Zabron Singers - Nitasubiri Lyrics

Lyrics

Ya nini Mungu kujificha wakati wa shida? Wakati mwingine kama kweli huoni Wajua yote yalonikuta hasimliki Nimelia na kujinyamazisha pekee yangu

Moyoni nikataabika, furaha ikaenda Sikumwona wa kumwelezea shida Rafiki pekee namwamini, ni Yesu mfariji Ndio maana sijamwambia mtu shida zangu

Nitasubiri na kusubiri sitachoka Nimeshamezana na wewe kwa maombi Usipojibu, au ujibu nitaelewa Nashukuru, hata kwa majaribu Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Nitasubiri na kusubiri sitachoka Nimeshamezana na wewe kwa maombi Usipojibu, au ujibu nitaelewa Nashukuru, hata kwa majaribu Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Kwa nini sasa umesimama mbali nami Bwana? Muda mwingi mi najihisi mi ni mpweke Jidhihirishe mi nikuone, nakuhitaji Bwana Nibariki sasa ukijibu maombi, yangu

Najua mengi nimekuudhi, nimetenda dhambi Ndio maana ukasimama mbali nami Nisamehe yote yote bure, kwa damu ya Yesu Nifanye mi niwe mtoto wako siku, zote

Nitasubiri na kusubiri sitachoka Nimeshamezana na wewe kwa maombi Usipojibu, au ujibu nitaelewa Nashukuru, hata kwa majaribu Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Nitasubiri na kusubiri sitachoka Nimeshamezana na wewe kwa maombi Usipojibu, au ujibu nitaelewa Nashukuru, hata kwa majaribu Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Video

Nitasubiri by Zabron Singers -Official Video (SMS SKIZA 7383818 TO 811)

Thumbnail for Nitasubiri video
Loading...
In Queue
View Lyrics