PaPi Clever & Dorcas - Mwokozi Wangu Ni mMwamba Bora Lyrics

Lyrics

Mwokozi wangu ni mwamba bora, ahadi kama milima Zaniletea amani tele, na mibaraka daima Katika mwamba ni raha kuu, baraka tele kutoka juu Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele Katika mwamba ni raha kuu, baraka tele kutoka juu Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele

Makimbilio ni mwamba huo katika teso lo lote Nisikimbie adui ‘kuu, nishinde katika vyote Dunia yote ikitingika, ahadi zake hazipunguki Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele Dunia yote ikitingika, ahadi zake hazipunguki Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele

Nakaa mbali ya udhalimu, hatia, dhambi, hukumu Na kwa imani nikisimama, adui atakimbia Nayo mawazo ya giza tupu hayatapata nafasi huko Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele Nayo mawazo ya giza tupu hayatapata nafasi huko Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele

Nafurahia baraka zote za ulimwengu wa roho Karama hizo nalizipewa katika kufa kwa Yesu Hakuna woga na shaka huko, hayatakuwa manung’uniko Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele Hakuna woga na shaka huko, hayatakuwa manung’uniko Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele Hakuna woga na shaka huko, hayatakuwa manung’uniko Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele

Video

MWOKOZI WANGU NI MWAMBA BORA - PAPI CLEVER & DORCAS Ft MERCI PIANIST : MORNING WORSHIP 150

Thumbnail for Mwokozi Wangu Ni mMwamba Bora video
Loading...
In Queue
View Lyrics