Amosi 2 Swahili & English
Listen/Download AudioAmosi 2 (Swahili) | Amos 2 (English) |
---|---|
Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Moabu, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu aliichoma moto mifupa ya mfalme wa Edomu hata ikawa chokaa; Amosi 2:1 |
Thus says Yahweh: "For three transgressions of Moab, yes, for four, I will not turn away its punishment; Because he burned the bones of the king of Edom into lime; |
lakini nitapeleka moto juu ya Moabu, nao utayateketeza majumba ya Keriothi; na Moabu atakufa pamoja na mshindo, na kelele, na sauti ya tarumbeta; Amosi 2:2 |
But I will send a fire on Moab, And it will devour the palaces of Kerioth; And Moab will die with tumult, with shouting, and with the sound of the trumpet; |
nami nitamkatilia mbali mwamuzi atoke kati yake, nami nitawaua wakuu wake pamoja naye, asema Bwana. Amosi 2:3 |
And I will cut off the judge from their midst, And will kill all its princes with him," says Yahweh. |
Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Yuda, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wameikataa sheria ya Bwana; wala hawakuzishika amri zake; na maneno yao ya uongo yamewakosesha, ambayo baba zao waliyafuata; Amosi 2:4 |
Thus says Yahweh: "For three transgressions of Judah, yes, for four, I will not turn away its punishment; Because they have rejected Yahweh's law, And have not kept his statutes, And their lies have led them astray, After which their fathers walked; |
lakini nitapeleka moto juu ya Yuda, nao utayateketeza majumba ya Yerusalemu. Amosi 2:5 |
But I will send a fire on Judah, And it will devour the palaces of Jerusalem." |
Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Israeli, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wamewauza wenye haki kwa fedha, na maskini kwa jozi ya viatu; Amosi 2:6 |
Thus says Yahweh: "For three transgressions of Israel, yes, for four, I will not turn away its punishment; Because they have sold the righteous for silver, And the needy for a pair of shoes; |
nao hutwetea mavumbi yaliyo juu ya vichwa vya maskini, na kuipotosha njia ya mwenye upole; na mtu na baba yake humwendea mwanamke mmoja, hata kulitia unajisi jina langu takatifu; Amosi 2:7 |
They trample on the dust of the earth on the head of the poor, And deny justice to the oppressed; And a man and his father use the same maiden, to profane my holy name; |
nao hujilaza karibu na kila madhabahu juu ya nguo zilizowekwa rehani, na katika nyumba ya Mungu wao hunywa divai ya watu waliotozwa fedha. Amosi 2:8 |
And they lay themselves down beside every altar on clothes taken in pledge; And in the house of their God they drink the wine of those who have been fined. |
Lakini nalimwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi, tena alikuwa na nguvu kama mialoni; lakini naliyaangamiza matunda yake toka juu, na mizizi yake toka chini. Amosi 2:9 |
Yet I destroyed the Amorite before them, Whose height was like the height of the cedars, And he was strong as the oaks; Yet I destroyed his fruit from above, and his roots from beneath. |
Pia naliwapandisha ninyi kutoka nchi ya Misri, nikawaongoza muda wa miaka arobaini jangwani, ili mpate kuimiliki nchi ya Mwamori. Amosi 2:10 |
Also I brought you up out of the land of Egypt, And led you forty years in the wilderness, To possess the land of the Amorite. |
Nami nikawainua watu miongoni mwa wana wenu wawe manabii, na katika vijana wenu wawe Wanadhiri; je! Sivyo hivyo, enyi wana wa Israeli? Asema Bwana. Amosi 2:11 |
I raised up some of your sons for prophets, And some of your young men for Nazirites. Isn't this true, You children of Israel?" says Yahweh. |
Lakini mliwapa Wanadhiri mvinyo wanywe; mkawaamuru manabii, mkisema, Msifanye unabii. Amosi 2:12 |
"But you gave the Nazirites wine to drink, And commanded the prophets, saying, 'Don't prophesy!' |
Tazameni, nitawalemea ninyi, Kama gari lilemeavyo lililojaa miganda. Amosi 2:13 |
Behold, I will crush you in your place, As a cart crushes that is full of grain. |
Naye apigaye mbio atapotewa na kimbilio; Wala aliye hodari hataongeza nguvu zake; Wala shujaa hatajiokoa nafsi yake; Amosi 2:14 |
Flight will perish from the swift; And the strong won't strengthen his force; Neither shall the mighty deliver himself; |
Wala apindaye upinde hatasimama; Wala aliye mwepesi wa miguu hataokoka; Wala apandaye farasi hatajiokoa nafsi yake; Amosi 2:15 |
Neither shall he stand who handles the bow; And he who is swift of foot won't escape; Neither shall he who rides the horse deliver himself; |
Naye mwenye moyo mkuu miongoni mwa mashujaa Atakimbia uchi siku ile, asema Bwana. Amosi 2:16 |
And he who is courageous among the mighty will flee away naked in that day," says Yahweh. |