Sifa Lyrics

E’ Mungu Mwenye Haki by PaPi Clever & Dorcas cover art

PaPi Clever & Dorcas - E’ Mungu Mwenye Haki Lyrics

Artist:
PaPi Clever & Dorcas

Lyrics

E’ Mungu mwenye haki, uniongoze huku
Katika mambo yote yanayokupendeza
Nikiwa huku bila wewe, vitisho hofu na mashaka
Yananitia tetemeko mpaka kufa
Nikiwa huku bila wewe, vitisho hofu na mashaka
Yananitia tetemeko mpaka kufa


Ni heri siku zote kutegemea Yesu
Na kuenenda sawa katika nyayo zake
Kwa kuwa yeye ni mchunga anayeniongoza vema
Nipate kuingia katika raha yake
Kwa kuwa yeye ni mchunga anayeniongoza vema
Nipate kuingia katika raha yake


Safari yangu sasa yaelekea mbingu
Mwokozi yuko huko, lazima nifikeko
Na siku nitakapofika ‘tashangilia kwa furaha
Kuona yeye aliyeninunua kwake
Na siku nitakapofika ‘tashangilia kwa furaha
Kuona yeye aliyeninunua kwake


Ulimwenguni humu, matata na kuchoka
Nikihitaji kitu nafadhahika bure
Lakini siku ile kuu nita’pomwona Mwokozi
Natumaini sitakosa dhawabu yangu
Lakini siku ile kuu nita’pomwona Mwokozi
Natumaini sitakosa dhawabu yangu


Mbinguni sitaona adui zangu tena
Hayatakuwa mambo yakupokonya pale
Mbinguni sitaona adui zangu tena
Hayatakuwa mambo yakupokonya pale
Sauti nitamtolea, kusema: Mungu, haleluya
Mikono nitaipepea kwa shangwe kuu
Sauti nitamtolea, kusema: Mungu, haleluya
Mikono nitaipepea kwa shangwe kuu


Video