Amosi 2 Swahili & English

Listen/Download Audio
Amosi 2 (Swahili) Amos 2 (English)

Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Moabu, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu aliichoma moto mifupa ya mfalme wa Edomu hata ikawa chokaa; Amosi 2:1

Thus says Yahweh: "For three transgressions of Moab, yes, for four, I will not turn away its punishment; Because he burned the bones of the king of Edom into lime;

lakini nitapeleka moto juu ya Moabu, nao utayateketeza majumba ya Keriothi; na Moabu atakufa pamoja na mshindo, na kelele, na sauti ya tarumbeta; Amosi 2:2

But I will send a fire on Moab, And it will devour the palaces of Kerioth; And Moab will die with tumult, with shouting, and with the sound of the trumpet;

nami nitamkatilia mbali mwamuzi atoke kati yake, nami nitawaua wakuu wake pamoja naye, asema Bwana. Amosi 2:3

And I will cut off the judge from their midst, And will kill all its princes with him," says Yahweh.

Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Yuda, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wameikataa sheria ya Bwana; wala hawakuzishika amri zake; na maneno yao ya uongo yamewakosesha, ambayo baba zao waliyafuata; Amosi 2:4

Thus says Yahweh: "For three transgressions of Judah, yes, for four, I will not turn away its punishment; Because they have rejected Yahweh's law, And have not kept his statutes, And their lies have led them astray, After which their fathers walked;

lakini nitapeleka moto juu ya Yuda, nao utayateketeza majumba ya Yerusalemu. Amosi 2:5

But I will send a fire on Judah, And it will devour the palaces of Jerusalem."

Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Israeli, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wamewauza wenye haki kwa fedha, na maskini kwa jozi ya viatu; Amosi 2:6

Thus says Yahweh: "For three transgressions of Israel, yes, for four, I will not turn away its punishment; Because they have sold the righteous for silver, And the needy for a pair of shoes;

nao hutwetea mavumbi yaliyo juu ya vichwa vya maskini, na kuipotosha njia ya mwenye upole; na mtu na baba yake humwendea mwanamke mmoja, hata kulitia unajisi jina langu takatifu; Amosi 2:7

They trample on the dust of the earth on the head of the poor, And deny justice to the oppressed; And a man and his father use the same maiden, to profane my holy name;

nao hujilaza karibu na kila madhabahu juu ya nguo zilizowekwa rehani, na katika nyumba ya Mungu wao hunywa divai ya watu waliotozwa fedha. Amosi 2:8

And they lay themselves down beside every altar on clothes taken in pledge; And in the house of their God they drink the wine of those who have been fined.

Lakini nalimwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi, tena alikuwa na nguvu kama mialoni; lakini naliyaangamiza matunda yake toka juu, na mizizi yake toka chini. Amosi 2:9

Yet I destroyed the Amorite before them, Whose height was like the height of the cedars, And he was strong as the oaks; Yet I destroyed his fruit from above, and his roots from beneath.

Pia naliwapandisha ninyi kutoka nchi ya Misri, nikawaongoza muda wa miaka arobaini jangwani, ili mpate kuimiliki nchi ya Mwamori. Amosi 2:10

Also I brought you up out of the land of Egypt, And led you forty years in the wilderness, To possess the land of the Amorite.

Nami nikawainua watu miongoni mwa wana wenu wawe manabii, na katika vijana wenu wawe Wanadhiri; je! Sivyo hivyo, enyi wana wa Israeli? Asema Bwana. Amosi 2:11

I raised up some of your sons for prophets, And some of your young men for Nazirites. Isn't this true, You children of Israel?" says Yahweh.

Lakini mliwapa Wanadhiri mvinyo wanywe; mkawaamuru manabii, mkisema, Msifanye unabii. Amosi 2:12

"But you gave the Nazirites wine to drink, And commanded the prophets, saying, 'Don't prophesy!'

Tazameni, nitawalemea ninyi, Kama gari lilemeavyo lililojaa miganda. Amosi 2:13

Behold, I will crush you in your place, As a cart crushes that is full of grain.

Naye apigaye mbio atapotewa na kimbilio; Wala aliye hodari hataongeza nguvu zake; Wala shujaa hatajiokoa nafsi yake; Amosi 2:14

Flight will perish from the swift; And the strong won't strengthen his force; Neither shall the mighty deliver himself;

Wala apindaye upinde hatasimama; Wala aliye mwepesi wa miguu hataokoka; Wala apandaye farasi hatajiokoa nafsi yake; Amosi 2:15

Neither shall he stand who handles the bow; And he who is swift of foot won't escape; Neither shall he who rides the horse deliver himself;

Naye mwenye moyo mkuu miongoni mwa mashujaa Atakimbia uchi siku ile, asema Bwana. Amosi 2:16

And he who is courageous among the mighty will flee away naked in that day," says Yahweh.