Jessica Honore - Nakuamini Lyrics

Contents:

Nakuamini Lyrics

Hata tusipokuamini
Wewe utabakia wa kuaminiwa
Heri mimi kukuamini
Maana umedhibitika wa kuaminiwa

Hakuna mtihani ule uliitwa
Kwako ukakosa jibiwa
Na hakuna jibu ulotoa
Likakosa jitosheleza

Nakuamini Yesu ee
Kiongozi wangu bora ee
Kama kipofu kwa fimbo yake
Sitakuacha ehe 

Nakuamini Yesu ee
Kiongozi wangu bora ee
Kama kichanga kwa mama yake

Kuna wakati ulinisubirisha
Nusura nikate tamaa
Nikakumbuka wako wema
Imani yangu ikainuka

Kumbe ulikuwa waniimarisha
Hatua zangu kuzisogeza
Sasa mwendo nimeuanza
Na imani yangu kwako imesimama

Nakuamini Yesu ee
Kiongozi wangu bora ee
Kama kipofu kwa fimbo yake
Sitakuacha ehe 

Nakuamini Yesu ee
Kiongozi wangu bora ee
Kama kichanga kwa mama yake

Naamini nguvu zako
Naamini uwezo wako
Upendo ni sifa yako

Naamini kazi zako
Naamini neno lako
Na yote uyafanyayo

Nakuamini Yesu ee
Kiongozi wangu bora ee
Kama kipofu kwa fimbo yake
Sitakuacha ehe 

Nakuamini Yesu ee
Kiongozi wangu bora ee
Kama kichanga kwa mama yake
Sitakuacha ehe 

Nakuamini Yesu ee
Kiongozi wangu bora ee
Kama kipofu kwa fimbo yake
Sitakuacha ehe 

Nakuamini Yesu ee
Kiongozi wangu bora ee
Kama kichanga kwa mama yake
Sitakuacha ehe 


Jessica Honore Songs

Related Songs