1 Petro 2 Swahili & English
Listen/Download Audio1 Petro 2 (Swahili) | 1st Peter 2 (English) |
---|---|
Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote. 1 Petro 2:1 |
Putting away therefore all wickedness, all deceit, hypocrisies, envies, and all evil speaking, |
Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu; 1 Petro 2:2 |
as newborn babes, long for the pure milk of the Word, that you may grow thereby, |
ikiwa mmeonja ya kwamba Bwana ni mwenye fadhili. 1 Petro 2:3 |
if indeed you have tasted that the Lord is gracious: |
Mmwendee yeye, jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima. 1 Petro 2:4 |
coming to him, a living stone, rejected indeed by men, but chosen by God, precious. |
Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo. 1 Petro 2:5 |
You also, as living stones, are built up as a spiritual house, to be a holy priesthood, to offer up spiritual sacrifices, acceptable to God through Jesus Christ. |
Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, Na kila amwaminiye hatatahayarika. 1 Petro 2:6 |
Because it is contained in Scripture, "Behold, I lay in Zion a chief cornerstone, chosen, and precious: He who believes in him will not be disappointed." |
Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini, Jiwe walilolikataa waashi, Limekuwa jiwe kuu la pembeni. 1 Petro 2:7 |
For you therefore who believe is the honor, but for such as are disobedient, "The stone which the builders rejected, Has become the chief cornerstone," |
Tena, Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha, Kwa maana hujikwaza kwa neno lile,wasiliamini,nao waliwekwa kusudi wapate hayo. 1 Petro 2:8 |
and, "A stone of stumbling, and a rock of offense." For they stumble at the word, being disobedient, whereunto also they were appointed. |
Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu; 1 Petro 2:9 |
But you are a chosen race, a royal priesthood, a holy nation, a people for God's own possession, that you may show forth the excellencies of him who called you out of darkness into his marvelous light: |
ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema. 1 Petro 2:10 |
who in time past were no people, but now are God's people, who had not obtained mercy, but now have obtained mercy. |
Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho. 1 Petro 2:11 |
Beloved, I beg you as foreigners and pilgrims, to abstain from fleshly lusts, which war against the soul; |
Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa. 1 Petro 2:12 |
having good behavior among the nations, so in that which they speak against you as evil-doers, they may by your good works, which they see, glorify God in the day of visitation. |
Tiini kila kiamriwacho na watu, kwa ajili ya Bwana; ikiwa ni mfalme, kama mwenye cheo kikubwa; 1 Petro 2:13 |
Therefore subject yourselves to every ordinance of man for the Lord's sake: whether to the king, as supreme; |
ikiwa ni wakubwa, kama wanaotumwa naye ili kuwalipiza kisasi watenda mabaya na kuwasifu watenda mema. 1 Petro 2:14 |
or to governors, as sent by him for vengeance on evil-doers and for praise to those who do well. |
Kwa sababu ndiyo mapenzi ya Mungu, kwamba kwa kutenda mema mzibe vinywa vya ujinga vya watu wapumbavu; 1 Petro 2:15 |
For this is the will of God, that by well-doing you should put to silence the ignorance of foolish men: |
kama walio huru, ila wasioutumia uhuru huo kwa kusitiri ubaya, bali kama watumwa wa Mungu. 1 Petro 2:16 |
as free, and not using your freedom for a cloak of wickedness, but as bondservants of God. |
Waheshimuni watu wote. Wapendeni ndugu. Mcheni Mungu. Mpeni heshima mfalme. 1 Petro 2:17 |
Honor all men. Love the brotherhood. Fear God. Honor the king. |
Enyi watumishi, watiini bwana zenu kwa hofu nyingi, sio wao walio wema na wenye upole tu, bali nao walio wakali. 1 Petro 2:18 |
Servants, be in subjection to your masters with all fear; not only to the good and gentle, but also to the wicked. |
Maana huu ndio wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo isivyo haki. 1 Petro 2:19 |
For it is commendable if someone endures pain, suffering unjustly, because of conscience toward God. |
Kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu. 1 Petro 2:20 |
For what glory is it if, when you sin, you patiently endure beating? But if, when you do well, you patiently endure suffering, this is commendable with God. |
Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake. 1 Petro 2:21 |
For to this you were called, because Christ also suffered for us, leaving you{TR reads "us" instead of "you"} an example, that you should follow his steps, |
Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake. 1 Petro 2:22 |
who did not sin, "neither was deceit found in his mouth." |
Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakuogofya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki. 1 Petro 2:23 |
Who, when he was cursed, didn't curse back. When he suffered, didn't threaten, but committed himself to him who judges righteously; |
Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa. 1 Petro 2:24 |
who his own self bore our sins in his body on the tree, that we, having died to sins, might live to righteousness; by whose stripes you were healed. |
Kwa maana mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu. 1 Petro 2:25 |
For you were going astray like sheep; but are now returned to the Shepherd and Overseer{"Overseer" is from the Greek episkopon, which can mean overseer, curator, guardian, or superintendent.} of your souls. |