Eunice Njeri - Baba Natamani Kuwa Nawe Lyrics

Lyrics

Natamani, Baba natamani kuwa nawe
Kuishi nawe kukaa nawe, natamani Yesu wewe wanitosha, Bwana wangu nakutamani

Baba natamani uwe wangu niwe wako Chote kilicho changu kiwe ni chako pia Upendo wako kwangu Yesu ni kama moto Nimekukimbilia nisiabike milele lee Eh Baba

Baba natamani kuwa nawe
Kuishi nawe kukaa nawe, natamani Yesu wewe wanitosha, Bwana wangu nakutamani

Baba nimeona upendo wako sio kwa mbali Moyo wangu wafurahi ndani ya moyo wako Nitakuinua umekuwa mwema kwangu Pokea sifa Wewe umekuwa mwema kwangu, wewe mwema

Baba natamani kuwa nawe
Kuishi nawe kukaa nawe, natamani Yesu wewe wanitosha, Bwana wangu nakutamani

Nitakuita hadi moyo wangu uzimie Uniongoze kwenye mwamba ulio juu zaidi yangu Nitakuita Bwana wangu unisikie Ombi langu sifa zangu kilio changu Ninapoomba (wanisikia eeh), Ninapoimba (wanisikia eeh) Ninapolia mimi (wanisikia eeh), Ninapokuita, wanisikia eeh

Baba natamani kuwa nawe
Kuishi nawe kukaa nawe, natamani Yesu wewe wanitosha, Bwana wangu nakutamani

Video

Kaberere ft Eunice Njeri Natamani

Thumbnail for Baba Natamani Kuwa Nawe video
Loading...
In Queue
View Lyrics