Zekaria 6 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zekaria 6 (Swahili) Zechariah 6 (English)

Nikainua macho yangu tena, nikaona, na tazama, yanatokea magari ya vita manne, yanatoka kati ya milima miwili, na milima hiyo ilikuwa ni milima ya shaba. Zekaria 6:1

Again I lifted up my eyes, and saw, and, behold, four chariots came out from between two mountains; and the mountains were mountains of brass.

Katika gari la kwanza walikuwa farasi wekundu; na katika gari la pili walikuwa farasi weusi; Zekaria 6:2

In the first chariot were red horses; in the second chariot black horses;

na katika gari la tatu walikuwa farasi weupe; na katika gari la nne walikuwa farasi wa rangi ya kijivujivu. Zekaria 6:3

in the third chariot white horses; and in the fourth chariot dappled horses, all of them powerful.

Nikajibu, nikamwuliza yule malaika aliyesema nami, Hawa ni nini, Bwana wangu? Zekaria 6:4

Then I asked the angel who talked with me, "What are these, my lord?"

Malaika akajibu, akaniambia, Hawa ni pepo nne za mbinguni, zitokeazo baada ya kusimama mbele za Bwana wa dunia yote. Zekaria 6:5

The angel answered me, "These are the four winds of the sky, which go forth from standing before the Lord of all the earth.

Gari lile lenye farasi weusi latoka kwenda hata nchi ya kaskazini; nao farasi weupe wakatoka wakafuata nyuma yao; na wale wa rangi ya kijivujivu wakatoka kwenda hata nchi ya kusini. Zekaria 6:6

The one with the black horses goes out toward the north country; and the white went out after them; and the dappled went forth toward the south country."

Na wale wekundu wakatoka, wakataka kwenda huko na huko katika dunia; naye akawaambia, Haya! Tokeni, mwende huko na huko katika dunia. Basi wakaenda huko na huko katika dunia. Zekaria 6:7

The strong went out, and sought to go that they might walk back and forth through the earth: and he said, "Go around and through the earth!" So they walked back and forth through the earth.

Ndipo akaniita, akaniambia akisema, Tazama, wale waendao mpaka nchi ya kaskazini wameituliza roho yangu katika nchi ya kaskazini. Zekaria 6:8

Then he called to me, and spoke to me, saying, "Behold, those who go toward the north country have quieted my spirit in the north country."

Neno la Bwana likanijia, kusema, Zekaria 6:9

The word of Yahweh came to me, saying,

Pokea vitu mikononi mwa baadhi ya watu waliohamishwa, yaani, Heldai, na Tobia, na Yedaya; na siku iyo hiyo enenda ukaingie katika nyumba ya Yosia, mwana wa Sefania, waliyoifikia kutoka Babeli; Zekaria 6:10

"Take of them of the captivity, even of Heldai, of Tobijah, and of Jedaiah; and come the same day, and go into the house of Josiah the son of Zephaniah, where they have come from Babylon.

naam, pokea fedha na dhahabu, ukafanye taji, ukamvike kichwani Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu; Zekaria 6:11

Yes, take silver and gold, and make crowns, and set them on the head of Joshua the son of Jehozadak, the high priest;

ukamwambie, ukisema, Bwana wa majeshi asema hivi, ya kwamba, Tazama, mtu huyu ndiye ambaye jina lake ni Chipukizi; naye atakua katika mahali pake, naye atalijenga hekalu la Bwana. Zekaria 6:12

and speak to him, saying, 'Thus says Yahweh of Hosts, "Behold, the man whose name is the Branch: and he shall grow up out of his place; and he shall build the temple of Yahweh;

Naam, yeye atalijenga hekalu la Bwana; naye atauchukua huo utukufu; ataketi akimiliki katika kiti chake cha enzi; na kutakuwa na kuhani katika kiti chake cha enzi; na shauri la amani litakuwa kati ya hao wawili. Zekaria 6:13

even he shall build the temple of Yahweh; and he shall bear the glory, and shall sit and rule on his throne; and he shall be a priest on his throne; and the counsel of peace shall be between them both.

Na hizo taji zitakuwa za Heldai, na Tobia, na Yedaya; na kwa fadhili za mwana wa Sefania; ziwe ukumbusho katika hekalu la Bwana. Zekaria 6:14

The crowns shall be to Helem, and to Tobijah, and to Jedaiah, and to Hen the son of Zephaniah, for a memorial in the temple of Yahweh.

Nao walio mbali watakuja na kujenga katika hekalu la Bwana, nanyi mtajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma kwenu. Na haya yatatokea, kama mkijitahidi kuitii sauti ya Bwana, Mungu wenu. Zekaria 6:15

Those who are far off shall come and build in the temple of Yahweh; and you shall know that Yahweh of hosts has sent me to you. This will happen, if you will diligently obey the voice of Yahweh your God."'"