Zekaria 7 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zekaria 7 (Swahili) Zechariah 7 (English)

Ikawa katika mwaka wa nne wa mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria, siku ya nne ya mwezi wa kenda, yaani, Kisleu. Zekaria 7:1

It happened in the fourth year of king Darius that the word of Yahweh came to Zechariah in the fourth day of the ninth month, the month of Chislev.

Basi watu wa Betheli walikuwa wamewatuma Shareza na Regem-meleki, na watu wao, ili kuomba fadhili za Bwana, Zekaria 7:2

The people of Bethel sent Sharezer and Regem Melech, and their men, to entreat Yahweh's favor,

na kusema na makuhani wa nyumba ya Bwana wa majeshi, na hao manabii, ya kwamba, Je! Yanipasa kulia katika mwezi wa tano, na kujitenga na watu, kama nilivyofanya miaka hii mingi iliyopita? Zekaria 7:3

and to speak to the priests of the house of Yahweh of Hosts, and to the prophets, saying, "Should I weep in the fifth month, separating myself, as I have done these so many years?"

Ndipo neno la Bwana wa majeshi likanijia, kusema, Zekaria 7:4

Then the word of Yahweh of Hosts came to me, saying,

Waambie watu wote wa nchi, na hao makuhani, ukisema, Hapo mlipofunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na mwezi wa saba, katika miaka hiyo sabini, je! Mlinifungia mimi kwa lo lote; mlinifungia mimi? Zekaria 7:5

"Speak to all the people of the land, and to the priests, saying, 'When you fasted and mourned in the fifth and in the seventh month for these seventy years, did you at all fast to me, really to me?

Na wakati mlapo chakula na kunywa, je! Hamli kwa ajili ya nafsi zenu, na kunywa kwa ajili ya nafsi zenu? Zekaria 7:6

When you eat, and when you drink, don't you eat for yourselves, and drink for yourselves?

Je! Hayo siyo maneno aliyoyasema Bwana kwa vinywa vya manabii wa zamani, wakati Yerusalemu ulipokaliwa na watu na kufanikiwa, na miji yake iliyokuwa ikiuzunguka; na wakati ule ambao nchi ya Negebu na Shefela ilipokuwa ikikaliwa na watu? Zekaria 7:7

Aren't these the words which Yahweh proclaimed by the former prophets, when Jerusalem was inhabited and in prosperity, and its cities around her, and the South and the lowland were inhabited?'"

Kisha neno la Bwana likamjia Zekaria, kusema, Zekaria 7:8

The word of Yahweh came to Zechariah, saying,

Bwana wa majeshi amesema hivi, ya kwamba, Fanyeni hukumu za kweli, kila mtu na amwonee ndugu yake rehema na huruma; Zekaria 7:9

"Thus has Yahweh of Hosts spoken, saying, 'Execute true judgment, and show kindness and compassion every man to his brother.

tena msimdhulumu mjane, wala yatima, wala mgeni, wala maskini; wala mtu awaye yote miongoni mwenu asiwaze mabaya juu ya ndugu yake moyoni mwake. Zekaria 7:10

Don't oppress the widow, nor the fatherless, the foreigner, nor the poor; and let none of you devise evil against his brother in your heart.'

Lakini hao walikataa kusikiliza, wakageuza bega lao, wakaziba masikio yao ili wasisikie. Zekaria 7:11

But they refused to listen, and turned their backs, and stopped their ears, that they might not hear.

Naam, walifanya mioyo yao kuwa kama jiwe gumu, wasije wakaisikia sheria na maneno ya Bwana wa majeshi, aliyoyapeleka kwa roho yake kwa mkono wa manabii wa kwanza; kwa sababu hiyo ghadhabu kuu ikatoka kwa Bwana wa majeshi. Zekaria 7:12

Yes, they made their hearts as hard as flint, lest they might hear the law, and the words which Yahweh of Hosts had sent by his Spirit by the former prophets. Therefore great wrath came from Yahweh of Hosts.

Ikawa kwa sababu alilia, wao wasitake kusikiliza; basi, wao nao watalia, wala mimi sitasikiliza, asema Bwana wa majeshi. Zekaria 7:13

It has come to pass that, as he called, and they refused to listen, so they will call, and I will not listen," said Yahweh of Hosts;

Lakini nitawatawanya kwa upepo wa kisulisuli, katikati ya mataifa yote wasiowajua. Basi hivyo ndivyo ilivyokuwa ukiwa nchi baada yao, hata hapakuwa na mtu aliyepita kati yake, wala aliyerudi; maana waliifanya nchi iliyopendeza sana kuwa ukiwa. Zekaria 7:14

"but I will scatter them with a whirlwind among all the nations which they have not known. Thus the land was desolate after them, so that no man passed through nor returned: for they made the pleasant land desolate."