Mika 5 Swahili & English

Listen/Download Audio
Mika 5 (Swahili) Micah 5 (English)

Sasa utajikusanya vikosi vikosi, Ee binti wa vikosi; yeye amemhusuru; watampiga mwamuzi wa Israeli shavuni mwake kwa fimbo. Mika 5:1

Now you shall gather yourself in troops, Daughter of troops. He has laid siege against us; They will strike the judge of Israel with a rod on the cheek.

Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele. Mika 5:2

But you, Bethlehem Ephrathah, Being small among the clans of Judah, Out of you one will come forth to me that is to be ruler in Israel; Whose goings forth are from of old, from everlasting.

Kwa sababu hiyo atawatoa, hata wakati wa kuzaa kwake aliye na utungu; ndipo hayo mabaki ya nduguze watawarudia wana wa Israeli. Mika 5:3

Therefore he will abandon them until the time that she who is in labor gives birth. Then the rest of his brothers will return to the children of Israel.

Naye atasimama, na kulisha kundi lake kwa nguvu za Bwana, kwa enzi ya jina la Bwana, Mungu wake; nao watakaa; maana sasa atakuwa mkuu hata miisho ya dunia. Mika 5:4

He shall stand, and shall shepherd in the strength of Yahweh, In the majesty of the name of Yahweh his God: And they will live, for then he will be great to the ends of the earth.

Na mtu huyu atakuwa amani yetu; wakati Mwashuri atakapoingia katika nchi yetu, na kuyakanyaga majumba yetu, hapo mtaondokesha wachungaji saba juu yake, na wakuu wanane. Mika 5:5

He will be our peace when Assyria invades our land, And when he marches through our fortresses, Then we will raise against him seven shepherds, And eight leaders of men.

Nao wataiharibu nchi ya Ashuru kwa upanga, na nchi ya Nimrodi katika malango yake; naye atatuokoa na Mwashuri, atakapoingia katika nchi yetu, na kukanyaga ndani ya mipaka yetu. Mika 5:6

They will rule the land of Assyria with the sword, And the land of Nimrod in its gates. He will deliver us from the Assyrian, When he invades our land, And when he marches within our border.

Na hayo mabaki ya Yakobo yatakuwa kati ya kabila nyingi mfano wa umande utokao kwa Bwana, mfano wa manyunyu katika manyasi; yasiyomngojea mtu, wala kuwakawilia wanadamu. Mika 5:7

The remnant of Jacob will be in the midst of many peoples, Like dew from Yahweh, Like showers on the grass, That don't wait for man, Nor wait for the sons of men.

Na hayo mabaki ya Yakobo yatakuwa kati ya mataifa, kati ya kabila nyingi, mfano wa simba kati ya wanyama wa msituni, kama mwana-simba kati ya makundi ya kondoo, ambaye, akiwa anapita katikati, hukanyaga-kanyaga na kurarua-rarua, wala hakuna wa kuokoa. Mika 5:8

The remnant of Jacob will be among the nations, In the midst of many peoples, Like a lion among the animals of the forest, Like a young lion among the flocks of sheep; Who, if he goes through, treads down and tears in pieces, And there is no one to deliver.

Mkono wako na uinuliwe juu ya adui zako, na adui zako wote wakauliwe mbali. Mika 5:9

Let your hand be lifted up above your adversaries, And let all of your enemies be cut off.

Kisha itakuwa katika siku hiyo, asema Bwana, nitawakatilia mbali farasi zako watoke kati yako, nami nitayaharibu magari yako ya vita; Mika 5:10

"It will happen in that day," says Yahweh, "That I will cut off your horses out of the midst of you, And will destroy your chariots.

nami nitaikatilia mbali miji ya nchi yako, na ngome zako zote nitaziangusha; Mika 5:11

I will cut off the cities of your land, And will tear down all your strongholds.

nami nitakatilia mbali uchawi, usiwe mkononi mwako; wala hutakuwa tena na watu wenye kutabana; Mika 5:12

I will destroy witchcraft from your hand; And you shall have no soothsayers.

nami nitakatilia mbali sanamu zako na nguzo zako, zitoke kati yako; wala hutaiabudu tena kazi ya mikono yako. Mika 5:13

I will cut off your engraved images and your pillars out of your midst; And you shall no more worship the work of your hands.

Nami nitayang'oa maashera yenu, yasiwe kati yako; nami nitaiangamiza miji yako. Mika 5:14

I will uproot your Asherim out of your midst; And I will destroy your cities.

Nami nitajilipiza kisasi katika hasira na ghadhabu juu ya mataifa wasiosikiliza. Mika 5:15

I will execute vengeance in anger, And wrath on the nations that didn't listen."