Kidum - Pokea Sifa (Uhimidiwe) Lyrics

Contents:

Pokea Sifa (Uhimidiwe) Lyrics

Oh oh oh, ah ah ah
Oh oh oh, ah ah ah

Nimekuja hapa mbele zako bwana
Kukupee sifa
Ninajua kwamba niko mwenye dhambi
Naomba unisamehe

Utukufu wako hauna kifani
Huruma na upendo wako kwa walimwengu
Hulinganishwi na chochote 
Baba wetu

Unapea mvua, wabaya na wazuri
Na mwangaza wa jua kwa wabaya na wazuri
Hubagui baba

Baba Baba pokea sifa, uhimidiwe
Baba Baba pokea sifa, uabudiwe

Watu wengi duniani wamekata tamaa
Wanadhani wakija kwako utawafukuza
Wanasema wewe ni Mungu wa walio wema tu
Wanasema wewe ni Mungu wa matajiri tu
Wanasema wewe ni Mungu wa mataifa yenye nguvu
Lakini

Kumbe wamekosa mwenye kuwapa ukweli
Kumbe hawajui wewe ni mwenye huruma
Kumbe wamekosa mwenye kuwapa ukweli
Kumbe hawajui wewe ni mwenye huruma

Niko hapa kutoa ushuhuda 
Na kukupa sifa zako baba

Baba Baba pokea sifa, uhimidiwe
Baba Baba pokea sifa, uabudiwe
Baba Baba pokea sifa, uhimidiwe
Baba Baba pokea sifa, uabudiwe

Kumbe wamekosa mwenye kuwapa ukweli
Kumbe hawajui wewe ni mwenye huruma
Kumbe wamekosa mwenye kuwapa ukweli
Kumbe hawajui wewe ni mwenye huruma

Baba Baba pokea sifa, uhimidiwe
Baba Baba pokea sifa, uabudiwe
Baba Baba pokea sifa, uhimidiwe
Baba Baba pokea sifa, uabudiwe


Kidum Songs

Related Songs