Sifa Lyrics

Napenda Niwe Na Wewe by Emmanuel Mgogo cover art

Emmanuel Mgogo - Napenda Niwe Na Wewe Lyrics

Artist:
Emmanuel Mgogo

Lyrics

Mimi napenda niwe karibu nawewe 


Niwe na wewe 


Univute niwe karibu na wewe Bwana 


Mimi napendanga 


Mimi napenda niwe karibu nawewe 


Niwe na wewe 


Univute niwe karibu na wewe Bwana 


Mimi napendanga 


Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 


Kuwa karibu nawewe ninapendanga 


Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 


Kuwa karibu nawewe ninapendanga 


Nina haja nawewe Bwana 


Ninatamani ukae nami 


Sioni mwingine Bwana 


Sijapata mwingine ila niwewe 


wakunifaa mimi wakunitunza ila niwewe 


Tabibu wa karibu Bwana 


Usinipite pembeni Bwana 


Sina mwingine wa kunihurumia 


Pale ninapojongiwa na wanyan'ganyi 


Uwe karibu, Wewe ni msamaria mwema utanihudumia 


Utanifunga majeraha na kunifariji 


Unionyeshe pendo lako maana wanipenda 


Unionyeshe pendo lako maana wanipenda 


Sioni la kunifurahisha nikiwa mbali nawe Bwana 


Kama mtu naelewa udongoni nitasinya na kudhoofika 


Ninaomba univute niwe karibu nawe 


Kama mti uliopandwa kando kando ya maji 


Uzao matunda mazuri wala majani yake hayanyauki 


Kila nitendalo lifanikiwe Bwana naomba 


Wewe ni maji ya uzima 


Wewe ni maji yaliyo hai 


Kisima cha uzima na upendo 


Kama ayala wa porini ayatamanivyo maji 


Ndivyo nafsi yangu yakutamani wewe 


Fanya hima usichelewe 


Univute karibu nawe niwe nawewe 


Napendaaaa 


Mimi napenda niwe karibu nawewe 


Niwe na wewe 


Univute niwe karibu na wewe Bwana 


Mimi napendanga 


Mimi napenda niwe karibu nawewe 


Niwe na wewe 


Univute niwe karibu na wewe Bwana 


Mimi napendanga 


Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 


Kuwa karibu nawewe ninapendanga 


Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 


Kuwa karibu nawewe ninapendanga 


Kukaa nawewe ni shauku pekee la moyo wangu Bwana 


Hapa nilipo sijaridhika natamani nipandishwe juu 


Univute karibu nawe 


Karibu zaidi ya jana 


Uwe nuru niangazie lengo lako kama maji 


Nizame kwenye kizima cha uwepo wako 


Nimesoma katika neno lako zaburi umesema 


Aketiye mahali pake pa siri pa aliye juu 


Atakaa katika uvuli wake mwenye enzi 


Ataokolewa na mitego ya adui 


Silaha zote na mishale haitofanikiwa 


Silaha zote na mishale haitofanikiwa 


Nichukue uniweke hapo Bwana 


Hili ni ombi la moyo wangu 


Niketishe kwenye uwepo wako 


Utuketishe kwenye uwepo wako 


Usiniache gizani Bwana 


pekee yangu siwezi 


Kaa nami karibu nami 


Ndani yangu nami ndani yako 


Univute karibu nawe 


mikononi mwako niwe salama 


Univute karibu nawe 


Niwe nawewe Bwana 


Mimi napenda niwe karibu nawewe 


Niwe na wewe 


Univute niwe karibu na wewe Bwana 


Mimi napendanga 


Mimi napenda niwe karibu nawewe 


Niwe na wewe 


Univute niwe karibu na wewe Bwana 


Mimi napendanga 


Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 


Kuwa karibu nawewe ninapendanga 


Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 


Kuwa karibu nawewe ninapendanga 


Video