Goodluck Gozbert - Wastahili Sifa Lyrics

Contents:

Wastahili Sifa Lyrics

Nasi tunainua sauti zetu kukusifu iushie milele
Hallelujah
Umeumba jambo jipya la sifa
Umeumba jambo jipya la sifa
Bwana U mkuu mwenye kusifiwa sana
Bwana U mkuu, mwenye kusifiwa sana
Tunakuabudu Yesu (Yesu)
Wastahili sifa, za moyo wangu
Wastahili sifa, za moyo wangu

Bwana U mkuu (Hakuna tena mwingine kama wewe)
Mwenye kusifiwa sana (Wewe uishiye juu na kutamalaki milele)
Wewe U mkuu mwenye kusifiwa sana (Wewe ni Mungu mkuu)
Mwenye kusifiwa sana (Tunakupenda wastahili sifa peke yako)
Tunakuabudu Yesu (Tunakuabudu Yesu)

(Wastahili)
Wastahili sifa (Za moyo) za moyo wangu
(Wastahili)
Wastahili (wasta., wasta., wasta...)
Sifa za moyo wangu
(Wastahili)
Wastahili (eeh Bwana, Bwana, Bwana)
Sifa za moyo (Hallelujah) wangu
(Bwana, ooh ooh ooooh)
Wastahili sifa (Bwana) za moyo wangu

Falme na tawala zote za Dunia
Zinajua hakukuwepo na kamwe
Hakutakuwepo mwenye mamlaka
Wa kuzidisha Mbingu na Nchi
Isipokuwa wewe Mtakatifu
Eeh Bwana wa Majeshi
Mungu utawalae na kumiliki daima

Nasi tunaziinua na kupaza sauti zetu juu sana
Tukilitukuza jina lako eeh mwamba wa kale
Asante tena na tena eeh Bwana wa Majeshi
Sifa na utukufu vikurudie wewe peke yako
Ooh asante asante asante

Bwana U mkuu mwenye kusifiwa sana
(Hapana tena Mungu kama wewe)
Bwana U mkuu (eeh eh) mwenye kusifiwa sana (God, uuh uh)
Tunakuabudu (Yesu, Yesu) Yesu
Wastahili (tumekuja kukuadhimisha Bwana)

Sifa, za moyo (eeh eh) wangu (Uuh, yeah, yeah)
Wastahili (eeh, eh Bwana, Bwana, Bwana)
Sifa za (eeh, eh) moyo wangu (Ooh, oh Bwana)
Wastahili (tunaliinua jina lako takatifu) sifa
(Asante Mungu), za moyo wangu
(Asante kwa sababu peke yako unastahili sifa)
(Ooh, ooh, ooh)

Wastahili (Lord yes, yes, yes, ooh asante)
Za moyo wangu (ooh asante)
Wastahili (yes Lord, oh oh) sifa
Za moyo (ooh, ooh) wangu
Wastahili
(Asante Mfalme wa amani, asante Jehovah, asante Mungu Mkuu)
(Fadhili zako ni za milele, wewe ni Mungu uliye kweli)


Goodluck Gozbert Songs

Related Songs