2 Wakorintho 8 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Wakorintho 8 (Swahili) 2nd Corinthians 8 (English)

Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia; 2 Wakorintho 8:1

Moreover, brothers, we make known to you the grace of God which has been given in the assemblies of Macedonia;

maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na umaskini wao uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao. 2 Wakorintho 8:2

how that in much proof of affliction the abundance of their joy and their deep poverty abounded to the riches of their liberality.

Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao; 2 Wakorintho 8:3

For according to their power, I testify, yes and beyond their power, they gave of their own accord,

wakituomba sana pamoja na kutusihi kwa habari ya neema hii, na shirika hili la kuwahudumia watakatifu. 2 Wakorintho 8:4

begging us with much entreaty to receive this grace and the fellowship in the service to the saints.

Tena walitenda hivi si kama tulivyotumaini tu, bali kwanza walijitoa nafsi zao kwa Bwana; na kwetu pia, kwa mapenzi ya Mungu. 2 Wakorintho 8:5

This was not as we had hoped, but first they gave their own selves to the Lord, and to us through the will of God.

Hata tukamwonya Tito kuwatimilizia neema hii kwenu kama vile yeye alivyotangulia kuianzisha. 2 Wakorintho 8:6

So we urged Titus, that as he made a beginning before, so he would also complete in you this grace.

Lakini kama mlivyo na wingi wa mambo yote; imani, na usemi, na elimu, na bidii yote, na upendo wenu kwetu sisi; basi vivyo hivyo mpate wingi wa neema hii pia. 2 Wakorintho 8:7

But as you abound in everything, in faith, utterance, knowledge, all earnestness, and in your love to us, see that you also abound in this grace.

Sineni ili kuwaamuru, bali kwa bidii ya watu wengine nijaribu unyofu wa upendo wenu. 2 Wakorintho 8:8

I speak not by way of commandment, but as proving through the earnestness of others the sincerity also of your love.

Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake. 2 Wakorintho 8:9

For you know the grace of our Lord Jesus Christ, that, though he was rich, yet for your sakes he became poor, that you through his poverty might become rich.

Nami katika neno hili natoa shauri langu; maana neno hili lawafaa ninyi mliotangulia, yapata mwaka, licha ya kutenda hata na kutaka pia. 2 Wakorintho 8:10

I give a judgment in this: for this is expedient for you, who were the first to start a year ago, not only to do, but also to be willing.

Lakini sasa timizeni kule kutenda nako, ili kama vile mlivyokuwa tayari kutaka, vivyo hivyo mkawe tayari na kutimiza, kwa kadiri ya mlivyo navyo. 2 Wakorintho 8:11

But now complete the doing also, that as there was the readiness to be willing, so there may be the completion also out of your ability.

Maana, kama nia ipo, hukubaliwa kwa kadiri ya alivyo navyo mtu, si kwa kadiri ya asivyo navyo. 2 Wakorintho 8:12

For if the readiness is there, it is acceptable according to what you have, not according to what you don't have.

Maana sisemi hayo, ili wengine wapate raha nanyi mpate dhiki; 2 Wakorintho 8:13

For this is not that others may be eased and you distressed,

bali mambo yawe sawasawa; wakati huu wa sasa wingi wenu uwafae upungufu wao, ili na wingi wao uwafae ninyi mtakapopungukiwa; ili mambo yawe sawasawa. 2 Wakorintho 8:14

but for equality. Your abundance at this present time supplies their lack, that their abundance also may become a supply for your lack; that there may be equality.

Kama ilivyoandikwa, Aliyekusanya vingi, hakuzidi, wala yeye aliyekusanya vichache hakupungukiwa. 2 Wakorintho 8:15

As it is written, "He who gathered much had nothing left over, and he who gathered little had no lack."

Lakini ahimidiwe Mungu atiaye bidii ile ile kwa ajili yenu katika moyo wa Tito. 2 Wakorintho 8:16

But thanks be to God, who puts the same earnest care for you into the heart of Titus.

Maana aliyapokea kweli yale maonyo; tena, huku akizidi kuwa na bidii, alisafiri kwenda kwenu kwa hiari yake mwenyewe. 2 Wakorintho 8:17

For he indeed accepted our exhortation, but being himself very earnest, he went out to you of his own accord.

Na pamoja naye tukamtuma ndugu yule ambaye sifa zake katika Injili zimeenea makanisani mwote. 2 Wakorintho 8:18

We have sent together with him the brother whose praise in the Gospel is known through all the assemblies.

Wala si hivyo tu, bali alichaguliwa na makanisa asafiri pamoja nasi katika jambo la neema hii, tunayoitumikia, ili Bwana atukuzwe, ukadhihirike utayari wetu. 2 Wakorintho 8:19

Not only so, but who was also appointed by the assemblies to travel with us in this grace, which is served by us to the glory of the Lord himself, and to show our readiness.

Tukijiepusha na neno hili, mtu asije akatulaumu kwa habari ya karama hii tunayoitumikia; 2 Wakorintho 8:20

We are avoiding this, that any man should blame us concerning this abundance which is administered by us.

tukitangulia kufikiri yaliyo mema, si mbele za Bwana tu, ila na mbele ya wanadamu. 2 Wakorintho 8:21

Having regard for honorable things, not only in the sight of the Lord, but also in the sight of men.

Nasi pamoja nao tumemtuma ndugu yetu tuliyemwona mara nyingi katika mambo mengi kuwa ana bidii, na sasa ana bidii zaidi sana kwa sababu ya tumaini kuu alilo nalo kwenu. 2 Wakorintho 8:22

We have sent with them our brother, whom we have many times proved earnest in many things, but now much more earnest, by reason of the great confidence which he has in you.

Basi mtu akitaka habari za Tito, yeye ni mshirika wangu, na mtenda kazi pamoja nami kwa ajili yenu; tena akitaka habari za ndugu zetu, wao ni mitume wa makanisa, na utukufu wa Kristo. 2 Wakorintho 8:23

As for Titus, he is my partner and fellow worker for you. As for our brothers, they are the apostles of the assemblies, the glory of Christ.

Basi waonyesheni mbele ya makanisa hakika ya upendo wenu, na ya kujisifu kwetu kwa ajili yenu. 2 Wakorintho 8:24

Therefore show the proof of your love to them in front of the assemblies, and of our boasting on your behalf.