2 Wakorintho 2 Swahili & English
Listen/Download Audio2 Wakorintho 2 (Swahili) | 2nd Corinthians 2 (English) |
---|---|
Lakini nafsini mwangu nalikusudia hivi, nisije kwenu tena kwa huzuni. 2 Wakorintho 2:1 |
But I determined this for myself, that I would not come to you again in sorrow. |
Maana mimi nikiwatia huzuni, basi ni nani anifurahishaye mimi ila yeye ahuzunishwaye nami? 2 Wakorintho 2:2 |
For if I make you sorry, then who will make me glad but he who is made sorry by me? |
Nami naliwaandikia neno lilo hilo, ili nijapo nisitiwe huzuni na wale ambao ilinipasa kuwafurahia; nikiwatumaini ninyi nyote kwamba furaha yangu ni yenu nyote pia. 2 Wakorintho 2:3 |
And I wrote this very thing to you, so that, when I came, I wouldn't have sorrow from them of whom I ought to rejoice; having confidence in you all, that my joy would be shared by all of you. |
Maana katika dhiki nyingi na taabu ya moyo niliwaandikia na machozi mengi; si kwamba mhuzunishwe, bali mpate kujua upendo wangu nilio nao kwenu jinsi ulivyo mwingi. 2 Wakorintho 2:4 |
For out of much affliction and anguish of heart I wrote to you with many tears, not that you should be made sorry, but that you might know the love that I have so abundantly for you. |
Lakini iwapo mtu amehuzunisha, hakunihuzunisha mimi tu, bali kwa sehemu (nisije nikalemea mno), amewahuzunisha ninyi nyote. 2 Wakorintho 2:5 |
But if any has caused sorrow, he has caused sorrow, not to me, but in part (that I not press too heavily) to you all. |
Yamtosha mtu wa namna hii adhabu ile aliyopewa na walio wengi; 2 Wakorintho 2:6 |
Sufficient to such a one is this punishment which was inflicted by the many; |
hata kinyume cha hayo, ni afadhali mmsamehe na kumfariji, mtu kama huyo asije akamezwa katika huzuni yake ipitayo kiasi. 2 Wakorintho 2:7 |
so that on the contrary you should rather forgive him and comfort him, lest by any means such a one should be swallowed up with his excessive sorrow. |
Kwa hiyo nawasihi kumthibitishia upendo wenu. 2 Wakorintho 2:8 |
Therefore I beg you to confirm your love toward him. |
Maana naliandika kwa sababu hii pia, ili nipate bayana kwenu kwamba mmekuwa wenye kutii katika mambo yote. 2 Wakorintho 2:9 |
For to this end I also wrote, that I might know the proof of you, whether you are obedient in all things. |
Lakini kama mkimsamehe mtu neno lo lote, nami nimemsamehe; kwa maana mimi nami, ikiwa nimemsamehe mtu neno lo lote, nimemsamehe kwa ajili yenu mbele za Kristo, 2 Wakorintho 2:10 |
Now I also forgive whomever you forgive anything. For if indeed I have forgiven anything, I have forgiven that one for your sakes in the presence of Christ, |
Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake. 2 Wakorintho 2:11 |
that no advantage may be gained over us by Satan; for we are not ignorant of his schemes. |
Basi nilipofika Troa kwa ajili ya Injili ya Kristo, nikafunguliwa mlango katika Bwana, 2 Wakorintho 2:12 |
Now when I came to Troas for the Gospel of Christ, and when a door was opened to me in the Lord, |
sikuona raha nafsini mwangu, kwa sababu sikumwona Tito ndugu yangu, bali niliagana nao, nikaondoka kwenda Makedonia. 2 Wakorintho 2:13 |
I had no relief for my spirit, because I didn't find Titus, my brother, but taking my leave of them, I went out into Macedonia. |
Ila Mungu ashukuriwe, anayetushangiliza daima katika Kristo, na kuidhihirisha harufu ya kumjua yeye kila mahali kwa kazi yetu. 2 Wakorintho 2:14 |
Now thanks be to God, who always leads us in triumph in Christ, and reveals through us the sweet aroma of his knowledge in every place. |
Kwa maana sisi tu manukato ya Kristo, mbele za Mungu, katika wao wanaookolewa, na katika wao wanaopotea; 2 Wakorintho 2:15 |
For we are a sweet aroma of Christ to God, in those who are saved, and in those who perish; |
katika hao wa pili harufu ya mauti iletayo mauti; katika hao wa kwanza harufu ya uzima iletayo uzima. Naye ni nani atoshaye kwa mambo hayo? 2 Wakorintho 2:16 |
to the one a stench from death to death; to the other a sweet aroma from life to life. Who is sufficient for these things? |
Kwa maana sisi si kama walio wengi, walighoshio neno la Mungu; bali kama kwa weupe wa moyo, kama kutoka kwa Mungu, mbele za Mungu, twanena katika Kristo. 2 Wakorintho 2:17 |
For we are not as so many, peddling the word of God. But as of sincerity, but as of God, in the sight of God, we speak in Christ. |