Sifa Lyrics

Uko Wapi Mungu by William Yilima cover art

William Yilima - Uko Wapi Mungu Lyrics

Artist:
William Yilima
Album:
Uko Wapi Mungu
Official Release:
09 Feb 2016

Lyrics

Verse 1


Uko wapi eh Mungu wangu
Uko wapi njoo uniokoe


Verse 2


Mawimbi yanataka kuniangamiza
Misukosuko yaniandama
Dhoruba na majaribu havikomi kwangu
Uko wapi fanya hima niokoe


Chorus (x2)


Uko wapi eh Bwana
Uko wapi mbona ni kama umeniacha
Usifiche uso wako eh Bwana
Usifiche uso nipone kwa rehema
Mwili huu wa nyama
unachoka pekee yangu sitaweza


Verse 3


Nimegumbikwa wimbi la huzuni na mawazo
Amani kwangu ni kama ndoto
Ole wangu nikifurahi siku moja
Siku sita nitalia wiki ipite
Mangumu yangu nikisimulia kwa ndugu zangu
Waniambia utajijua na Mungu wako
Nikielezea magumu yangu kwa wapendwa
Waniambia tumechoka kukufariji
Wakati mwingine natamani heri nife
Kuliko kuishi ninyanyasike hivi


Verse 4


Uko wapi eh Mungu wa Elijah
Uko wapi eh Mungu wa Ibrahimu
Uko wapi eh Mungu wa isaka
Elshadai fanya hima uniokoe


Outro


Nina neno juu yako eh mpendwa
Usilie kwa mangumu uliyonayo
Usitazame jaribu ulilonalo
Inua macho msalabani umtazame yesu
Japo ndugu wakikutenga na kukuacha
Yesu atakukumbatia majaribu ipo siku yatakoma
Utasahau shida zote ulizopata


Credits & Song Information

Performed By
William Yilima
Community reviewed · Apple Music
Release Date
2016-02-09
Community reviewed · Apple Music

Add song information · Add a supporting source

Video

Meaning & Inspiration

In “Uko Wapi Mungu,” William Yilima voices a prayer from a place of distress, asking why God seems absent and pleading for mercy and rescue. The repeated appeal gives the recording a lament-like focus while keeping hope centered on divine intervention.