William Yalima - Uko Wapi Lyrics

Uko Wapi Lyrics

Uko wapi eh Mungu wangu  
Uko wapi njoo uniokoe

Mawimbi yanataka kuniangamiza 
Misukosuko yaniandama 
Dhoruba na majaribu havikomi kwangu 
Uko wapi fanya hima niokoe 

Uko wapi eh Bwana 
Uko wapi mbona ni kama umeniacha
Usifiche uso wako eh Bwana 
Usifiche uso nipone kwa rehema 
Mwili huu wa nyama 
unachoka pekee yangu sitaweza

Nimegumbikwa wimbi la huzuni na mawazo 
Amani kwangu ni kama ndoto 
Ole wangu nikifurahi siku moja 
Siku sita nitalia wiki ipite 
Mangumu yangu nikisimulia kwa ndugu zangu 
Waniambia utajijua na Mungu wako 
Nikielezea magumu yangu kwa wapendwa 
Waniambia tumechoka kukufariji 
Wakati mwingine natamani heri nife
Kuliko kuishi ninyanyasike hivi 

Uko wapi eh Mungu wa Elijah 
Uko wapi eh Mungu wa Ibrahimu 
Uko wapi eh Mungu wa isaka 
Elshadai fanya hima uniokoe 
Uko wapi eh Bwana  
Uko wapi mbona ni kama umeniacha 
Usifiche uso wako eh Bwana 
Usifiche uso nipone kwa rehema 
Mwili huu wa nyama 
Unachoka pekee yangu sitaweza

Nina neno juu yako eh mpendwa 
Usilie kwa mangumu uliyonayo 
Usitazame jaribu ulilonalo 
Inua macho msalabani umtazame yesu 
Japo ndugu wakikutenga na kukuacha 
Yesu atakukumbatia majaribu ipo siku yatakoma 
Utasahau shida zote ulizopata 


Uko Wapi Video

William Yalima Songs

Related Songs