1
Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe;
When Jesus had spoken these things, He lifted up His eyes to heaven and said, “Father, the hour has come. Glorify Your Son, that Your Son may glorify You.
2
kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele.
For You granted Him authority over all people, so that He may give eternal life to all those You have given Him.
3
Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.
Now this is eternal life, that they may know You, the only true God, and Jesus Christ, whom You have sent.
4
Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.
I have glorified You on earth by accomplishing the work You gave Me to do.
5
Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.
And now, Father, glorify Me in Your presence with the glory I had with You before the world existed.
6
Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika.
I have revealed Your name to those You have given Me out of the world. They were Yours; You gave them to Me, and they have kept Your word.
7
Sasa wamejua ya kuwa yote uliyonipa yatoka kwako.
Now they know that everything You have given Me comes from You.
8
Kwa kuwa maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua hakika ya kuwa nalitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
For I have given them the words You gave Me, and they have received them. They knew with certainty that I came from You, and they believed that You sent Me.
9
Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako;
I ask on their behalf. I do not ask on behalf of the world, but on behalf of those You have given Me; for they are Yours.
10
na wote walio wangu ni wako, na walio wako ni wangu; nami nimetukuzwa ndani yao.
All I have is Yours, and all You have is Mine; and in them I have been glorified.
11
Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo.
I will no longer be in the world, but they are in the world, and I am coming to You. Holy Father, protect them by Your name, the name You gave Me, so that they may be one as We are one.
12
Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.
While I was with them, I protected and preserved them by Your name, the name You gave Me. Not one of them has been lost, except the son of destruction, so that the Scripture would be fulfilled.
13
Na sasa naja kwako; na maneno haya nayasema ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu imetimizwa ndani yao.
But now I am coming to You; and I am saying these things while I am in the world, so that they may have My joy fulfilled within them.
14
Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.
I have given them Your word and the world has hated them. For they are not of the world, just as I am not of the world.
15
Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu.
I am not asking that You take them out of the world, but that You keep them from the evil one.
16
Wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.
They are not of the world, just as I am not of the world.
17
Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli.
Sanctify them by the truth; Your word is truth.
18
Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami vivyo hivyo naliwatuma hao ulimwenguni.
As You sent Me into the world, I have also sent them into the world.
19
Na kwa ajili yao najiweka wakfu mwenyewe, ili na hao watakaswe katika kweli.
For them I sanctify Myself, so that they too may be sanctified by the truth.
20
Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao.
I am not asking on behalf of them alone, but also on behalf of those who will believe in Me through their message,
21
Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
that all of them may be one, as You, Father, are in Me, and I am in You. May they also be in Us, so that the world may believe that You sent Me.
22
Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.
I have given them the glory You gave Me, so that they may be one as We are one—
23
Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi.
I in them and You in Me—that they may be perfectly united, so that the world may know that You sent Me and have loved them just as You have loved Me.
24
Baba, hao ulionipa nataka wawe pamoja nami po pote nilipo, wapate na kuutazama utukufu wangu ulionipa; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu.
Father, I want those You have given Me to be with Me where I am, that they may see the glory You gave Me because You loved Me before the foundation of the world.
25
Baba mwenye haki, ulimwengu haukukujua; lakini mimi nalikujua, na hao wamejua ya kuwa ndiwe uliyenituma.
Righteous Father, although the world has not known You, I know You, and they know that You sent Me.
26
Nami naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo; ili pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao.
And I have made Your name known to them and will continue to make it known, so that the love You have for Me may be in them, and I in them.”