Eunice Njeri - Nguvu Ya Msalaba Lyrics
Lyrics
Nguvu ya msalaba imeniweka Dhabihu hiyo Mungu mwenyewe alitoa Sababu anijali nguvu ya msalaba
Nimeoshwa nimetakaswa damu ya Yesu imeniokoa Gharama yangu Yesu amelipa kwa mapigo yake mimi nimepona Nimeokolewa nimekombolewa kwa damu Yako mi ni salama Sina wasiwasi wala huzuni ndani yako ni salama
Nguvu ya msalaba imeniweka Dhabihu hiyo Mungu mwenyewe alitoa Sababu anijali nguvu ya msalaba
Nina sababu ya kukupenda nina sababu kuwa ndani Yako Maisha yangu nayatoa kwako maisha yangu nayatoa kwako Naishi nina haki natembea ni halali kama si Yesu singelikuwa hai Asante Bwana kwa wokovu wasiwasi sina tena mimi nina hakika ya uhai
Nguvu ya msalaba imeniweka Dhabihu hiyo Mungu mwenyewe alitoa Sababu anijali nguvu ya msalaba
Ukiona mimi naimba imba ni nguvu msalaba Ukiona nikitembea ni nguvu msalaba Ukiona mimi siendi hepi tena ni nguvu msalaba Ukiona nikisifu nakuimba ni nguvu msalaba
Nguvu ya msalaba Nguvu ya msalaba imeniweka Dhabihu hiyo Mungu mwenyewe alitoa Sababu anijali nguvu ya msalaba
Eunice Njeri & Billy Frank
Video
Nguvu ya Msalaba - Eunice Njeri feat Billy Frank