Zekaria 1 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zekaria 1 (Swahili) Zechariah 1 (English)

Katika mwezi wa nane, mwaka wa pili wa Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria, mwana wa Berekia, mwana wa Ido, nabii, kusema, Zekaria 1:1

In the eighth month, in the second year of Darius, the word of Yahweh came to Zechariah the son of Berechiah, the son of Iddo, the prophet, saying,

Bwana amewakasirikia sana baba zenu. Zekaria 1:2

"Yahweh was very displeased with your fathers.

Basi, uwaambie, Bwana wa majeshi asema hivi, Nirudieni mimi, asema Bwana wa majeshi, nami nitawarudia ninyi, asema Bwana wa majeshi. Zekaria 1:3

Therefore tell them: Thus says Yahweh of Hosts: 'Return to me,' says Yahweh of Hosts, 'and I will return to you,' says Yahweh of Hosts.

Msiwe ninyi kama baba zenu, ambao manabii wa zamani waliwalilia, wakisema, Bwana wa majeshi asema hivi, Rudini sasa, na kuziacha njia zenu mbovu, na matendo yenu maovu; lakini hawakusikia, wala kunisikiliza, asema Bwana. Zekaria 1:4

Don't you be like your fathers, to whom the former prophets proclaimed, saying: Thus says Yahweh of hosts, 'Return now from your evil ways, and from your evil doings;' but they did not hear, nor listen to me, says Yahweh.

Je! Baba zenu wako wapi? Nao manabii je! Waishi milele? Zekaria 1:5

Your fathers, where are they? And the prophets, do they live forever?

Lakini maneno yangu, na amri zangu nilizowaagiza hao manabii, watumishi wangu, je! Hazikuwapata baba zenu? Nao wakageuka na kusema, Vile vile kama Bwana wa majeshi alivyoazimia kututenda, sawasawa na njia zetu, na sawasawa na matendo yetu, ndivyo alivyotutenda. Zekaria 1:6

But my words and my decrees, which I commanded my servants the prophets, didn't they overtake your fathers? "Then they repented and said, 'Just as Yahweh of Hosts determined to do to us, according to our ways, and according to our practices, so he has dealt with us.'"

Siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani, mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria, mwana wa Berekia, mwana wa Ido, nabii, kusema, Zekaria 1:7

On the twenty-fourth day of the eleventh month, which is the month Shebat, in the second year of Darius, the word of Yahweh came to Zechariah the son of Berechiah, the son of Iddo, the prophet, saying,

Naliona wakati wa usiku, na tazama, mtu amepanda farasi mwekundu, akasimama kati ya mihadasi iliyokuwa mahali penye uvuli; na nyuma yake walikuwapo farasi wengine wekundu, na wa rangi ya kijivujivu, na weupe. Zekaria 1:8

"I had a vision in the night, and, behold, a man riding on a red horse, and he stood among the myrtle trees that were in a ravine; and behind him there were red, brown, and white horses.

Ndipo nikasema, Ee Bwana wangu, ni nini hawa? Basi yule malaika aliyesema nami akaniambia, Nitakuonyesha ni nini hawa. Zekaria 1:9

Then I asked, 'My lord, what are these?'" The angel who talked with me said to me, "I will show you what these are."

Na yule mtu aliyesimama kati ya mihadasi akajibu, akasema, Hawa ndio Bwana aliowatuma, waende huko na huko duniani. Zekaria 1:10

The man who stood among the myrtle trees answered, "They are the ones Yahweh has sent to go back and forth through the earth."

Nao wakamjibu yule malaika wa Bwana aliyesimama kati ya mihadasi, wakasema, Tumekwenda huko na huko duniani, na tazama, dunia yote inatulia, nayo imestarehe. Zekaria 1:11

They reported to the angel of Yahweh who stood among the myrtle trees, and said, "We have walked back and forth through the earth, and, behold, all the earth is at rest and in peace."

Ndipo yule malaika wa Bwana akajibu, akasema, Ee Bwana wa majeshi, hata lini utakataa kuurehemu Yerusalemu, na miji ya Yuda uliyoikasirikia miaka hii sabini? Zekaria 1:12

Then the angel of Yahweh replied, "O Yahweh of Hosts, how long will you not have mercy on Jerusalem and on the cities of Judah, against which you have had indignation these seventy years?"

Naye Bwana akamjibu yule malaika aliyesema nami kwa maneno mazuri, maneno yenye faraja. Zekaria 1:13

Yahweh answered the angel who talked with me with kind and comforting words.

Basi yule malaika aliyesema nami akaniambia, Haya, piga kelele na kusema, Bwana wa majeshi asema hivi, Naona wivu kwa ajili ya Yerusalemu, na kwa ajili ya Sayuni; naona wivu mkuu sana. Zekaria 1:14

So the angel who talked with me said to me, "Proclaim, saying, 'Thus says Yahweh of Hosts: "I am jealous for Jerusalem and for Zion with a great jealousy.

Nami ninawakasirikia sana mataifa wanaokaa hali ya raha; kwa maana mimi sikukasirika ila kidogo tu, na wao waliyahimiza mateso. Zekaria 1:15

I am very angry with the nations that are at ease; for I was but a little displeased, but they added to the calamity."

Kwa sababu hiyo Bwana asema hivi, Ninaurudia Yerusalemu kwa rehema nyingi; nyumba yangu itajengwa ndani yake, asema Bwana wa majeshi, na kamba itanyoshwa juu ya Yerusalemu. Zekaria 1:16

Therefore thus says Yahweh: "I have returned to Jerusalem with mercy. My house shall be built in it," says Yahweh of Hosts, "and a line shall be stretched forth over Jerusalem."'

Piga kelele tena, na kusema, Bwana wa majeshi asema hivi, Miji yangu kwa kufanikiwa itaenezwa huko na huko tena; naye Bwana ataufariji Sayuni tena, atauchagua Yerusalemu tena. Zekaria 1:17

"Proclaim further, saying, 'Thus says Yahweh of Hosts: "My cities will again overflow with prosperity, and Yahweh will again comfort Zion, and will again choose Jerusalem."'"

Nami nikainua macho yangu, nikaona, na tazama, pembe nne. Zekaria 1:18

I lifted up my eyes, and saw, and, behold, four horns.

Nami nikamwuliza yule malaika aliyesema nami, Nini hizi? Naye akanijibu, Hizi ndizo pembe zilizowatawanya watu wa Yuda, na Israeli, na Yerusalemu. Zekaria 1:19

I asked the angel who talked with me, "What are these?" He answered me, "These are the horns which have scattered Judah, Israel, and Jerusalem."

Kisha Bwana akanionyesha wafua chuma wanne. Zekaria 1:20

Yahweh showed me four craftsmen.

Ndipo nikauliza Hawa wanakuja kufanya nini? Akasema kwamba, Hizi ndizo pembe zilizowatawanya watu wa Yuda, hata ikawa hakuna mtu aliyeinua kichwa chake; lakini hawa wamekuja kuzifukuza, kuziangusha pembe za mataifa, walioinua pembe yao juu ya nchi ya Yuda, ili kuwatawanya watu wake. Zekaria 1:21

Then I asked, "What are these coming to do?" He said, "These are the horns which scattered Judah, so that no man lifted up his head; but these have come to terrify them, to cast down the horns of the nations, which lifted up their horn against the land of Judah to scatter it."