Wagalatia BSB

Wagalatia 3

Galatians Chapter 3

1
Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa?
O foolish Galatians! Who has bewitched you? Before your very eyes Jesus Christ was clearly portrayed as crucified.
2
Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani?
I would like to learn just one thing from you: Did you receive the Spirit by works of the law, or by hearing with faith?
3
Je! Mmekuwa wajinga namna hii? Baada ya kuanza katika Roho, mnataka kukamilishwa sasa katika mwili?
Are you so foolish? After starting in the Spirit, are you now finishing in the flesh?
4
Mmepatikana na mateso makubwa namna hii bure? Ikiwa ni bure kweli.
Have you suffered so much for nothing, if it really was for nothing?
5
Basi, yeye awapaye Roho na kufanya miujiza kati yenu, je! Afanya hayo kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani?
Does God lavish His Spirit on you and work miracles among you because you practice the law, or because you hear and believe?
6
Kama vile Ibrahimu alivyomwamini Mungu akahesabiwa haki.
So also, “Abraham believed God, and it was credited to him as righteousness.”
7
Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu.
Understand, then, that those who have faith are sons of Abraham.
8
Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe Mataifa yote watabarikiwa.
The Scripture foresaw that God would justify the Gentiles by faith, and foretold the gospel to Abraham: “All nations will be blessed through you.”
9
Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani.
So those who have faith are blessed along with Abraham, the man of faith.
10
Kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye.
All who rely on works of the law are under a curse. For it is written: “Cursed is everyone who does not continue to do everything written in the Book of the Law.”
11
Ni dhahiri ya kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa imani.
Now it is clear that no one is justified before God by the law, because, “The righteous will live by faith.”
12
Na torati haikuja kwa imani, bali, Ayatendaye hayo ataishi katika hayo.
The law, however, is not based on faith; on the contrary, “The man who does these things will live by them.”
13
Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;
Christ redeemed us from the curse of the law by becoming a curse for us. For it is written: “Cursed is everyone who is hung on a tree.”
14
ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.
He redeemed us in order that the blessing promised to Abraham would come to the Gentiles in Christ Jesus, so that by faith we might receive the promise of the Spirit.
15
Ndugu zangu, nanena kwa jinsi ya kibinadamu. Lijapokuwa ni agano la mwanadamu, hata hivyo likiisha kuthibitika, hakuna mtu alibatilishaye, wala kuliongeza neno.
Brothers, let me put this in human terms. Even a human covenant, once it is ratified, cannot be canceled or amended.
16
Basi ahadi zilinenwa kwa Ibrahimu na kwa mzao wake. Hasemi, Kwa wazao, kana kwamba ni wengi, bali kana kwamba ni mmoja, Kwa mzao wako, yaani, Kristo.
The promises were spoken to Abraham and to his seed. The Scripture does not say, “and to seeds,” meaning many, but “and to your seed,” meaning One, who is Christ.
17
Nisemalo ni hili; agano lililothibitishwa kwanza na Mungu, torati iliyotokea miaka mia nne na thelathini baadaye hailitangui, hata kuibatilisha ile ahadi.
What I mean is this: The law that came 430 years later does not revoke the covenant previously established by God, so as to nullify the promise.
18
Kwa maana urithi ukiwa kwa sheria, hauwi tena kwa ahadi; lakini Mungu alimkirimia Ibrahimu kwa njia ya ahadi.
For if the inheritance depends on the law, then it no longer depends on a promise; but God freely granted it to Abraham through a promise.
19
Torati ni nini basi? Iliingizwa kwa sababu ya makosa, hata aje huyo mzao aliyepewa ile ahadi; iliamriwa kwa utumishi wa malaika kwa mkono wa mjumbe.
Why then was the law given? It was added because of transgressions, until the arrival of the seed to whom the promise referred. It was administered through angels by a mediator.
20
Basi aliye mjumbe si mjumbe wa mmoja; bali Mungu ni mmoja.
A mediator is unnecessary, however, for only one party; but God is one.
21
Basi je! Torati haipatani na ahadi za Mungu? Hasha! Kwa kuwa, kama ingalitolewa sheria iwezayo kuhuisha, yakini haki ingalipatikana kwa sheria.
Is the law, then, opposed to the promises of God? Certainly not! For if a law had been given that could impart life, then righteousness would certainly have come from the law.
22
Lakini andiko limeyafunga yote chini ya nguvu ya dhambi, makusudi hao waaminio wapewe ile ahadi kwa imani ya Yesu Kristo.
But the Scripture pronounces all things confined by sin, so that by faith in Jesus Christ the promise might be given to those who believe.
23
Lakini kabla ya kuja ile imani tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ije ile imani itakayofunuliwa.
Before this faith came, we were held in custody under the law, locked up until faith should be revealed.
24
Hivyo torati imekuwa kiongozi kutuleta kwa Kristo, ili tuhesabiwe haki kwa imani.
So the law became our guardian to lead us to Christ, that we might be justified by faith.
25
Lakini, iwapo imani imekuja, hatupo tena chini ya kiongozi.
Now that faith has come, we are no longer under a guardian.
26
Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.
You are all sons of God through faith in Christ Jesus.
27
Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo.
For all of you who were baptized into Christ have clothed yourselves with Christ.
28
Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu.
There is neither Jew nor Greek, slave nor free, male nor female, for you are all one in Christ Jesus.
29
Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.
And if you belong to Christ, then you are Abraham’s seed and heirs according to the promise.

Chagua Sura

1 2 3 4 5 6