Waefeso 5 Swahili & English

Listen/Download Audio
Waefeso 5 (Swahili) Ephesians 5 (English)

Hivyo mfuateni Mungu, kama watoto wanaopendwa; Waefeso 5:1

Be therefore imitators of God, as beloved children.

mkaenende katika upendo, kama Kristo naye alivyowapenda ninyi tena akajitoa kwa ajili yetu, sadaka na dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukato. Waefeso 5:2

Walk in love, even as Christ also loved you, and gave himself up for us, an offering and a sacrifice to God for a sweet-smelling fragrance.

Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu; Waefeso 5:3

But sexual immorality, and all uncleanness, or covetousness, let it not even be mentioned among you, as becomes saints;

wala aibu wala maneno ya upuzi wala ubishi; hayo hayapendezi; bali afadhali kushukuru. Waefeso 5:4

nor filthiness, nor foolish talking, nor jesting, which are not appropriate; but rather giving of thanks.

Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu. Waefeso 5:5

Know this for sure, that no sexually immoral person, nor unclean person, nor covetous man, who is an idolater, has any inheritance in the Kingdom of Christ and God.

Mtu asiwadanganye kwa maneno yasiyo na maana; kwa kuwa kwa sababu ya hayo hasira ya Mungu huwajia wana wa uasi. Waefeso 5:6

Let no one deceive you with empty words. For because of these things, the wrath of God comes on the children of disobedience.

Basi msishirikiane nao. Waefeso 5:7

Therefore don't be partakers with them.

Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika Bwana; enendeni kama watoto wa nuru, Waefeso 5:8

For you were once darkness, but are now light in the Lord. Walk as children of light,

kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli; Waefeso 5:9

for the fruit of the Spirit is in all goodness and righteousness and truth,

mkihakiki ni nini impendezayo Bwana. Waefeso 5:10

proving what is well-pleasing to the Lord.

Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee; Waefeso 5:11

Have no fellowship with the unfruitful works of darkness, but rather even reprove them.

kwa kuwa yanayotendeka kwao kwa siri, ni aibu hata kuyanena. Waefeso 5:12

For the things which are done by them in secret, it is a shame even to speak of.

Lakini yote yaliyokemewa hudhihirishwa na nuru maana kila kilichodhihirika ni nuru. Waefeso 5:13

But all things, when they are reproved, are revealed by the light, for everything that is revealed is light.

Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza. Waefeso 5:14

Therefore he says, "Awake, you who sleep, and arise from the dead, and Christ will shine on you."

Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; Waefeso 5:15

Therefore watch carefully how you walk, not as unwise, but as wise;

mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu. Waefeso 5:16

redeeming the time, because the days are evil.

Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana. Waefeso 5:17

Therefore don't be foolish, but understand what the will of the Lord is.

Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho; Waefeso 5:18

Don't be drunken with wine, in which is dissipation, but be filled with the Spirit,

mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu; Waefeso 5:19

speaking to one another in psalms, hymns, and spiritual songs; singing, and singing praises in your heart to the Lord;

na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo; Waefeso 5:20

giving thanks always concerning all things in the name of our Lord Jesus Christ, to God, even the Father;

hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo. Waefeso 5:21

subjecting yourselves one to another in the fear of Christ.

Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. Waefeso 5:22

Wives, be subject to your own husbands, as to the Lord.

Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. Waefeso 5:23

For the husband is the head of the wife, and Christ also is the head of the assembly, being himself the savior of the body.

Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. Waefeso 5:24

But as the assembly is subject to Christ, so let the wives also be to their own husbands in everything.

Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; Waefeso 5:25

Husbands, love your wives, even as Christ also loved the assembly, and gave himself up for it;

ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; Waefeso 5:26

that he might sanctify it, having cleansed it by the washing of water with the word,

apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa. Waefeso 5:27

that he might present the assembly to himself gloriously, not having spot or wrinkle or any such thing; but that it should be holy and without blemish.

Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. Waefeso 5:28

Even so ought husbands also to love their own wives as their own bodies. He who loves his own wife loves himself.

Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa. Waefeso 5:29

For no man ever hated his own flesh; but nourishes and cherishes it, even as the Lord also does the assembly;

Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. Waefeso 5:30

because we are members of his body, of his flesh and bones.

Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. Waefeso 5:31

"For this cause a man will leave his father and mother, and will be joined to his wife. The two will become one flesh."

Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. Waefeso 5:32

This mystery is great, but I speak concerning Christ and of the assembly.

Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe. Waefeso 5:33

Nevertheless each of you must also love his own wife even as himself; and let the wife see that she respects her husband.