Eunice Njeri - Nguvu Ya Msalaba Lyrics

Lyrics

Nguvu ya msalaba imeniweka Dhabihu hiyo Mungu mwenyewe alitoa Sababu anijali nguvu ya msalaba

Nimeoshwa nimetakaswa damu ya Yesu imeniokoa Gharama yangu Yesu amelipa kwa mapigo yake mimi nimepona Nimeokolewa nimekombolewa kwa damu Yako mi ni salama Sina wasiwasi wala huzuni ndani yako ni salama

Nguvu ya msalaba imeniweka Dhabihu hiyo Mungu mwenyewe alitoa Sababu anijali nguvu ya msalaba

Nina sababu ya kukupenda nina sababu kuwa ndani Yako Maisha yangu nayatoa kwako maisha yangu nayatoa kwako Naishi nina haki natembea ni halali kama si Yesu singelikuwa hai Asante Bwana kwa wokovu wasiwasi sina tena mimi nina hakika ya uhai

Nguvu ya msalaba imeniweka Dhabihu hiyo Mungu mwenyewe alitoa Sababu anijali nguvu ya msalaba

Ukiona mimi naimba imba ni nguvu msalaba Ukiona nikitembea ni nguvu msalaba Ukiona mimi siendi hepi tena ni nguvu msalaba Ukiona nikisifu nakuimba ni nguvu msalaba

Nguvu ya msalaba Nguvu ya msalaba imeniweka Dhabihu hiyo Mungu mwenyewe alitoa Sababu anijali nguvu ya msalaba

Eunice Njeri & Billy Frank

Video

Nguvu ya Msalaba - Eunice Njeri feat Billy Frank

Thumbnail for Nguvu Ya Msalaba video
Loading...
In Queue
View Lyrics