Sifa Lyrics

Watangoja Sana by Annastacia Mukabwa cover art

Annastacia Mukabwa - Watangoja Sana Lyrics

Artist:
Annastacia Mukabwa
Album:
Watangoja Sana - Single
Official Release:
01 Jan 2018

Lyrics

watangoja sana 


Wanaongoja kuanguka kwako 


Wanaongoja kushindwa kwako 


Wanaongoja umuache Yesu 


Wanaongoja uharibikiwe wacheke 


Waambie pole, pole pole 


Ninaye Yesu, ninaye mwokozi 


Waambie pole, pole pole 


Watangoja sana 


Yesu alipokufa akazikwa kaburini 


Wengi walicheka sana Wengine walisema 


“Si unajifanya ni mwana wa Mungu” 


“Hebu jifufue tukuone” 


Waliweka na walinzi walinde kaburi 


Ili Yesu asifufuke 


Waliweka na jiwe kubwa, pale kaburini 


Ili Yesu asifufuke, Siku ya tatu ilipofika 


Walinzi walishangaa, Yesu hayupo kaburini 


Siku ya tatu ilipofika, Walinzi walishangaa 


Yesu hayupo kaburini, amefufuka 


watangoja sana 


Wanaongoja matanga yako,


Wanaongoja urudiwe kwenyu nani wateleza 


Wanaongoja ufutwe kazi wacheke 


Waambie, pole, pole, pole 


Ninaye yesu sibabaiki mimi nalindwa na Jehova 


Ananipigia vita, Watangoja sana


Eh ni Mungu pekee yake


Analalamishwa juu yako 


Hakuna silaha itainuka 


Kinyume chako ifanikiwe


Maneno ya watu yasikuvunje moyo 


Tegemea we utashinda, utashinda 


watangoja sana 


Wanaongoja kuanguka kwako 


Wanaotaka ndoa yako ivunjike wacheke 


Wanaotamani ufilisike wacheke 


Wanaosema utakufa bila kuzaa mama 


Waambie pole, pole, pole 


Ninalindwa na jeshi la mbinguni 


Wambie, pole, pole, pole 


Watangoja sana 


watangoja sana, Wanasema hutaolewa 


Wanasema utashindwa na elimu 


Wanaofitini ushukishwe cheo 


Wanaosema huwezi fika popote 


Waambie pole, pole pole 


Wanaotabiri, wanaokuwazia 


Watangoja sana 


Ninaye Yesu, nasonga mbele 


Nyuma sirudi tena 


Watangoja sana 


BweniEve Productions


Video