Emmanuel Mgogo - Napenda Niwe Na Wewe Lyrics

Napenda Niwe Na Wewe Lyrics

Mimi napenda niwe karibu nawewe 
Niwe na wewe 
Univute niwe karibu na wewe Bwana 
Mimi napendanga 

Mimi napenda niwe karibu nawewe 
Niwe na wewe 
Univute niwe karibu na wewe Bwana 
Mimi napendanga 

Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 
Kuwa karibu nawewe ninapendanga 
Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 
Kuwa karibu nawewe ninapendanga 

Nina haja nawewe Bwana 
Ninatamani ukae nami 
Sioni mwingine Bwana 
Sijapata mwingine ila niwewe 
wakunifaa mimi wakunitunza ila niwewe 
Tabibu wa karibu Bwana 
Usinipite pembeni Bwana 
Sina mwingine wa kunihurumia 
Pale ninapojongiwa na wanyan'ganyi 
Uwe karibu, Wewe ni msamaria mwema utanihudumia 
Utanifunga majeraha na kunifariji 
Unionyeshe pendo lako maana wanipenda 
Unionyeshe pendo lako maana wanipenda 
Sioni la kunifurahisha nikiwa mbali nawe Bwana 
Kama mtu naelewa udongoni nitasinya na kudhoofika 
Ninaomba univute niwe karibu nawe 
Kama mti uliopandwa kando kando ya maji 
Uzao matunda mazuri wala majani yake hayanyauki 
Kila nitendalo lifanikiwe Bwana naomba 

Wewe ni maji ya uzima 
Wewe ni maji yaliyo hai 
Kisima cha uzima na upendo 
Kama ayala wa porini ayatamanivyo maji 
Ndivyo nafsi yangu yakutamani wewe 
Fanya hima usichelewe 
Univute karibu nawe niwe nawewe 
Napendaaaa 

Mimi napenda niwe karibu nawewe 
Niwe na wewe 
Univute niwe karibu na wewe Bwana 
Mimi napendanga 

Mimi napenda niwe karibu nawewe 
Niwe na wewe 
Univute niwe karibu na wewe Bwana 
Mimi napendanga 

Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 
Kuwa karibu nawewe ninapendanga 
Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 
Kuwa karibu nawewe ninapendanga 

Kukaa nawewe ni shauku pekee la moyo wangu Bwana 
Hapa nilipo sijaridhika natamani nipandishwe juu 
Univute karibu nawe 
Karibu zaidi ya jana 
Uwe nuru niangazie lengo lako kama maji 
Nizame kwenye kizima cha uwepo wako 
Nimesoma katika neno lako zaburi umesema 
Aketiye mahali pake pa siri pa aliye juu 
Atakaa katika uvuli wake mwenye enzi 
Ataokolewa na mitego ya adui 
Silaha zote na mishale haitofanikiwa 
Silaha zote na mishale haitofanikiwa 
Nichukue uniweke hapo Bwana 
Hili ni ombi la moyo wangu 
Niketishe kwenye uwepo wako 
Utuketishe kwenye uwepo wako 
Usiniache gizani Bwana 
pekee yangu siwezi 

Kaa nami karibu nami 
Ndani yangu nami ndani yako 
Univute karibu nawe 
mikononi mwako niwe salama 
Univute karibu nawe 
Niwe nawewe Bwana 

Mimi napenda niwe karibu nawewe 
Niwe na wewe 
Univute niwe karibu na wewe Bwana 
Mimi napendanga 

Mimi napenda niwe karibu nawewe 
Niwe na wewe 
Univute niwe karibu na wewe Bwana 
Mimi napendanga 

Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 
Kuwa karibu nawewe ninapendanga 
Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 
Kuwa karibu nawewe ninapendanga 


Napenda Niwe Na Wewe Video

Napenda Niwe Na Wewe Lyrics -  Emmanuel Mgogo

Emmanuel Mgogo Songs

Related Songs