Wagalatia 3 Swahili & English

Listen/Download Audio
Wagalatia 3 (Swahili) Galatians 3 (English)

Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa? Wagalatia 3:1

Foolish Galatians, who has bewitched you not to obey the truth, before whose eyes Jesus Christ was openly set forth among you as crucified?

Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani? Wagalatia 3:2

I just want to learn this from you. Did you receive the Spirit by the works of the law, or by hearing of faith?

Je! Mmekuwa wajinga namna hii? Baada ya kuanza katika Roho, mnataka kukamilishwa sasa katika mwili? Wagalatia 3:3

Are you so foolish? Having begun in the Spirit, are you now completed in the flesh?

Mmepatikana na mateso makubwa namna hii bure? Ikiwa ni bure kweli. Wagalatia 3:4

Did you suffer so many things in vain, if it is indeed in vain?

Basi, yeye awapaye Roho na kufanya miujiza kati yenu, je! Afanya hayo kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani? Wagalatia 3:5

He therefore who supplies the Spirit to you, and works miracles among you, does he do it by the works of the law, or by hearing of faith?

Kama vile Ibrahimu alivyomwamini Mungu akahesabiwa haki. Wagalatia 3:6

Even as Abraham "believed God, and it was counted to him for righteousness."

Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu. Wagalatia 3:7

Know therefore that those who are of faith, the same are children of Abraham.

Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe Mataifa yote watabarikiwa. Wagalatia 3:8

The Scripture, foreseeing that God would justify the Gentiles by faith, preached the Gospel beforehand to Abraham, saying, "In you all the nations will be blessed."

Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani. Wagalatia 3:9

So then, those who are of faith are blessed with the faithful Abraham.

Kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye. Wagalatia 3:10

For as many as are of the works of the law are under a curse. For it is written, "Cursed is everyone who doesn't continue in all things that are written in the book of the law, to do them."

Ni dhahiri ya kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa imani. Wagalatia 3:11

Now that no man is justified by the law before God is evident, for, "The righteous will live by faith."

Na torati haikuja kwa imani, bali, Ayatendaye hayo ataishi katika hayo. Wagalatia 3:12

The law is not of faith, but, "The man who does them will live by them."

Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti; Wagalatia 3:13

Christ redeemed us from the curse of the law, having become a curse for us. For it is written, "Cursed is everyone who hangs on a tree,"

ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani. Wagalatia 3:14

that the blessing of Abraham might come on the Gentiles through Christ Jesus; that we might receive the promise of the Spirit through faith.

Ndugu zangu, nanena kwa jinsi ya kibinadamu. Lijapokuwa ni agano la mwanadamu, hata hivyo likiisha kuthibitika, hakuna mtu alibatilishaye, wala kuliongeza neno. Wagalatia 3:15

Brothers, I speak like men. Though it is only a man's covenant, yet when it has been confirmed, no one makes it void, or adds to it.

Basi ahadi zilinenwa kwa Ibrahimu na kwa mzao wake. Hasemi, Kwa wazao, kana kwamba ni wengi, bali kana kwamba ni mmoja, Kwa mzao wako, yaani, Kristo. Wagalatia 3:16

Now the promises were spoken to Abraham and to his seed. He doesn't say, "To seeds," as of many, but as of one, "To your seed," which is Christ.

Nisemalo ni hili; agano lililothibitishwa kwanza na Mungu, torati iliyotokea miaka mia nne na thelathini baadaye hailitangui, hata kuibatilisha ile ahadi. Wagalatia 3:17

Now I say this. A covenant confirmed beforehand by God in Christ, the law, which came four hundred thirty years after, does not annul, so as to make the promise of no effect.

Kwa maana urithi ukiwa kwa sheria, hauwi tena kwa ahadi; lakini Mungu alimkirimia Ibrahimu kwa njia ya ahadi. Wagalatia 3:18

For if the inheritance is of the law, it is no more of promise; but God has granted it to Abraham by promise.

Torati ni nini basi? Iliingizwa kwa sababu ya makosa, hata aje huyo mzao aliyepewa ile ahadi; iliamriwa kwa utumishi wa malaika kwa mkono wa mjumbe. Wagalatia 3:19

What then is the law? It was added because of transgressions, until the seed should come to whom the promise has been made. It was ordained through angels by the hand of a mediator.

Basi aliye mjumbe si mjumbe wa mmoja; bali Mungu ni mmoja. Wagalatia 3:20

Now a mediator is not between one, but God is one.

Basi je! Torati haipatani na ahadi za Mungu? Hasha! Kwa kuwa, kama ingalitolewa sheria iwezayo kuhuisha, yakini haki ingalipatikana kwa sheria. Wagalatia 3:21

Is the law then against the promises of God? Certainly not! For if there had been a law given which could make alive, most assuredly righteousness would have been of the law.

Lakini andiko limeyafunga yote chini ya nguvu ya dhambi, makusudi hao waaminio wapewe ile ahadi kwa imani ya Yesu Kristo. Wagalatia 3:22

But the Scriptures shut up all things under sin, that the promise by faith in Jesus Christ might be given to those who believe.

Lakini kabla ya kuja ile imani tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ije ile imani itakayofunuliwa. Wagalatia 3:23

But before faith came, we were kept in custody under the law, shut up to the faith which should afterwards be revealed.

Hivyo torati imekuwa kiongozi kutuleta kwa Kristo, ili tuhesabiwe haki kwa imani. Wagalatia 3:24

So that the law has become our tutor to bring us to Christ, that we might be justified by faith.

Lakini, iwapo imani imekuja, hatupo tena chini ya kiongozi. Wagalatia 3:25

But now that faith has come, we are no longer under a tutor.

Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu. Wagalatia 3:26

For you are all children of God, through faith in Christ Jesus.

Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo. Wagalatia 3:27

For as many of you as were baptized into Christ have put on Christ.

Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu. Wagalatia 3:28

There is neither Jew nor Greek, there is neither slave nor free man, there is neither male nor female; for you are all one in Christ Jesus.

Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi. Wagalatia 3:29

If you are Christ's, then you are Abraham's seed and heirs according to promise.