Walter Chilambo - Unaniona Lyrics

Contents: Song Information
  • Song Title: Unaniona
  • Album: Thank You Lord
  • Artist: Walter Chilambo
  • Released On: 30 Jan 2021
  • Download/Stream: iTunes Music Amazon Music
Walter Chilambo Unaniona

Unaniona Lyrics

Kama Mungu angechagua watu wake 
Mimi singekuwepo duniani 
Kama Mungu angechagua watakatifu 
Mimi singekuwepo duniani 

Mimi binadamu wala si malaika 
Mengi ninakosea na kukuchukiza 
Ninafanya mambo yasiyostahili 
Nimevuruga-vuruga mipango yako 
Wanihurumia, 

Mbele ya macho ya wanadamu 
Nilikuwa nikijificha 
Kumbe wewe waniona 
Kwa Kujifanya (mtakatifu) tena (mkarimu) 
Nilikuwa (mnyenyekevu tena mpole sana) 
Kwa Kujifanya (mtakatifu) tena (mkarimu) 
Kwenye ibada (mnyenyekevu tena mpole sana)

Kumbe Mungu aniona, macho yako yanitazama 
Sikio lako lanisikia, siwezi jificha aah 
Kumbe Mungu aniona, macho yako yanitazama 
Sikio lako lanisikia, siwezi jificha aah 

Sasa nimetambua mbivu na mbichi ni zipi 
Sasa ninaelewa njia salama ni wapi 
Na nimejua bila ya wewe sifiki 
Hata nikila pasipo neno lako sishibi 
Neema yako (ila kwa neema yako) 
Upendo wako (ila kwa upendo wako) 
Na rehema zako zimenihimarisha tena 

Mbele ya macho ya wanadamu 
Nilikuwa nikijificha 
Kumbe wewe waniona 
Kwa Kujifanya (mtakatifu) tena (mkarimu) 
Nilikuwa (mnyenyekevu tena mpole sana) 
Kwa Kujifanya (mtakatifu) tena (mkarimu) 
Kwenye ibada (mnyenyekevu tena mpole sana) 

Kumbe Mungu aniona, macho yako yanitazama 
Sikio lako lanisikia, siwezi jificha aah 
Kumbe Mungu aniona, macho yako yanitazama 
Sikio lako lanisikia, siwezi jificha aah 


Unaniona Video

Walter Chilambo Songs

Related Songs