Kambua - Bado Nasimama Lyrics

Lyrics

Bado nasimama, bado naendelea Bado najikaza, nifike kule

Bila nehema na rehema zako, ningekuwa wapi mimi Bila upendo, na fadhili zako, maisha yangu yangekuwa bure Kwa wema wako, kanisimamisha Na imani yangu, ukaiweka salama Kama si wewe, Mwamba wa wokovu wangu Nisingeweza. ningeangamia

Nainua macho yangu kwako wewe Baba yangu Msaada wangu utatoka wapi Msaada wangu u katika bwana Hasinzii anilindaye, haniachi mimi niteleze Anipa nguvu, na uwezo wake Ili mimi nifike kule Nifike kule

Bado nasimama, bado naendelea Bado najikaza, nifike kule (x6)

Still Standing

Video

Kambua - Bado Nasimama (Official Music Video)

Thumbnail for Bado Nasimama video
Loading...
In Queue
View Lyrics