Esta 1 Swahili & English

Listen/Download Audio
Esta 1 (Swahili) Esther 1 (English)

Zamani za Ahasuero; naye huyu Ahasuero alimiliki toka Bara Hindi mpaka Kushi, juu ya majimbo mia na ishirini na saba; Esta 1:1

Now it happened in the days of Ahasuerus (this is Ahasuerus who reigned from India even to Ethiopia, over one hundred twenty-seven provinces),

siku zile mfalme Ahasuero alipoketi katika kiti cha enzi cha ufalme wake, huko Shushani ngomeni; Esta 1:2

that in those days, when the king Ahasuerus sat on the throne of his kingdom, which was in Shushan the palace,

mwaka wa tatu wa kumiliki kwake, ikawa aliwafanyia karamu maakida wake wote na majumbe wake; wakuu wa Uajemi na Umedi, watu wenye cheo na maakida wa majimbo, wakihudhuria mbele zake. Esta 1:3

in the third year of his reign, he made a feast to all his princes and his servants; the power of Persia and Media, the nobles and princes of the provinces, being before him;

Akawaonyesha utajiri wa ufalme wake mtukufu, na heshima ya enzi yake bora siku nyingi, maana siku mia na themanini. Esta 1:4

when he shown the riches of his glorious kingdom and the honor of his excellent majesty many days, even one hundred eighty days.

Hata siku hizo zilipotimia, mfalme akawafanyia karamu watu wote waliokuwapo huko Shushani ngomeni, wakubwa kwa wadogo, muda wa siku saba, katika behewa la bustani ya ngome ya mfalme. Esta 1:5

When these days were fulfilled, the king made a feast to all the people who were present in Shushan the palace, both great and small, seven days, in the court of the garden of the king's palace.

Palikuwa na mapazia ya bafta, nyeupe na samawi, yamefungiwa kamba za kitani safi za rangi ya zambarau kwa pete za fedha na nguzo za marumaru; pia na vitanda vilikuwa vya dhahabu na fedha juu ya sakafu ya marumaru, mawe mekundu, na meupe, na ya manjano, na meusi. Esta 1:6

[There were hangings of] white [cloth], [of] green, and [of] blue, fastened with cords of fine linen and purple to silver rings and pillars of marble: the couches were of gold and silver, on a pavement of red, and white, and yellow, and black marble.

Wakawanywesha kileo katika vyombo vya dhahabu, na vile vyombo vilikuwa mbalimbali, na divai tele ya namna ya kifalme, sawasawa na ukarimu wa mfalme; Esta 1:7

They gave them drink in vessels of gold (the vessels being diverse one from another), and royal wine in abundance, according to the bounty of the king.

kunywa kulikuwa kama ilivyoamriwa, bila sharti; maana ndivyo mfalme alivyowaagiza watumishi-wa-nyumbani, kila mtu afanye apendavyo. Esta 1:8

The drinking was according to the law; none could compel: for so the king had appointed to all the officers of his house, that they should do according to every man's pleasure.

Tena Vashti, malkia, naye akawafanyia karamu wanawake ndani ya nyumba ya kifalme ya mfalme Ahasuero. Esta 1:9

Also Vashti the queen made a feast for the women in the royal house which belonged to king Ahasuerus.

Hata siku ya saba, mfalme alipofurahiwa moyo wake kwa divai, aliwaamuru Mehumani, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zethari, na Karkasi, wale wasimamizi-wa-nyumba saba waliohudumu mbele za mfalme Ahasuero, Esta 1:10

On the seventh day, when the heart of the king was merry with wine, he commanded Mehuman, Biztha, Harbona, Bigtha, and Abagtha, Zethar, and Carcass, the seven chamberlains who ministered in the presence of Ahasuerus the king,

wamlete Vashti, malkia, mbele ya mfalme, amevaa taji ya kifalme; ili kuwaonyesha watu na maakida uzuri wake, maana alikuwa mzuri wa uso. Esta 1:11

to bring Vashti the queen before the king with the crown royal, to show the peoples and the princes her beauty; for she was beautiful to look on.

