Jessica Honore - Nakuamini Lyrics
Lyrics
Hata tusipokuamini Wewe utabakia wa kuaminiwa Heri mimi kukuamini Maana umedhibitika wa kuaminiwa
Hakuna mtihani ule uliitwa Kwako ukakosa jibiwa Na hakuna jibu ulotoa Likakosa jitosheleza
Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kipofu kwa fimbo yake Sitakuacha ehe
Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kichanga kwa mama yake
Kuna wakati ulinisubirisha Nusura nikate tamaa Nikakumbuka wako wema Imani yangu ikainuka
Kumbe ulikuwa waniimarisha Hatua zangu kuzisogeza Sasa mwendo nimeuanza Na imani yangu kwako imesimama
Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kipofu kwa fimbo yake Sitakuacha ehe
Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kichanga kwa mama yake
Naamini nguvu zako Naamini uwezo wako Upendo ni sifa yako
Naamini kazi zako Naamini neno lako Na yote uyafanyayo
Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kipofu kwa fimbo yake Sitakuacha ehe
Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kichanga kwa mama yake Sitakuacha ehe
Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kipofu kwa fimbo yake Sitakuacha ehe
Nakuamini Yesu ee Kiongozi wangu bora ee Kama kichanga kwa mama yake Sitakuacha ehe
Video
Nakuamini