Waefeso 5 Swahili & English
Listen/Download AudioWaefeso 5 (Swahili) | Ephesians 5 (English) |
---|---|
Hivyo mfuateni Mungu, kama watoto wanaopendwa; Waefeso 5:1 |
Be therefore imitators of God, as beloved children. |
mkaenende katika upendo, kama Kristo naye alivyowapenda ninyi tena akajitoa kwa ajili yetu, sadaka na dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukato. Waefeso 5:2 |
Walk in love, even as Christ also loved you, and gave himself up for us, an offering and a sacrifice to God for a sweet-smelling fragrance. |
Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu; Waefeso 5:3 |
But sexual immorality, and all uncleanness, or covetousness, let it not even be mentioned among you, as becomes saints; |
wala aibu wala maneno ya upuzi wala ubishi; hayo hayapendezi; bali afadhali kushukuru. Waefeso 5:4 |
nor filthiness, nor foolish talking, nor jesting, which are not appropriate; but rather giving of thanks. |
Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu. Waefeso 5:5 |
Know this for sure, that no sexually immoral person, nor unclean person, nor covetous man, who is an idolater, has any inheritance in the Kingdom of Christ and God. |
Mtu asiwadanganye kwa maneno yasiyo na maana; kwa kuwa kwa sababu ya hayo hasira ya Mungu huwajia wana wa uasi. Waefeso 5:6 |
Let no one deceive you with empty words. For because of these things, the wrath of God comes on the children of disobedience. |
Basi msishirikiane nao. Waefeso 5:7 |
Therefore don't be partakers with them. |
Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika Bwana; enendeni kama watoto wa nuru, Waefeso 5:8 |
For you were once darkness, but are now light in the Lord. Walk as children of light, |
kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli; Waefeso 5:9 |
for the fruit of the Spirit is in all goodness and righteousness and truth, |
mkihakiki ni nini impendezayo Bwana. Waefeso 5:10 |
proving what is well-pleasing to the Lord. |
Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee; Waefeso 5:11 |
Have no fellowship with the unfruitful works of darkness, but rather even reprove them. |
kwa kuwa yanayotendeka kwao kwa siri, ni aibu hata kuyanena. Waefeso 5:12 |
For the things which are done by them in secret, it is a shame even to speak of. |
Lakini yote yaliyokemewa hudhihirishwa na nuru maana kila kilichodhihirika ni nuru. Waefeso 5:13 |
But all things, when they are reproved, are revealed by the light, for everything that is revealed is light. |
Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza. Waefeso 5:14 |
Therefore he says, "Awake, you who sleep, and arise from the dead, and Christ will shine on you." |
Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; Waefeso 5:15 |
Therefore watch carefully how you walk, not as unwise, but as wise; |
mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu. Waefeso 5:16 |
redeeming the time, because the days are evil. |
Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana. Waefeso 5:17 |
Therefore don't be foolish, but understand what the will of the Lord is. |
Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho; Waefeso 5:18 |
Don't be drunken with wine, in which is dissipation, but be filled with the Spirit, |
mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu; Waefeso 5:19 |
speaking to one another in psalms, hymns, and spiritual songs; singing, and singing praises in your heart to the Lord; |
na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo; Waefeso 5:20 |
giving thanks always concerning all things in the name of our Lord Jesus Christ, to God, even the Father; |
hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo. Waefeso 5:21 |
subjecting yourselves one to another in the fear of Christ. |
Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. Waefeso 5:22 |
Wives, be subject to your own husbands, as to the Lord. |
Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. Waefeso 5:23 |
For the husband is the head of the wife, and Christ also is the head of the assembly, being himself the savior of the body. |
Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. Waefeso 5:24 |
But as the assembly is subject to Christ, so let the wives also be to their own husbands in everything. |
Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; Waefeso 5:25 |
Husbands, love your wives, even as Christ also loved the assembly, and gave himself up for it; |
ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; Waefeso 5:26 |
that he might sanctify it, having cleansed it by the washing of water with the word, |
apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa. Waefeso 5:27 |
that he might present the assembly to himself gloriously, not having spot or wrinkle or any such thing; but that it should be holy and without blemish. |
Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. Waefeso 5:28 |
Even so ought husbands also to love their own wives as their own bodies. He who loves his own wife loves himself. |
Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa. Waefeso 5:29 |
For no man ever hated his own flesh; but nourishes and cherishes it, even as the Lord also does the assembly; |
Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. Waefeso 5:30 |
because we are members of his body, of his flesh and bones. |
Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. Waefeso 5:31 |
"For this cause a man will leave his father and mother, and will be joined to his wife. The two will become one flesh." |
Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. Waefeso 5:32 |
This mystery is great, but I speak concerning Christ and of the assembly. |
Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe. Waefeso 5:33 |
Nevertheless each of you must also love his own wife even as himself; and let the wife see that she respects her husband. |