Zekaria 10 Swahili & English
Listen/Download AudioZekaria 10 (Swahili) | Zechariah 10 (English) |
---|---|
Mwombeni Bwana mvua wakati wa masika, naam, Bwana afanyaye umeme, naye atawapa manyunyu ya mvua, kila mtu atapewa nyasi kondeni. Zekaria 10:1 |
Ask of Yahweh rain in the spring time, Yahweh who makes storm clouds, And he gives rain showers to everyone for the plants in the field. |
Kwa maana vinyago vimenena maneno ya ubatili, nao waaguzi wameona uongo; nao wameleta habari za ndoto za uongo, wafariji bure; kwa sababu hiyo waenda zao kama kondoo, wateswa, kwa sababu hapana mchungaji. Zekaria 10:2 |
For the teraphim have spoken vanity, and the diviners have seen a lie; And they have told false dreams. They comfort in vain. Therefore they go their way like sheep. They are oppressed, because there is no shepherd. |
Hasira yangu imewaka juu ya wachungaji, nami nitawaadhibu mbuzi waume; kwa maana Bwana wa majeshi ameliangalia kundi lake, yaani, nyumba ya Yuda, naye atawafanya kuwa kama farasi wake mzuri vitani. Zekaria 10:3 |
My anger is kindled against the shepherds, And I will punish the male goats; For Yahweh of Hosts has visited his flock, the house of Judah, And will make them as his horse in the battle that he is proud of. |
Kwake yeye litatoka lile jiwe la pembeni, kwake yeye utatoka msumari, kwake yeye utatoka upinde wa vita, kwake yeye atatoka kila mtawala pamoja. Zekaria 10:4 |
From him will come forth the corner-stone, From him the nail, From him the battle bow, From him every ruler together. |
Nao watakuwa kama mashujaa, wakanyagao adui zao katika matope ya njia vitani; nao watapiga vita, kwa sababu Bwana yu pamoja nao; na hao wapandao farasi watafadhaishwa. Zekaria 10:5 |
They shall be as mighty men, Treading down muddy streets in the battle; And they shall fight, because Yahweh is with them; And the riders on horses will be confounded. |
Nami nitaitia nguvu nyumba ya Yuda, nami nitaiokoa nyumba ya Yusufu, nami nitawarudisha, kwa maana nawaonea rehema; nao watakuwa kana kwamba sikuwatupa; kwa maana mimi ni Bwana, Mungu wao, nami nitawasikia. Zekaria 10:6 |
"I will strengthen the house of Judah, And I will save the house of Joseph, And I will bring them back; For I have mercy on them; And they will be as though I had not cast them off: For I am Yahweh their God, and I will hear them. |
Na watu wa Efraimu watakuwa kama shujaa, na moyo wao utafurahi kana kwamba ni kwa divai; naam, watoto wao wataona mambo haya, na kufurahi; mioyo yao itamfurahia Bwana. Zekaria 10:7 |
Ephraim will be like a mighty man, And their heart will rejoice as through wine; Yes, their children will see it, and rejoice. Their heart will be glad in Yahweh. |
Nitawapigia kelele, na kuwakusanya pamoja; kwa maana nimewakomboa; nao wataongezeka kama walivyoongezeka. Zekaria 10:8 |
I will signal for them, and gather them; For I have redeemed them; And they will increase as they have increased. |
Nami nitawapanda kama mbegu kati ya mataifa; nao watanikumbuka katika nchi zilizo mbali; nao watakaa pamoja na watoto wao; tena watarudi. Zekaria 10:9 |
I will sow them among the peoples; And they will remember me in far countries; And they will live with their children, and will return. |
Tena nitawarudisha toka nchi ya Misri, nitawakusanya na kuwatoa katika Ashuru; nami nitawaingiza katika nchi ya Gileadi na Lebanoni; ila nafasi ya kuwatosha haitaonekana. Zekaria 10:10 |
I will bring them again also out of the land of Egypt, And gather them out of Assyria; And I will bring them into the land of Gilead and Lebanon; And there won't be room enough for them. |
Naye atapita kati ya bahari ya mateso, na kuyapiga mawimbi ya bahari, na vilindi vyote vya mto wa Nile vitakauka; na kiburi cha Ashuru kitashushwa; na fimbo ya enzi ya Misri itatoweka. Zekaria 10:11 |
He will pass through the sea of affliction, And will strike the waves in the sea, And all the depths of the Nile will dry up; And the pride of Assyria will be brought down, And the scepter of Egypt will depart. |
Nami nitawatia nguvu katika Bwana; nao watatembea huko na huko katika jina lake, asema Bwana. Zekaria 10:12 |
I will strengthen them in Yahweh; And they will walk up and down in his name," says Yahweh. |