1 Petro 2 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Petro 2 (Swahili) 1st Peter 2 (English)

Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote. 1 Petro 2:1

Putting away therefore all wickedness, all deceit, hypocrisies, envies, and all evil speaking,

Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu; 1 Petro 2:2

as newborn babes, long for the pure milk of the Word, that you may grow thereby,

ikiwa mmeonja ya kwamba Bwana ni mwenye fadhili. 1 Petro 2:3

if indeed you have tasted that the Lord is gracious:

Mmwendee yeye, jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima. 1 Petro 2:4

coming to him, a living stone, rejected indeed by men, but chosen by God, precious.

Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo. 1 Petro 2:5

You also, as living stones, are built up as a spiritual house, to be a holy priesthood, to offer up spiritual sacrifices, acceptable to God through Jesus Christ.

Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, Na kila amwaminiye hatatahayarika. 1 Petro 2:6

Because it is contained in Scripture, "Behold, I lay in Zion a chief cornerstone, chosen, and precious: He who believes in him will not be disappointed."

Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini, Jiwe walilolikataa waashi, Limekuwa jiwe kuu la pembeni. 1 Petro 2:7

For you therefore who believe is the honor, but for such as are disobedient, "The stone which the builders rejected, Has become the chief cornerstone,"

Tena, Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha, Kwa maana hujikwaza kwa neno lile,wasiliamini,nao waliwekwa kusudi wapate hayo. 1 Petro 2:8

and, "A stone of stumbling, and a rock of offense." For they stumble at the word, being disobedient, whereunto also they were appointed.

Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu; 1 Petro 2:9

But you are a chosen race, a royal priesthood, a holy nation, a people for God's own possession, that you may show forth the excellencies of him who called you out of darkness into his marvelous light:

ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema. 1 Petro 2:10

who in time past were no people, but now are God's people, who had not obtained mercy, but now have obtained mercy.

Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho. 1 Petro 2:11

Beloved, I beg you as foreigners and pilgrims, to abstain from fleshly lusts, which war against the soul;

Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa. 1 Petro 2:12

having good behavior among the nations, so in that which they speak against you as evil-doers, they may by your good works, which they see, glorify God in the day of visitation.

Tiini kila kiamriwacho na watu, kwa ajili ya Bwana; ikiwa ni mfalme, kama mwenye cheo kikubwa; 1 Petro 2:13

Therefore subject yourselves to every ordinance of man for the Lord's sake: whether to the king, as supreme;

ikiwa ni wakubwa, kama wanaotumwa naye ili kuwalipiza kisasi watenda mabaya na kuwasifu watenda mema. 1 Petro 2:14

or to governors, as sent by him for vengeance on evil-doers and for praise to those who do well.

Kwa sababu ndiyo mapenzi ya Mungu, kwamba kwa kutenda mema mzibe vinywa vya ujinga vya watu wapumbavu; 1 Petro 2:15

For this is the will of God, that by well-doing you should put to silence the ignorance of foolish men:

kama walio huru, ila wasioutumia uhuru huo kwa kusitiri ubaya, bali kama watumwa wa Mungu. 1 Petro 2:16

as free, and not using your freedom for a cloak of wickedness, but as bondservants of God.

Waheshimuni watu wote. Wapendeni ndugu. Mcheni Mungu. Mpeni heshima mfalme. 1 Petro 2:17

Honor all men. Love the brotherhood. Fear God. Honor the king.

Enyi watumishi, watiini bwana zenu kwa hofu nyingi, sio wao walio wema na wenye upole tu, bali nao walio wakali. 1 Petro 2:18

Servants, be in subjection to your masters with all fear; not only to the good and gentle, but also to the wicked.

Maana huu ndio wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo isivyo haki. 1 Petro 2:19

For it is commendable if someone endures pain, suffering unjustly, because of conscience toward God.

Kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu. 1 Petro 2:20

For what glory is it if, when you sin, you patiently endure beating? But if, when you do well, you patiently endure suffering, this is commendable with God.

Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake. 1 Petro 2:21

For to this you were called, because Christ also suffered for us, leaving you{TR reads "us" instead of "you"} an example, that you should follow his steps,

Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake. 1 Petro 2:22

who did not sin, "neither was deceit found in his mouth."

Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakuogofya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki. 1 Petro 2:23

Who, when he was cursed, didn't curse back. When he suffered, didn't threaten, but committed himself to him who judges righteously;

Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa. 1 Petro 2:24

who his own self bore our sins in his body on the tree, that we, having died to sins, might live to righteousness; by whose stripes you were healed.

Kwa maana mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu. 1 Petro 2:25

For you were going astray like sheep; but are now returned to the Shepherd and Overseer{"Overseer" is from the Greek episkopon, which can mean overseer, curator, guardian, or superintendent.} of your souls.