1 Petro 4 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Petro 4 (Swahili) 1st Peter 4 (English)

Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi. 1 Petro 4:1

Forasmuch then as Christ suffered for us in the flesh, arm yourselves also with the same mind; for he who has suffered in the flesh has ceased from sin;

Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani. 1 Petro 4:2

that you no longer should live the rest of your time in the flesh for the lusts of men, but for the will of God.

Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali; 1 Petro 4:3

For we have spent enough of our past time doing the desire of the Gentiles, and having walked in lewdness, lusts, drunken binges, orgies, carousings, and abominable idolatries.

mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana. 1 Petro 4:4

They think it is strange that you don't run with them into the same excess of riot, blaspheming:

Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa. 1 Petro 4:5

who will give account to him who is ready to judge the living and the dead.

Maana kwa ajili hiyo hata hao waliokufa walihubiriwa Injili, ili kwamba wahukumiwe katika mwili kama wahukumiwavyo wanadamu; bali wawe hai katika roho kama Mungu alivyo hai. 1 Petro 4:6

For to this end was the Gospel preached even to the dead, that they might be judged indeed as men in the flesh, but live as to God in the spirit.

Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili, mkeshe katika sala. 1 Petro 4:7

But the end of all things is near. Therefore be of sound mind, self-controlled, and sober in prayer.

Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi. 1 Petro 4:8

And above all things be earnest in your love among yourselves, for love covers a multitude of sins.

Mkaribishane ninyi kwa ninyi, pasipo kunung'unika; 1 Petro 4:9

Be hospitable one to another without grumbling.

kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu. 1 Petro 4:10

According as each has received a gift, be ministering it among yourselves, as good stewards of the grace of God in its various forms.

Mtu akisema, na aseme kama mausia ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina. 1 Petro 4:11

If any man speaks, let it be as it were oracles of God. If any man serves, let it be as of the strength which God supplies, that in all things God may be glorified through Jesus Christ, to whom belong the glory and the dominion forever and ever. Amen.

Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho. 1 Petro 4:12

Beloved, don't be astonished at the fiery trial which has come upon you, to test you, as though a strange thing happened to you.

Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe. 1 Petro 4:13

But because you are partakers of Christ's sufferings, rejoice; that at the revelation of his glory also you may rejoice with exceeding joy.

Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia. 1 Petro 4:14

If you are insulted for the name of Christ, blessed are you; because the Spirit of glory and of God rests on you. On their part he is blasphemed, but on your part he is glorified.

Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine. 1 Petro 4:15

For let none of you suffer as a murderer, or a thief, or an evil doer, or as a meddler in other men's matters.

Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo. 1 Petro 4:16

But if one of you suffers for being a Christian, let him not be ashamed; but let him glorify God in this matter.

Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya Mungu; na ikianza kwetu sisi, mwisho wao wasioitii injili ya Mungu utakuwaje? 1 Petro 4:17

For the time has come for judgment to begin at the house of God. If it begins first with us, what will happen to those who don't obey the Gospel of God?

Na mwenye haki akiokoka kwa shida, yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi ataonekana wapi? 1 Petro 4:18

"If it is hard for the righteous to be saved, what will happen to the ungodly and the sinner?"

Basi wao wateswao kwa mapenzi ya Mungu na wamwekee amana roho zao, katika kutenda mema, kama kwa Muumba mwaminifu. 1 Petro 4:19

Therefore let them also who suffer according to the will of God in doing good entrust their souls to him, as to a faithful Creator.