Mika 7 Swahili & English

Listen/Download Audio
Mika 7 (Swahili) Micah 7 (English)

Ole wangu! Maana mimi ni kama hapo walipokwisha kuyachuma matunda ya wakati wa hari, kama zabibu zichumwazo baada ya mavuno; hapana shada la kuliwa; roho yangu inatamani tini iivayo kwanza. Mika 7:1

Misery is mine! Indeed, I am like one who gathers the summer fruits, as gleanings of the vinyard: There is no cluster of grapes to eat. My soul desires to eat the early fig.

Mtu amchaye Mungu ametoweka, asionekane katika nchi, wala hapana mtu mwenye adili katika wanadamu; wote huotea ili kumwaga damu; kila mtu humwinda ndugu yake kwa wavu. Mika 7:2

The godly man has perished out of the earth, And there is no one upright among men. They all lie in wait for blood; Every man hunts his brother with a net.

Mikono yao inayashika mabaya wayatende kwa bidii; mtu mkuu aomba rushwa, kadhi yu tayari kuipokea; mtu mkubwa hunena madhara yaliyomo rohoni mwake; hivyo ndivyo wayafumavyo hayo pamoja. Mika 7:3

Their hands are on that which is evil to do it diligently. The ruler and judge ask for a bribe; And the powerful man dictates the evil desire of his soul. Thus they conspire together.

Mtu aliye mwema miongoni mwao ni kama mbigili; mtu aliye mwenye adili miongoni mwao ni mbaya kuliko boma la michongoma; hiyo siku ya walinzi wako, yaani, siku ya kujiliwa kwako, imefika; sasa kutatokea kufadhaika kwao. Mika 7:4

The best of them is like a brier. The most upright is worse than a thorn hedge. The day of your watchmen, Even your visitation, has come; Now is the time of their confusion.

Msimwamini rafiki, msimwekee kiongozi tumaini; ilinde milango ya midomo ya kinywa chako ili mkeo alalaye kifuani mwako asijue habari. Mika 7:5

Don't trust in a neighbor. Don't put confidence in a friend. With the woman lying in your embrace, Be careful of the words of your mouth!

Kwa maana mwana humwaibisha babaye, na binti huondoka ashindane na mamaye; na mwanamke aliyeolewa hushindana na mavyaaye; adui za mtu ni watu wa nyumbani mwake mwenyewe. Mika 7:6

For the son dishonors the father, The daughter rises up against her mother, The daughter-in-law against her mother-in-law; A man's enemies are the men of his own house.

Lakini mimi, nitamtazamia Bwana; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia. Mika 7:7

But as for me, I will look to Yahweh. I will wait for the God of my salvation. My God will hear me.

Usifurahi juu yangu, Ee adui yangu; niangukapo, nitasimama tena; nikaapo gizani, Bwana atakuwa nuru kwangu. Mika 7:8

Don't rejoice against me, my enemy. When I fall, I will arise. When I sit in darkness, Yahweh will be a light to me.

Nitaivumilia ghadhabu ya Bwana, kwa kuwa nimemwasi; hata atakaponitetea teto langu, na kunifanyia hukumu; atanileta nje kwenye nuru, nami nitaiona haki yake. Mika 7:9

I will bear the indignation of Yahweh, Because I have sinned against him, Until he pleads my case, and executes judgment for me. He will bring me forth to the light. I will see his righteousness.

Ndipo adui yangu ataliona jambo hilo, na aibu itamfunika, yeye aliyeniambia, Yuko wapi Bwana, Mungu wako? Macho yangu yatamtazama; sasa atakanyagwa kama matope ya njia kuu. Mika 7:10

Then my enemy will see it, And shame will cover her who said to me, Where is Yahweh your God? Then my enemy will see me and will cover her shame. Now she will be trodden down like the mire of the streets.

Ni siku ya kujengwa kuta zako! Siku hiyo mpaka utasongezwa mbali. Mika 7:11

A day to build your walls-- In that day, he will extend your boundary.

Siku hiyo watakujia kutoka Ashuru na miji ya Misri, na kutoka Misri mpaka huo Mto, na kutoka bahari hii mpaka bahari hii, na kutoka mlima huu mpaka mlima huu. Mika 7:12

In that day they will come to you from Assyria and the cities of Egypt, And from Egypt even to the River, And from sea to sea, And mountain to mountain.

Hata hivyo nchi itakuwa ukiwa kwa sababu ya hao wakaao ndani yake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao. Mika 7:13

Yet the land will be desolate because of those who dwell therein, For the fruit of their doings.

Walishe watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, wakaao peke yao, mwituni katikati ya Karmeli; na walishe katika Bashani na Gileadi, kama siku za kale. Mika 7:14

Shepherd your people with your staff, The flock of your heritage, Who dwell by themselves in a forest, In the midst of fertile pasture land, let them feed; In Bashan and Gilead, as in the days of old.

Kama katika siku zile za kutoka kwako katika nchi ya Misri nitamwonyesha mambo ya ajabu. Mika 7:15

"As in the days of your coming forth out of the land of Egypt, I will show them marvelous things."

Mataifa wataona, na kuzitahayarikia nguvu zao zote; wataweka mikono yao juu ya vinywa vyao, masikio yao yatakuwa na uziwi. Mika 7:16

The nations will see and be ashamed of all their might. They will lay their hand on their mouth. Their ears will be deaf.

Watayaramba mavumbi kama nyoka, kama vitu vitambaavyo juu ya nchi watatoka katika mahali walimojificha, wakitetemeka; watakuja kwa Bwana, Mungu wetu, kwa hofu, nao wataogopa kwa sababu yako. Mika 7:17

They will lick the dust like a serpent. Like crawling things of the earth they shall come trembling out of their dens. They will come with fear to Yahweh our God, And will be afraid because of you.

Ni nani aliye Mungu kama wewe, mwenye kusamehe uovu, na kuliachilia kosa la watu wa urithi wake waliosalia? Hashiki hasira yake milele, kwa maana yeye hufurahia rehema. Mika 7:18

Who is a God like you, who pardons iniquity, And passes over the disobedience of the remnant of his heritage? He doesn't retain his anger forever, Because he delights in loving kindness.

Atarejea na kutuhurumia; atayakanyaga maovu yetu; nawe utazitupa dhambi zao zote katika vilindi vya bahari. Mika 7:19

He will again have compassion on us. He will tread our iniquities under foot; And you will cast all their sins into the depths of the sea.

Wewe utamtimilizia Yakobo kweli yako, na Ibrahimu rehema zako, ulizowaapia baba zetu tangu siku za kale. Mika 7:20

You will give truth to Jacob, and mercy to Abraham, As you have sworn to our fathers from the days of old.