Jessica Honore - Nakuamini Lyrics

Lyrics

Hata tusipokuamini Wewe utabakia wa kuaminiwa Heri mimi kukuamini Maana umedhibitika wa kuaminiwa

Hakuna mtihani ule uliitwa Kwako ukakosa jibiwa Na hakuna jibu ulotoa Likakosa jitosheleza

Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kipofu kwa fimbo yake Sitakuacha ehe 

Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kichanga kwa mama yake

Kuna wakati ulinisubirisha Nusura nikate tamaa Nikakumbuka wako wema Imani yangu ikainuka

Kumbe ulikuwa waniimarisha Hatua zangu kuzisogeza Sasa mwendo nimeuanza Na imani yangu kwako imesimama

Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kipofu kwa fimbo yake Sitakuacha ehe 

Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kichanga kwa mama yake

Naamini nguvu zako Naamini uwezo wako Upendo ni sifa yako

Naamini kazi zako Naamini neno lako Na yote uyafanyayo

Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kipofu kwa fimbo yake Sitakuacha ehe 

Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kichanga kwa mama yake Sitakuacha ehe 

Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kipofu kwa fimbo yake Sitakuacha ehe 

Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kichanga kwa mama yake Sitakuacha ehe 

Video

Nakuamini

Thumbnail for Nakuamini video
Loading...
In Queue
View Lyrics