Rose Muhando - Bado Lyrics

Lyrics

Niiii, niiini, niii? Niiii, niiini, niii? Je nataka kuwa na nini? Nauliza mnataka kuwa na nini? Wasomi mnataka kuwa na nini? Kanisa linataka kuwa na nini? Ndipo mjue yametimia

Dunia hey, kama kulemewa Imelema sana  Dunia hey, kama kuanguka Imeanguka sana 

Hivi mnataka kuwa na nini? Ndipo mjue yametimia  Dunia inataka kuwa na nini? Ndipo mjue Mungu anasema

Ona akili za wenye akili Zimefika kikomo jamani Maarifa ya wenye akili Yameshindwa kabisa Hekima ya wenye hekima haisaidii kitu

Hivi mnataka kuwa na nini? Nauliza mnataka muone nini? Ndivyo mjue Mungu anasema

Bado, bado, bado bado bado Kama ni mapito, bado bado  Kama ni magonjwa, bado bado  Kama timbwili timbwili, bado na bado  Kama ni heka heka, bado bado  Msishangazwe na ya leo, bado bado 

Baragumu ya kwanza imekwisha kupigwa Dunia ijipange  Baragumu ya kwanza imekwisha kulia Kanisa lijipange  Na hapa ndipo penye imani na subira Ya watakatifu wajipange  Wenye masikio na wasikie neno hili Roho asema mjipange Na bado, bado, bado ni ishara tu

Basi inueni macho yenu Tazama vilele vimeinama Wafalme wamechanganyikiwa Wenye akili hawana la kufanya Manabii maono yamekoma Ufunuo maono yamekoma Ayaa sasa dunia yote mikono juu Semeni Mungu pekee ndiye Bwana 

Basi inueni macho yenu Tazama vilele vimeinama Wafalme wamechanganyikiwa Wenye akili hawana la kufanya Manabii maono yamekoma Ufunuo maono yamekoma, bado

Nani basi asimame, mbele za Mungu aseme Alete moja nyingine ashindane na Mungu tuone

Maneno ya Mungu kamwe hayatapita Nasema mjipange Kengele ya hatari imeshakwisha kulia Nasema mjipange Bado, bado, bado ni ishara tu

Bado, bado, bado bado bado Na magonjwa bado, bado bado bado  Na shida bado, bado bado bado Njaa na matetemeko, bado bado bado Msishangazwe na ya leo, bado bado bado Msisitishwe na ya leo, bado bado bado Ah nasema bado, bado bado bado Uwiii, bado bado bado

Video

Rose Muhando - Bado (Official Music Video) SMS SKIZA 76310049 TO 811

Thumbnail for Bado video
Loading...
In Queue
View Lyrics