Beda Andrew - Nguvu za Mungu Lyrics
Lyrics
Rafiki hivi unavyoniona Ni kwa neema tu Na hata uzima nilio nao Ni upendeleo tu
Na kufika hapa sio sababu ya kuwa Mimi ni mwema sana (Kuliko wale) Tena natambua kama si wake mkono Ningeshatumbukia shimoni na nipotee
Ninalindwa, kwa nguvu za Mungu Ni kwa nguvu za Mungu Si kwa ujanja wala akili zangu Ila ni kwa nguvu za Mungu
Ninalindwa, kwa nguvu za Mungu Ni kwa nguvu za Mungu Si kwa ujanja wala akili zangu Ila ni kwa nguvu za Mungu
Nia ya mwovu ni kutaka ona mi naangamia Kusudi la Mungu maishani mwangu nisipate timia Anatega mitego, ili mradi kuniangamiza Kunimaliza kunipoteza, ila Yahweh ananilinda
Nimeokolewa na ajali Magonjwa na kila hatari Mpaka sasa nipo hai Nakushukuru jemedari
Uzima wangu, hauko mikoni mwangu Uzima wangu, uko mikononi mwake
Kwa nguvu za Mungu Ni kwa nguvu za Mungu Kwa nguvu za Mungu Ni kwa nguvu za Mungu
Ni kwa nguvu za Mungu Si kwa ujanja wala akili zangu Ila ni kwa nguvu za Mungu
Ninalindwa, kwa nguvu za Mungu Ni kwa nguvu za Mungu Si kwa ujanja wala akili zangu Ila ni kwa nguvu za Mungu
Ninalindwa, kwa nguvu za Mungu Ni kwa nguvu za Mungu Si kwa ujanja wala akili zangu
Ni kwa neema tu za aliye juu Aliye juu ni Mungu mkuu Ni kwa neema tu za aliye juu Aliye juu ni Mungu mkuu
Ni kwa neema tu za aliye juu Aliye juu ni Mungu mkuu Ni kwa neema tu za aliye juu Aliye juu ni Mungu mkuu
Kwa nguvu za Mungu Ni kwa nguvu za Mungu Si kwa ujanja wala akili zangu Ila ni kwa nguvu za Mungu
Video
Beda Andrew - NGUVU ZA MUNGU (Official Music Video)