Bali Vashti, malkia, alikataa kuja kwa amri ya mfalme kwa mkono wa wasimamizi-wa-nyumba; kwa hiyo mfalme akaghadhibika sana, na hasira yake ikawaka ndani yake. Esta 1:12

But the queen Vashti refused to come at the king's commandment by the chamberlains: therefore was the king very angry, and his anger burned in him.

Basi mfalme akawaambia wenye hekima, walio na elimu ya nyakati; maana ndivyo ilivyokuwa desturi ya mfalme kwa wote waliojua sheria na hukumu; Esta 1:13

Then the king said to the wise men, who knew the times, (for so was the king's manner toward all who knew law and judgment;

na karibu naye wameketi Karshena, Shethari, Admatha, Tarshishi, Meresi, Marsena, na Memukani, wale maakida saba wa Uajemi na Umedi, waliouona uso wa mfalme, na kuketi wa kwanza katika ufalme; akawauliza, Esta 1:14

and the next to him were Carshena, Shethar, Admatha, Tarshish, Meres, Marsena, and Memucan, the seven princes of Persia and Media, who saw the king's face, and sat first in the kingdom),

Tumfanyieje Vashti, malkia, kwa sheria, kwa sababu hakufanya kama vile alivyoamriwa na mfalme Ahasuero kwa mkono wa wasimamizi-wa-nyumba? Esta 1:15

What shall we do to the queen Vashti according to law, because she has not done the bidding of the king Ahasuerus by the chamberlains?

Basi Memukani akajibu mbele ya mfalme na maakida, Huyu Vashti, malkia, hakumkosa mfalme tu peke yake, ila na maakida wote, na watu wote pia walioko katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero. Esta 1:16

Memucan answered before the king and the princes, Vashti the queen has not done wrong to the king only, but also to all the princes, and to all the peoples who are in all the provinces of the king Ahasuerus.

Kwa maana tendo hilo la malkia litajulikana na wanawake wote, hata waume zao watadharauliwa machoni pao, itakaponenwa ya kuwa mfalme Ahasuero aliamuru Vashti, malkia, aletwe mbele yake, bali hakuja. Esta 1:17

For this deed of the queen will come abroad to all women, to make their husbands contemptible in their eyes, when it shall be reported, The king Ahasuerus commanded Vashti the queen to be brought in before him, but she didn't come.

Hata na leo hivi mabibi wastahiki wa Uajemi na Umedi waliokwisha kuzisikia habari za tendo lake malkia watawaambia vivi hivi maakida wote wa mfalme. Hivyo kutatokea dharau nyingi na ghadhabu tele. Esta 1:18

This day will the princesses of Persia and Media who have heard of the deed of the queen say [the like] to all the king's princes. So [will there arise] much contempt and wrath.

Basi mfalme akiona vema, na itoke kwake amri ya kifalme, nayo iandikwe katika sheria za Waajemi na Wamedi isitanguke, ya kwamba Vashti asifike tena mbele ya mfalme Ahasuero; na umalkia wake mfalme ampe mwingine aliye mwema kuliko yeye. Esta 1:19

If it please the king, let there go forth a royal commandment from him, and let it be written among the laws of the Persians and the Medes, that it not be altered, that Vashti come no more before king Ahasuerus; and let the king give her royal estate to another who is better than she.

Basi mbiu ya mfalme atakayoipiga itakapotangazwa katika ufalme wake wote, nao ni mkubwa, wake wote watawaheshimu waume zao, wakubwa kwa wadogo. Esta 1:20

When the king's decree which he shall make shall be published throughout all his kingdom (for it is great), all the wives will give to their husbands honor, both to great and small.

Basi neno hili likawapendeza mfalme na maakida; naye mfalme akafanya sawasawa na neno lake Memukani. Esta 1:21

The saying pleased the king and the princes; and the king did according to the word of Memucan:

Kwa maana alipeleka nyaraka katika majimbo yote ya mfalme, kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake, ya kwamba kila mwanamume atawale nyumbani mwake, na kuitangaza habari hii kwa lugha ya watu wake. Esta 1:22

for he sent letters into all the king's provinces, into every province according to the writing of it, and to every people after their language, that every man should bear rule in his own house, and should speak according to the language of his people.