hakutokea nabii. Yohana 7:53 |
Everyone went to his own house, |