Lyrics
Verse 1
Ndoa ni mpango takatifu tangu mwanzo,
ujumbe njema utokao kwa Baba,
yahitajika hekima kuitunza
hadi kifo kiwatenganishe.
Chorus
Mke si kidude cha kujaribu miguu yako,
Mume si kipasa sauti cha kupigia kelele
Mpendaneni, msichokozane,
amani ya Bwana iwe ndani yenu.
Verse 2
Kazi kwenu sasa maishani mwenu,
mdumu milele kwenye upendo wa Yesu,
ni Mungu pekee aweza kuwalinda na kutatua
mashaka yenu ya Maisha.
Bridge
Muwe mfano bora kwa watoto wenu,
waonyeshe njia ile ya uzima ya wokovu,
Nanyi watoto wote watiini wazazi wenu,
mibaraka yake Mungu 'tawakirimia.
Credits & Song Information
Video
Meaning & Inspiration
Wimbo huu unaeleza ndoa kama agano takatifu lililowekwa na Mungu tangu mwanzo. Unawahimiza wanandoa kuheshimiana, kupendana bila kuchokozana, na kudumu katika upendo wa Yesu. Pia unaweka familia kama mfano bora kwa watoto, huku watoto wakihimizwa kuwatii wazazi wao na kufuata njia ya wokovu.