Esta 4 Swahili & English

Listen/Download Audio
Esta 4 (Swahili) Esther 4 (English)

Basi Mordeikai alipojua mambo yote yaliyofanyika, alizirarua nguo zake, akajivika gunia pamoja na majivu, akatoka hata kufika katikati ya mji, akalia kwa sauti kuu ya uchungu. Esta 4:1

Now when Mordecai knew all that was done, Mordecai tore his clothes, and put on sackcloth with ashes, and went out into the midst of the city, and cried with a loud and a bitter cry;

Pia akafika hata mbele ya mlango wa mfalme; maana hakuna awezaye kuingia ndani ya mlango wa mfalme hali amevaa magunia. Esta 4:2

and he came even before the king's gate: for none might enter within the king's gate clothed with sackcloth.

Na katika kila jimbo, ambako amri ya mfalme na mbiu yake imewasili, palikuwako msiba mkuu kwa Wayahudi, na kufunga, na kulia, na kuomboleza; hata na wengi wakalala juu ya gunia na majivu. Esta 4:3

In every province, wherever the king's commandment and his decree came, there was great mourning among the Jews, and fasting, and weeping, and wailing; and many lay in sackcloth and ashes.

Basi wajakazi wake Esta, na wasimamizi wake wa nyumba, wakamjia, wakampasha habari; naye malkia akahuzunika mno; akampelekea Mordekai mavazi, ili kumvika, na kumwondolea gunia lake; walakini yeye asikubali. Esta 4:4

Esther's maidens and her chamberlains came and told it her; and the queen was exceedingly grieved: and she sent clothing to clothe Mordecai, and to take his sackcloth from off him; but he didn't receive it.

Kisha Esta akamwita Hathaki, msimamizi-wa-nyumba mmojawapo wa mfalme, aliyemwagiza amhudumu Esta, akamtuma kwa Mordekai, ili ajue mambo hayo, na maana yake ni nini. Esta 4:5

Then called Esther for Hathach, one of the king's chamberlains, whom he had appointed to attend on her, and charged him to go to Mordecai, to know what this was, and why it was.

Basi yule Hathaki akatoka nje kumwendea Mordekai kwenye uwanda wa mji ulipo mbele ya mlango wa mfalme. Esta 4:6

So Hathach went forth to Mordecai to the broad place of the city, which was before the king's gate.

Naye Mordekai akamweleza yote yaliyompata, na hesabu ya fedha Hamani aliyoahidi kulipa katika hazina ya mfalme, ili Wayahudi waangamizwe. Esta 4:7

Mordecai told him of all that had happened to him, and the exact sum of the money that Haman had promised to pay to the king's treasuries for the Jews, to destroy them.

Pia akampa na nakili ya andiko la mbiu ya kuwaangamiza, iliyotangazwa Shushani, ili amwonyeshe Esta, na kumweleza; tena amwagize aingie kwa mfalme, kumsihi na kuwaombea watu wake. Esta 4:8

Also he gave him the copy of the writing of the decree that was given out in Shushan to destroy them, to show it to Esther, and to declare it to her, and to charge her that she should go in to the king, to make supplication to him, and to make request before him, for her people.

Basi Hathaki akaja, akamwambia Esta maneno ya Mordekai. Esta 4:9

Hathach came and told Esther the words of Mordecai.

Ndipo Esta akasema na Hathaki, akamtuma tena kwa Mordekai, kusema, Esta 4:10

Then Esther spoke to Hathach, and gave him a message to Mordecai [saying]:

Watumwa wote wa mfalme wanajua sana, hata na watu wa majimbo ya mfalme, ya kwamba mtu ye yote, akiwa mwanamume au mwanamke, atakayemjia mfalme katika ua wa ndani, wala hakuitwa, kuna sheria moja kwake, ni kwamba auawe; isipokuwa yeye ambaye mfalme atamnyoshea fimbo ya dhahabu, ili aishi; wala mimi sikuitwa niingie kwa mfalme yapata siku thelathini. Esta 4:11

All the king's servants, and the people of the king's provinces, do know, that whoever, whether man or woman, shall come to the king into the inner court, who is not called, there is one law for him, that he be put to death, except those to whom the king shall hold out the golden scepter, that he may live: but I have not been called to come in to the king these thirty days.

Basi wakamwambia Mordekai maneno ya Esta. Esta 4:12

They told to Mordecai Esther's words.

Naye Mordekai akawaagiza wampelekee Esta jibu la kusema, Wewe usijidhanie kuwa wewe utaokoka nyumbani mwa mfalme, zaidi ya Wayahudi wote. Esta 4:13

Then Mordecai bade them return answer to Esther, Don't think to yourself that you shall escape in the king's house, more than all the Jews.

Kwa maana wewe ukinyamaza kabisa wakati huu, ndipo kutakapowatokea Wayahudi msaada na wokovu kwa njia nyingine; ila wewe utaangamia pamoja na mlango wote wa baba yako; walakini ni nani ajuaye kama wewe hukuujia ufalme kwa ajili ya wakati kama huo? Esta 4:14

For if you altogether hold your peace at this time, then will relief and deliverance arise to the Jews from another place, but you and your father's house will perish: and who knows whether you haven't come to the kingdom for such a time as this?

Basi Esta akawatuma ili wamjibu Mordekai, Esta 4:15

Then Esther bade them return answer to Mordecai,

Uende ukawakusanye Wayahudi wote waliopo hapa Shushani, mkafunge kwa ajili yangu; msile wala kunywa muda wa siku tatu, usiku wala mchana, nami na wajakazi wangu tutafunga vile vile; kisha nitaingia kwa mfalme, kinyume cha sheria; nami nikiangamia, na niangamie. Esta 4:16

Go, gather together all the Jews who are present in Shushan, and fast you for me, and neither eat nor drink three days, night or day: I also and my maidens will fast in like manner; and so will I go in to the king, which is not according to the law: and if I perish, I perish.

Basi Mordekai akaenda zake, akafanya yote kama vile Esta alivyomwagiza. Esta 4:17

So Mordecai went his way, and did according to all that Esther had commanded him.