Walter Chilambo - Usinipite Lyrics
Lyrics
Ee Bwana nainamisha kichwa changu Ninakuabudu we Na tena nainua mikono yangu Kukuadhimisha we
Na ninashuka kwa unyenyekevu Madhahabuni pako Maana majibu ya maswali yangu Baba nitapata kwako
Kwanza nahitaji rehema zako Nisafishe Bwana Kwa yale nayajua na nisoyajua Niwe safi Bwana ninaomba nehema yako Na kibali chako juu yangu wee Nitembee kifua mbele
Yesu unapozuru wengine usinipite Nikumbuke, usinipite Maombi yangu, usinipite Baba uyakumbuke, usinipite
Nyakati za majaribu, usinipite Uniguze, usinipite Ingawa mi si mkamilifu, usinipite Ah ah, usinipite
Natamani nikuone Yesu niguse vazi lako Natamani niwe Batimayo Unifumbue macho
Unifundishe maana we mwalimu wa imani Nitapita salama Maana akili zangu zimefika mwisho Tumaini lipo kwako bwana
Na unijaze roho wako mtakatifu Ashike fahamu zangu Nihisi niki kulingana nawe Bwana
Maana wajua ninayoyapitia Nahitaji huruma yako Ee Mungu kadiri ya fadhili zako Usinipite
Ninaomba neema yako Zaidi nisimame nitangaze Uzuri wako bwana
Yesu unapozuru wengine usinipite Nikumbuke, usinipite Maombi yangu, usinipite Baba uyakumbuke, usinipite
Nyakati za majaribu, usinipite Uniguze, usinipite Ingawa mi si mkamilifu, usinipite Ah ah, usinipite
Maana hakuna nguvu ipitayo jina lako, usinipite Ni we unaweza, usinipite Navunja maagano yote Nikumbuke, usinipite
Adui ni mkali, usinipite We Yesu nakuomba, usinipite Ninapokosa tumaini, usinipite Unikumbuke, usinipite
Video
Walter Chilambo - Usinipite (Official Music Video) For SKIZA SMS 5960136 TO 811