Waefeso 4 Swahili & English

Listen/Download Audio
Waefeso 4 (Swahili) Ephesians 4 (English)

Kwa hiyo nawasihi, mimi niliye mfungwa katika Bwana, mwenende kama inavyoustahili wito wenu mlioitiwa; Waefeso 4:1

I therefore, the prisoner in the Lord, beg you to walk worthily of the calling with which you were called,

kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo; Waefeso 4:2

with all lowliness and humility, with patience, bearing with one another in love;

na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani. Waefeso 4:3

being eager to keep the unity of the Spirit in the bond of peace.

Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu. Waefeso 4:4

There is one body, and one Spirit, even as you also were called in one hope of your calling;

Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. Waefeso 4:5

one Lord, one faith, one baptism,

Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote. Waefeso 4:6

one God and Father of all, who is over all, and through all, and in us all.

Lakini kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo. Waefeso 4:7

But to each one of us was the grace given according to the measure of the gift of Christ.

Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa. Waefeso 4:8

Therefore he says, "When he ascended on high, he led captivity captive, and gave gifts to men."

Basi neno hilo, Alipaa, maana yake nini kama siyo kusema kwamba yeye naye alishuka mpaka pande zilizo chini za nchi? Waefeso 4:9

Now this, "He ascended," what is it but that he also first descended into the lower parts of the earth?

Naye aliyeshuka ndiye yeye aliyepaa juu sana kupita mbingu zote, ili avijaze vitu vyote. Waefeso 4:10

He who descended is the one who also ascended far above all the heavens, that he might fill all things.

Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; Waefeso 4:11

He gave some to be apostles; and some, prophets; and some, evangelists; and some, shepherds{The word for "shepherds" (poimenas) can also be correctly translated "pastors."} and teachers;

kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; Waefeso 4:12

for the perfecting of the saints, to the work of serving, to the building up of the body of Christ;

hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo; Waefeso 4:13

until we all attain to the unity of the faith, and of the knowledge of the Son of God, to a full grown man, to the measure of the stature of the fullness of Christ;

ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu. Waefeso 4:14

that we may no longer be children, tossed back and forth and carried about with every wind of doctrine, by the trickery of men, in craftiness, after the wiles of error;

Lakini tuishike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, Kristo. Waefeso 4:15

but speaking truth in love, we may grow up in all things into him, who is the head, Christ;

Katika yeye mwili wote ukiungamanishwa na kushikanishwa kwa msaada wa kila kiungo, kwa kadiri ya utendaji wa kila sehemu moja moja, huukuza mwili upate kujijenga wenyewe katika upendo. Waefeso 4:16

from whom all the body, being fitted and knit together through that which every joint supplies, according to the working in measure of each individual part, makes the body increase to the building up of itself in love.

Basi nasema neno hili, tena nashuhudia katika Bwana, tangu sasa msienende kama Mataifa waenendavyo, katika ubatili wa nia zao; Waefeso 4:17

This I say therefore, and testify in the Lord, that you no longer walk as the rest of the Gentiles also walk, in the futility of their mind,

ambao; akili zao zimetiwa giza, nao wamefarikishwa na uzima wa Mungu, kwa sababu ya ujinga uliomo ndani yao, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao; Waefeso 4:18

being darkened in their understanding, alienated from the life of God, because of the ignorance that is in them, because of the hardening of their hearts;

ambao wakiisha kufa ganzi wanajitia katika mambo ya ufisadi wapate kufanyiza kila namna ya uchafu kwa kutamani. Waefeso 4:19

who having become callous gave themselves up to lust, to work all uncleanness with greediness.

Bali ninyi, sivyo mlivyojifunza Kristo; Waefeso 4:20

But you did not learn Christ that way;

ikiwa mlimsikia mkafundishwa katika yeye, kama kweli ilivyo katika Yesu, Waefeso 4:21

if indeed you heard him, and were taught in him, even as truth is in Jesus:

mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya; Waefeso 4:22

that you put away, as concerning your former way of life, the old man, that grows corrupt after the lusts of deceit;

na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu; Waefeso 4:23

and that you be renewed in the spirit of your mind,

mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli. Waefeso 4:24

and put on the new man, who in the likeness of God has been created in righteousness and holiness of truth.

Basi uvueni uongo, mkaseme kweli kila mtu na jirani yake; kwa maana tu viungo, kila mmoja kiungo cha wenzake. Waefeso 4:25

Therefore, putting away falsehood, speak truth each one with his neighbor. For we are members one of another.

Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; Waefeso 4:26

"Be angry, and don't sin." Don't let the sun go down on your wrath,

wala msimpe Ibilisi nafasi. Waefeso 4:27

neither give place to the devil.

Mwibaji asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akitenda kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe, apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji. Waefeso 4:28

Let him who stole steal no more; but rather let him labor, working with his hands the thing that is good, that he may have something to give to him who has need.

Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia. Waefeso 4:29

Let no corrupt speech proceed out of your mouth, but such as is good for building up as the need may be, that it may give grace to those who hear.

Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi. Waefeso 4:30

Don't grieve the Holy Spirit of God, in whom you were sealed for the day of redemption.

Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya; Waefeso 4:31

Let all bitterness, wrath, anger, outcry, and slander, be put away from you, with all malice.

tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi. Waefeso 4:32

And be kind to one another, tenderhearted, forgiving each other, just as God also in Christ forgave you.