Jessica Honore - Nitatulia Lyrics
Lyrics
Bwana wangu, jabari langu Uzima wangu, amani yangu Jibu langu
Nitatulia, nitanyamaza Ahadi zako Mungu zinatimia Nitanyamaza, nitatulia Ahadi zako Mungu zinatimia
Eeh Baba, eeeh Yahweh
Umesema nitulie, niuone mkono wako Maana ahadi zako zinatimia Mavumbini wainua, na wakuu waketisha Ahadi zako Mungu zinatimia
Nitatulia, nitanyamaza Ahadi zako Mungu zinatimia Nitatulia , Nitanyamaza Ahadi zako Mungu zinatimia
Ooh, Hallelujah, Hallelujah
Wewe hauwahi wala hauchelewi Unajibu kwa wakati unatimiza Jibu lako ni ndio na tena Amina Ila kuna kusubiri, unatimiza
Nitatulia Nitanyamaza Ahadi zako Mungu zinatimia Nitatulia , Nitanyamaza Ahadi zako Mungu zinatimia
Ukisema ndio, hakuna wa kupinga Neno halirudi bure Unatimiza Mtetezi wangu, pigana vita vyangu Na ijulikane upo, Mungu pamoja Nami
Mtetezi wangu pigana vita vyangu Na ijulikane upo Mungu pamoja Nami
Nitatulia, nitanyamaza Ahadi zako Mungu zinatimia Nitatulia, nitanyamaza Ahadi zako Mungu zinatimia
Unatimiza..... (Still Alive)
Video
Jessica Honore (NITATULIA LIVE)