Eunice Njeri - Baba Natamani Kuwa Nawe Lyrics
Lyrics
Natamani, Baba natamani kuwa nawe
Kuishi nawe kukaa nawe, natamani
Yesu wewe wanitosha, Bwana wangu nakutamani
Baba natamani uwe wangu niwe wako Chote kilicho changu kiwe ni chako pia Upendo wako kwangu Yesu ni kama moto Nimekukimbilia nisiabike milele lee Eh Baba
Baba natamani kuwa nawe
Kuishi nawe kukaa nawe, natamani
Yesu wewe wanitosha, Bwana wangu nakutamani
Baba nimeona upendo wako sio kwa mbali Moyo wangu wafurahi ndani ya moyo wako Nitakuinua umekuwa mwema kwangu Pokea sifa Wewe umekuwa mwema kwangu, wewe mwema
Baba natamani kuwa nawe
Kuishi nawe kukaa nawe, natamani
Yesu wewe wanitosha, Bwana wangu nakutamani
Nitakuita hadi moyo wangu uzimie Uniongoze kwenye mwamba ulio juu zaidi yangu Nitakuita Bwana wangu unisikie Ombi langu sifa zangu kilio changu Ninapoomba (wanisikia eeh), Ninapoimba (wanisikia eeh) Ninapolia mimi (wanisikia eeh), Ninapokuita, wanisikia eeh
Baba natamani kuwa nawe
Kuishi nawe kukaa nawe, natamani
Yesu wewe wanitosha, Bwana wangu nakutamani
Video
Kaberere ft Eunice Njeri Natamani